LUKUVI AWAPA HATI ZA KUMILIKI ARDHI WA HADZABE

Maboso

JF-Expert Member
Feb 18, 2013
5,164
5,761
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amewapatia hati miliki za Ardhi kwa jamii ya wa Hadzabe wanaoishi wilayani Karatu Mkoani Arusha.

Waziri Lukuvi amefika katika maeneo yao na kuwapa hati miliki za kimila kwa vijiji na wanayoishi jamii ya wa Hadzabe na jamii nyingine za kifugaji ili kulinda maeneo yao ya malisho na maeneo wanayotumia kuwinda wanyama.

Jamii ya wa Hadzabe ni watu ambao huishi kwa mfumo wa maisha ya kuwinda, kufuga wanyama pori na kula mimea na matunda ya miti inayowazunguka. Jamii hii kwa miaka mingi imekuwa ikiishi bila kufuata mipaka ya maeneo yao na hivyo kusababisha migogoro ya ardhi kwa jamii nyingine zinazoishi karibu na maeneo yao.


Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwapatia hati miliki za Ardhi kwa jamii ya wa Hadzabe wanaoishi wilayani Karatu Mkoani Arusha.

Pamoja na ziara hiyo Mhe. William Lukuvi amtatua migogoro ya Ardhi ya wananchi wa wilayani Karatu Mkoani Arusha na wananchi walio na kero za migogoro ya ardhi na kuzipatia ufumbuzi pamoja na kupokea vielelezo vya kero za wananchi walizoziwasilisha kwa Waziri ili azitolee maamuzi.

Wananchi wa vijiji vya Mang’ola juu na Midabini wilayani Karatu Mkoani Arusha walisimamisha msafara wa Mhe. Lukuvi ili awasikilize kero zao za ardhi, ambapo Waziri Lukuvi alisimama na kuzitatua pamoja na kumuagiza Mkuu wa wilaya ya karatu Bibi Therezia Mahongo kutafutia ufumbuzi baadhi ya migogoro hiyo.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi anaendelea na Ziara zake za utatuzi wa Migogoro ya Ardhi nchini, ambayo imejikita zaidi katika kutatua migogoro ya ardhi ya Mikoa ya kanda ya Magharibi, Kaskazini na ile ya Kanda ya Ziwa hapa nchini.

Hadi sasa Mhe. Lukuvi ndani ya mwezi huu wa Desemba ameishatatua migogoro ya ardhi ya Mkoa wa Kigoma na wilaya zake za Kigoma mjini, Kasulu na Kibondo na katika Mkoa wa Shinyanga na wilaya zake za Kishapu na Shinyanga mjini na katika mkoa wa Geita amefanya ziara katika wilayani Chato.

Pia Mhe. Lukuvi ametatua migogoro ya ardhi ya Mkoa wa Mara katika wilaya za Musoma na Bunda ambapo kwa Arusha ametatua migogoro ya wilaya ya Arumeru na Karatu.


Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (wa nne kulia mbele) akiwasili wilayani Karatu kwa ajili ya kuwapatia hati miliki za Ardhi jamii ya wa Hadzabe.


Wa Hadzabe wakimkaribisha Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kwa kumvusha taji.


Wa Hadzabe wakifurahi na Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi baada ya kuwapa hati miliki za Ardhi.


Wakazi wa kijiji cha Midabini wilayani Karatu Mkoani Arusha wakisimamisha msafara wa Mhe. Lukuvi ili awasikilize kero zao za ardhi, ambapo Waziri Lukuvi alisimama na kuzitatua.


Wakazi wa kijiji cha Mang’ola juu wilayani Karatu Mkoani Arusha waliosimamisha msafara wa Mhe. Lukuvi wakimsikiliza wakati akitatua mgogoro wao wa Ardhi.
 
Kafanya vzr maana nao ni watz hivyo wana haki sawa na wengine hususan la kumiliki ardhi
 
safi sana hii wale maharamia wa vitalu kutoka arabuni sasa washapigwa stop maana walitaka watumie mapesa yao kuwaondoa washkaji kwa kisingizio cha kitalu,good job lukuvi
 
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amewapatia hati miliki za Ardhi kwa jamii ya wa Hadzabe wanaoishi wilayani Karatu Mkoani Arusha.

