Lundenga: Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu ni miss halali mwenye vigezo vyote

GIBA KB

JF-Expert Member
Jul 3, 2012
367
110
10305180_1056198341061250_1640188852373839142_n.jpg


Muda mfupi uliopita,Lundenga akiongea na waandishi wa habari amesema Miss TZ 2014-2015 ana miaka 23 na hana masters ana degree.Kwa maelezo hayo anafaa kuwa miss Tz na hatavuliwa taji.

Mwaka 2005 kulikua na ushindani kidogo, mwaka 2006 kulikua na ushindani wa Wema na Jokate na upinzani huu umeendelea kuwepo kwenye mashindano yetu lakini ya mwaka huu imezidi mno, kumekua na matusi.kashfa na hata naona wamevuka mpaka na kuingiza mambo ya kisiasa ambayo sisi hatuyapendi, huu ni mchezo kama mchezo mwingine wowote… yani taji la mwaka mmoja limefunika mpaka katiba na Simba na Yanga?

Hayo ni maelezo aliyoyatoa Mr. Hasheem Lundenga mbele ya Waandishi wa habari Dar es salaam October 21 2014 kuhusu ishu ya Miss Tanzania ambae aliandikwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mrembo huyu kudanganya umri, elimu na mambo mengine.

Yafuatayo ni mambo waliyoyasema Hasheem Lundenga na Miss Tanzania Sitti.

‘Walidai kwamba Miss Tanzania ana mtoto baada ya kutoka picha moja akiwa na mtoto, nasema katika utafiti wetu sisi Miss Tanzania hana mtoto na mwenye vithibitisho halali kwamba ana mtoto atuletee, kama kuna uthibitisho wa cheti cha kuzaliwa cha mtoto….. leta hicho cheti'– Lundenga

‘Hili la sisi kuchukua rushwa kutoka kwa baba wa Sitti, Abbas Mtemv.jamani hii ni stori ya kijingajinga, ni mambo ya kipumbavu sana kuandika haya mambo, hamjui taratibu zetu tunavyowapata majaji na wanavyofanya kazi…Majaji huwa wanatafutwa siku nne za mwisho na huwa hakuna mtu anajua atakua Jaji na huwa tupeleka majina 15 BASATA na wao ndio wanaturudishia majina tisa ya Majaji waliopitishwa' – Lundenga

Magazeti mbalimbali yameripoti kwamba Sitti alikua na Masters, ukweli ni kwamba katika fomu tulizonazo sisi Sitti hajaandika hata sehemu moja kwamba amesoma mpaka Masters, swala la Masters limetoka wapi? ni uongo huo' - Lundenga

‘Kuhusu swala la yeye kuzungumza kifaransa, mtu anajua lugha ya kimataifa mbona kwenye mashindano ya dunia wanazungumza Kifaransa na lugha nyingine? lakini mbona hata kwenye fainali alijibu kwa Kiingereza pia? Kifaransa zilikua ni mbwembwe kuwashawishi Majaji, na kweli walishawishika na ndio maana akashinda' – Lundenga

‘Jingine ambalo ni kubwa zaidi ni swala la umri lililozungumzwa sana, katika mashindano yetu washiriki wote hujaza fomu na kuandika tarehe ya kuzaliwa, fomu ya Sitti hii hapa na inaonyesha amezaliwa May 31 1991 kwa hiyo alitimiza masharti ya kushiriki kwa kuwa ana umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 24′ – Lundenga

‘Wote walioshiriki Miss Tanzania 2014 akiwemo Sitti walituletea vyeti vyao Original vya kuzaliwa tarehe 13 na kisha tukatoa nakala kupitia hivyo vyeti vyao Original' – Lundenga

‘Sisi kazi yetu sio kupeleleza sana, tukipata information chache zinatutosha… kama mtu anatatizo na hiki cheti cha Sitti cha kuzaliwa akafanye utafiti, ukipata ukweli tuletee sisi lakini kazi ya uchunguzi sio ya kwetu' – Lundenga

