CCM wataendelea na hizi sarakasi na hii midundo mpaka 2025.... mtashangaa wanakwenda kwenye chaguzi wakiwa nguvu moja wanashinda tunaanza tena oooooh tumeibiwa kura...
Upinzani wanacheza ngoma ya CCM kila inavyopigwa hahaahahahah
 
Salaam Wakuu,

Aliyekuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi na Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, wametakiwa kwenda Ikulu kumsaidia kazi Rais Samia ya kuwasimamia Mawaziri.


Rais Samia kasema watu Wasimpake matope Lukuvi. Wala Wasimsingizie kwamba anaenda kugombea Uspika bali Wamuache amsaidie kazi Ikulu ya Kusimamia hawa Mawaziri Vijana aliowateua.

"Wengine wameanza kumletea [William Lukuvi] meseji za ajabu ajabu wakijua atagombea Uspika, hatogombea. Ana kazi na mimi. Kaka yangu Lukuvi, yeye ana kazi na mimi, mtaisikia baadaye. Lakini namvuta Ikulu, kazi yetu ni kuwasimamia nyinyi.kasema Rais Samia

Rais Samia amesema Kabudi atakuwa na Kazi moja tu Ikulu, Kusimamia kupitia na Kushughulikia Mikataba yote ambayo Serikali inaingia.

"Kabudi amefanya kazi nzuri sana kusimamia majadiliano ya serikali na mashirika, na ndiyo kazi ninayotaka nimkabidhi sasa kindakindaki...Mashirika yote, kazi zote zitakazoingia ubia na serikali, Kabudi ataongoza hiyo timu. Kwa hiyo yeye ni baba mikataba." amesema Rais Samia Suluhu

Amesema hizi kazi hazipo kwenye Muundo wa Serikali lakini anaona ni Msaada Mkubwa Kwake.

MY TAKE:

Je, Kassim Majaliwa na Mkuchika Wameshindwa kumsaidia rais? Kwanini Lukuvi na Kabudi wawe juu yao?

Kapteni George Huruma Mkuchika yeye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) na Waziri Mkuu ni msimamizi wa shughuli zote za serikali katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anawakilisha serikali katika bunge la taifa. Yuko chini ya mamlaka ya rais.

Kama Babangida wa Nigeria aliitwa Maradona, basi napendekeza mama tumbatize MESSY!
1641880131300.png
 
Kama kawaida yao Chaga gang walikuwa wameshaanza kuwanyemelea ili wawe wagombea wao wa urais 2025.

CCM kuing'oa madarakani kwa hivi vyama uchwara vya siasa itachukua miaka 2000, Unapohisi na kudhani kuwa CCM wanaenda kugombana hapo hapo wanaunda umoja wenye nguvu. Hiki ndo kitaifanya CCM itawale Karne na Karne.

Samia Ni master plan,kumwangusha itachukua muda Sana ,Samia for 2025-2030.

Long live CCM!! Long live Samia

#kazi iendelee
Kidumu chama cha mapinduzi
 
Tena Mama ana sitara kubwa sana
Aliepita alikuwa anafukuza kama mbwa na waliogopa
Wengine walizimia na wengine kufa kabisa baada ya kutumbuliwa

Acha wapige kelele mziki bado sana
Hawa ndio binaadam mkuu.

Hawana jema hawa! Juzi juzi kulikuwa na msemo wa "usitufokee"

Walikuwa wakifokewa na kutukanwa huku watoto wao wanaangalia kwenye TV,Leo wamepata mtu msikivu mstaarabu wanachonga ngenga
 
Kazi ya kusimamia mawaziri ni ya PM - Kassimu akae mkao wa kunyolewa! Bunge likishapata Spika, hiyo kazi ya Lukuvi ya usimamizi wa mawaziri inaanza rasmi kwa jina lake kupelekwa Bungeni kuthibitishwa!!!
Thubutu yakeeeeee.

Lukuvi akatubu Zanzibar kwanza. Aende mpaka Makunduchi akaombe radhi
 
Umewaza pamoja na mimi, kusema anawaweka ikuku iliwamsaidie kazi, hiyo ndio maana yake sababu kila wizara ina mtendaji wake mkuu anaeripoti kwake.

Mwanasheria mkuu wa serikali na waziri mkuu wanatosha kabisa kufanya hizo kazi alizowapa hao kina kabudi na lukuvi.

Pia barazalote la mawaziri kaziyao nikumshauri rais pia.

Sasa hawa anaokwenda kukaanao ikulu manayake niuraisi shirikishi,itakuwa utatu mtakatifu hahahahaaa.

Ila kama atawatumia vizuri kwa haki na ukweli,hawa watu wanaenda kumsidia rais mawazo na maamuzi bora kabisa kwa ustawi wa taifa.
Binasfi namuamini sana kabudi na pia Lukuvi ni mtu smart na asietaka ujinga ujinga.
Lukuvi ni mtu smart??
 
Kama Hamjui ni hivi.. Rais ana angali jinsi ya Kuntoa Kasimu Majaliwa ili Luluvi awe PM.. hii ni ya ndani kabisa ninaye andika hapa nineyapata kwa Mtu wa ikulu ndani.. na hiv Karibuni Majaliwa na pigwa chini Lukuvi ana tangazwa PM..

Mark my alert..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Eti ni ya ndani kabisa!!!!!

Jinga kabisa.

Kuandika hujui nani atakupa taarifa za "ndani kabisa"??
 
Hawa ndio binaadam mkuu.

Hawana jema hawa! Juzi juzi kulikuwa na msemo wa "usitufokee"

Walikuwa wakifokewa na kutukanwa huku watoto wao wanaangalia kwenye TV,Leo wamepata mtu msikivu mstaarabu wanachonga ngenga

Mswahili hana jema kila kitu kwake baya tu
Unamshonea kiatu yeye anakuandalia sanda
 
Maza ameona aibu kuwatosa bila sababu ya msingi na kuchagua vijana ambao atawamudu na kufeel conformable kuwaongoza.

Kama Kabudi na Lukuvi wametolewa pale kwa ajili ya uzee wao vipi Mkuchika ambaye yupo toka enzi za Mwinyi/Mkapa bado anaendelea kupeta na yuko beyond 70s ...!!?
 
Back
Top Bottom