Waziri Lukuvi amefika katika maeneo yao na kuwapa hati miliki za kimila kwa vijiji na wanayoishi jamii ya wa Hadzabe na jamii nyingine za kifugaji ili kulinda maeneo yao ya malisho na maeneo wanayotumia kuwinda wanyama.

Jamii ya wa Hadzabe ni watu ambao huishi kwa mfumo wa maisha ya kuwinda, kufuga wanyama pori na kula mimea na matunda ya miti inayowazunguka. Jamii hii kwa miaka mingi imekuwa ikiishi bila kufuata mipaka ya maeneo yao na hivyo kusababisha migogoro ya ardhi kwa jamii nyingine zinazoishi karibu na maeneo yao.


Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwapatia hati miliki za Ardhi kwa jamii ya wa Hadzabe wanaoishi wilayani Karatu Mkoani Arusha.

Pamoja na ziara hiyo Mhe. William Lukuvi amtatua migogoro ya Ardhi ya wananchi wa wilayani Karatu Mkoani Arusha na wananchi walio na kero za migogoro ya ardhi na kuzipatia ufumbuzi pamoja na kupokea vielelezo vya kero za wananchi walizoziwasilisha kwa Waziri ili azitolee maamuzi.

Wananchi wa vijiji vya Mang’ola juu na Midabini wilayani Karatu Mkoani Arusha walisimamisha msafara wa Mhe. Lukuvi ili awasikilize kero zao za ardhi, ambapo Waziri Lukuvi alisimama na kuzitatua pamoja na kumuagiza Mkuu wa wilaya ya karatu Bibi Therezia Mahongo kutafutia ufumbuzi baadhi ya migogoro hiyo.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi anaendelea na Ziara zake za utatuzi wa Migogoro ya Ardhi nchini, ambayo imejikita zaidi katika kutatua migogoro ya ardhi ya Mikoa ya kanda ya Magharibi, Kaskazini na ile ya Kanda ya Ziwa hapa nchini.

Hadi sasa Mhe. Lukuvi ndani ya mwezi huu wa Desemba ameishatatua migogoro ya ardhi ya Mkoa wa Kigoma na wilaya zake za Kigoma mjini, Kasulu na Kibondo na katika Mkoa wa Shinyanga na wilaya zake za Kishapu na Shinyanga mjini na katika mkoa wa Geita amefanya ziara katika wilayani Chato.

Pia Mhe. Lukuvi ametatua migogoro ya ardhi ya Mkoa wa Mara katika wilaya za Musoma na Bunda ambapo kwa Arusha ametatua migogoro ya wilaya ya Arumeru na Karatu.


Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (wa nne kulia mbele) akiwasili wilayani Karatu kwa ajili ya kuwapatia hati miliki za Ardhi jamii ya wa Hadzabe.


Wa Hadzabe wakimkaribisha Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kwa kumvusha taji.


Wa Hadzabe wakifurahi na Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi baada ya kuwapa hati miliki za Ardhi.


Wakazi wa kijiji cha Midabini wilayani Karatu Mkoani Arusha wakisimamisha msafara wa Mhe. Lukuvi ili awasikilize kero zao za ardhi, ambapo Waziri Lukuvi alisimama na kuzitatua.


Wakazi wa kijiji cha Mang’ola juu wilayani Karatu Mkoani Arusha waliosimamisha msafara wa Mhe. Lukuvi wakimsikiliza wakati akitatua mgogoro wao wa Ardhi.
Bila elimu, hati miliki ya ardhi kwa jamii zinazoishi primitive life mfano wa Hadzabe haina msaada sana.
 
Bila elimu, hati miliki ya ardhi kwa jamii zinazoishi primitive life mfano wa Hadzabe haina msaada sana.
Lengo kuu ni hiyo jamii isiharibiwe mazingira yake ya kiutamaduni. Eneo likiwa na hati miliki ni rahisi hata kutatua mgogoro pindi unapotokea.
 
Back
Top Bottom