Baada ya Lundenga kuongea, Miss Tanzania 2014 Sitti nae aliongea machache kwamba ni kweli ana umri wa miaka 23 vilevile cheti chake cha kuzaliwa kilipotea sababu amekua akisafiri mara kwa mara' -Sitti

Waandishi wa habari walipotaka awaambie na uthibitisho kama aliripoti Polisi kuhusu kupotea kwa cheti chake, Sitti alisema ‘sikutegemea haya maswali leo kwahiyo sikuja nimejiandaa kihivyo, kama mtakua mnahitaji kunihoji mnaweza kupanga siku yenu na mkanihoji' – Sitti

Kuhusu yeye kuwa na mtoto Sitti amejibu kwa ufupi kwa kusema >>> ‘Nadhani inajieleza kama Muheshimiwa alivyosema kwamba sina mtoto na mkitaka tunaweza kwenda Hospitali kwa sababu naona kama mnaniandama kwa vitu ambavyo sio vya kweli'

Kuhusu ukweli kama hati ya kusafiria pamoja na leseni ya gari vilivyosambazwa mitandaoni ni kweli vikionyesha kwamba amezaliwa mwaka 1989, Sitti amesema ‘Sitogusia hilo swala sababu nilivyokua nakuja kuomba Miss Tanzania niliomba cheti cha kuzaliwa, hivyo vitu vingine ni maisha binafsi…. kwahiyo sidhani kama na nyie mngependa kuona mtu anachukua leseni ya gari au Passport iwe ya kweli ama feki na kuiweka kwenye mtandao'


Chanzo: millardayo.com


Post update : Video

Tujikumbushie kile ambacho amesema mrembo wetu 'Kihiyo' Sitti Mtemvu

http://www.youtube.com/watch?v=OdFexQC8U10

MISS TANZANIA 2014,SITTI MTEMVU - YouTube
 
je, ameleta vielelezo gani katika kuthibitisha hayo aliyoyasema!?
 
Mbona hajatoa hoja za kutu convince kuwa hajamuuzia taji kama inavyosemekana.Au wewe mleta mada ndo hujatuainishia vizuri.Ushahidi tafadhali.
 
He he he raha jamani' watu wameweka Document kama vithibitisho yeye analeta maneno' Doc speak for itself' miss alikua anaona rahaaa kujaza jaza pasport' leseni ya mbele na kujiweka weka mtandaoni pasipo kuwa na malengo. Brother Hashimu amebugi thic tym
 
heee kwa hiyo ametoa maneno matupu bila evidence yoyote na wanahabari wakakubali??? so ile paspot na lesen imefojiwa??? sasa hapo si alipaswa kuonesha original jamani??? mmmmmh!!! makubwa haya
 
Huyu msichana lazima ana birth certificate. Iko wapi? Ina maana mamaake mzazi ni mwongo?
 
Lundenga amesema hakuna suala la yeye kupewa rushwa, ila Sitti Mtemvu ameshinda kihalali kwa kupitishwa na Majaji.
Juu ya tuhuma za unene amesema wao huwa hawaangalii wembamba wala ufupi, muhimu ni awe na vigezo vinavyotakiwa.
Kuhusu suala la passport na leseni zikionesha Sitti amezaliwa 1989, Lundenga amesema wao huwa hawangaali vitu hivyo.
Lundenga amesema kuwa cheti halali walichonacho wao ni kile kinachoonesha Sitti Mtemvu kazaliwa 24 mei 1991.
Nafungua mjadala miss TZ 2014.
 
kitendo tu chakusema alikua na miaka 18 then tukaja kujua ana 23 tayari alikua keshapoteza sifa. kama miaka 23 anasifa yakugombea why alisema ana 18? poor us...
 
Back
Top Bottom