SubiriJibu
JF-Expert Member
- Jun 26, 2009
- 1,803
- 1,863
William Lukuvi leo mchana wakati anafanya rewinding kujibu hoja za wabunge ameeleza jambo moja kwamba wabunge wa CCM wasitishwe na kitendo cha wapinzani kuzunguka sasa nchi nzima.
Lukuvi inaelekea alikuwa anajibu hoja wanayoulizwa kwamba "mbona nyinyi CCM hamzunguki wakati wenzenu wanazunguka nchi nzima".
Katika majibu yake Lukuvi kaeleza kwamba wao CCM hawazunguki kwa sababu wana kazi ya kufanya. Wao ndiyo wameshikilia serikali na hivyo wako kazini. Wasio na kazi waache wazunguke na huko wanakozunguka watakuta matatito ambayo hawawezi kuyatatua bali watayaleta tena kwenye serikali ya CCM iyatatue.
Ni kweli CCM ndiyo iko serikalini.
Sijui kama Lukuvi aliwasiliana na watu kama Nape Nnauye. Kwani wao wenyewe humo ndani ya CCM wamelaumiana kwamba Nape kazi yake ni kuzunguka mara kuwapaka wengine matope, mara kuwaita watu mafisadi, mara kuwaambia watu kuwa wajivue magamba. Yote hayo ni hukohuko ndani ya CCM.
Lakini kazi nyingine anayofanya Nape na wenzake ni kuzunguka walikotoka wapinzani iwe kimaeneo au kikauli. Kikauli ameanza siku hizi. Wenzake wamebuni VUA GAMBA VAA GWANDA yeye kaiga kwa kusema VUA GWANDA VAA UZALENDO. Hiyo ndiyo CCM. Kila mmoja na kaui yake maadam imetoka ubongoni ikateremka mdomoni.
Lakini Lukuvi kama walivyo wana CCM wengi wanadhani bado tu wepesi wa kusahau. Lukuvi anasahau kwamba Bunge la Bajeti mwaka 2007 lilipoisha Serikali ilituma Mawaziri wazunguke mikoani kuhubiri umuhimu wa Bajeti. Ni kipindi kile ambacho Zitto kabwe kafungiwa miezi kadhaa na akatumia kifungo hicho kuzunguka huku na kule kama Godbless Lema anavyofanya sasa.
Kilichotokea ni kwamba mawaziri hao walizunguka lakini wakaishia kuwa wanazomewa ovyo. Matokeo ya kuzomewa tumeyaona, kidogo nchi iwachomoke 2010.
Sasa, Lukuvi inawezekana kasahau na anafikiri na sisi tunasahau. Anasahau kwamba kuna kitu inaitwa Jamii Forum na mitandao mingine anayoiogopa inakumbushana kila leo na inachambua kila kauli wanayotoa.
Hivyo, Lukuvi lete kauli nyingine hii umepitwa na hoja. bahat nzuri mawaziri siku hizi mnaangalia JF kila mpatapo nafasi. Hivyo, wakati mnarudi mjengoni jioni leo jua kwamba wananachi tayari tumeshatoa tamko letu kama hili mitandaoni na kauli zenu zinapata majibu palepale hukuhuku mitandaoni mapema ndani ya dakika chache.
Lukuvi inaelekea alikuwa anajibu hoja wanayoulizwa kwamba "mbona nyinyi CCM hamzunguki wakati wenzenu wanazunguka nchi nzima".
Katika majibu yake Lukuvi kaeleza kwamba wao CCM hawazunguki kwa sababu wana kazi ya kufanya. Wao ndiyo wameshikilia serikali na hivyo wako kazini. Wasio na kazi waache wazunguke na huko wanakozunguka watakuta matatito ambayo hawawezi kuyatatua bali watayaleta tena kwenye serikali ya CCM iyatatue.
Ni kweli CCM ndiyo iko serikalini.
Sijui kama Lukuvi aliwasiliana na watu kama Nape Nnauye. Kwani wao wenyewe humo ndani ya CCM wamelaumiana kwamba Nape kazi yake ni kuzunguka mara kuwapaka wengine matope, mara kuwaita watu mafisadi, mara kuwaambia watu kuwa wajivue magamba. Yote hayo ni hukohuko ndani ya CCM.
Lakini kazi nyingine anayofanya Nape na wenzake ni kuzunguka walikotoka wapinzani iwe kimaeneo au kikauli. Kikauli ameanza siku hizi. Wenzake wamebuni VUA GAMBA VAA GWANDA yeye kaiga kwa kusema VUA GWANDA VAA UZALENDO. Hiyo ndiyo CCM. Kila mmoja na kaui yake maadam imetoka ubongoni ikateremka mdomoni.
Lakini Lukuvi kama walivyo wana CCM wengi wanadhani bado tu wepesi wa kusahau. Lukuvi anasahau kwamba Bunge la Bajeti mwaka 2007 lilipoisha Serikali ilituma Mawaziri wazunguke mikoani kuhubiri umuhimu wa Bajeti. Ni kipindi kile ambacho Zitto kabwe kafungiwa miezi kadhaa na akatumia kifungo hicho kuzunguka huku na kule kama Godbless Lema anavyofanya sasa.
Kilichotokea ni kwamba mawaziri hao walizunguka lakini wakaishia kuwa wanazomewa ovyo. Matokeo ya kuzomewa tumeyaona, kidogo nchi iwachomoke 2010.
Sasa, Lukuvi inawezekana kasahau na anafikiri na sisi tunasahau. Anasahau kwamba kuna kitu inaitwa Jamii Forum na mitandao mingine anayoiogopa inakumbushana kila leo na inachambua kila kauli wanayotoa.
Hivyo, Lukuvi lete kauli nyingine hii umepitwa na hoja. bahat nzuri mawaziri siku hizi mnaangalia JF kila mpatapo nafasi. Hivyo, wakati mnarudi mjengoni jioni leo jua kwamba wananachi tayari tumeshatoa tamko letu kama hili mitandaoni na kauli zenu zinapata majibu palepale hukuhuku mitandaoni mapema ndani ya dakika chache.