Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,495
- 51,089
Majuzi umetoa kauli tata kuhusu umiliki wa ardhi katika ndoa, tumekueleza kuwa uwe makini na kaulikauli hizi.
Kisha naona unatoa kauli nyingine kutishiatishia wananchi kutwaa ardhi zao.
Ni hivi ndugu Lukuvi, sisi wananchi hatupendi stress, kutishwatishwa, kusukumwasukumwa, kupelekwapelekwa.
Kama ardhi tunazimiliki kihalali, wewe tulia ofisini uje na mawazo yenye tija juu ya namna ya kuboresha umiliki wa ardhi, kuboresha masuala ya mipango miji. Lakini siyo kila ukiamka unaanza kutupigapiga mikwara, mara hili mara lile.
Lukuvi kwani ukikaa ofisini ukapanga mipango mizuri ya wizara unaona hiyo ni kazi ngumu isipokuwa kutishatisha wananchi kunyang'anya ardhi zao?
Najua serikali inataka kodi ya ardhi kama chanzo cha kodi, lakini katika kipindi hiki cha December ambapo wananchi tuna mambo mengi yanayohitaji pesa unakuja kupushpushwananchi utadhani askari Magereza anavyopush wafungwa hayo mambo sisi wananchi hatuyataki!
Lukuvi Kama umedhamiria kufuta hati za wananchi, Au kunyang'anya mali za wananchi hebu fuata sheria, haya mambo ya kupelekeshanapelekeshana hatutaki.
Hivi nyie viongozi, mtaanza lini kuheshimu wananchi badala ya kujiimpose juu yetu utadhani nyie ni manyapara wetu?
Lukuvi awamu hii umeanza na mguu mbaya, hebu tuliza ball kwanza, Mambo ya msingi hayataki manguvunguvu. Tuliza mshono, achana na mawazo ya unyang'anyinyang'anyi, fanya kazi zenye tija!
Kisha naona unatoa kauli nyingine kutishiatishia wananchi kutwaa ardhi zao.
Ni hivi ndugu Lukuvi, sisi wananchi hatupendi stress, kutishwatishwa, kusukumwasukumwa, kupelekwapelekwa.
Kama ardhi tunazimiliki kihalali, wewe tulia ofisini uje na mawazo yenye tija juu ya namna ya kuboresha umiliki wa ardhi, kuboresha masuala ya mipango miji. Lakini siyo kila ukiamka unaanza kutupigapiga mikwara, mara hili mara lile.
Lukuvi kwani ukikaa ofisini ukapanga mipango mizuri ya wizara unaona hiyo ni kazi ngumu isipokuwa kutishatisha wananchi kunyang'anya ardhi zao?
Najua serikali inataka kodi ya ardhi kama chanzo cha kodi, lakini katika kipindi hiki cha December ambapo wananchi tuna mambo mengi yanayohitaji pesa unakuja kupushpushwananchi utadhani askari Magereza anavyopush wafungwa hayo mambo sisi wananchi hatuyataki!
Lukuvi Kama umedhamiria kufuta hati za wananchi, Au kunyang'anya mali za wananchi hebu fuata sheria, haya mambo ya kupelekeshanapelekeshana hatutaki.
Hivi nyie viongozi, mtaanza lini kuheshimu wananchi badala ya kujiimpose juu yetu utadhani nyie ni manyapara wetu?
Lukuvi awamu hii umeanza na mguu mbaya, hebu tuliza ball kwanza, Mambo ya msingi hayataki manguvunguvu. Tuliza mshono, achana na mawazo ya unyang'anyinyang'anyi, fanya kazi zenye tija!