Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, ametaka kunguru weusi au maarufu kama kunguru wa Zenji waangamizwe. Mimi binafsi ninamuunga mkono mkuu wa mkoa kwani kunguru hawa ni kero kweli kweli hasa kwenye ma bar ya chini ya miti. Mimi binafsi wameisha nifanyia vurugu mara nyingi tu, nakumbuka kuna siku niliagiza maziwa fresh, nikanywa mara ya kwanza, kuweka grasi chini nikaona baadhi ya maziwa yameruka kama mtu katumbukiza jiwe vile. Nikaangalia juu nikaona kunguru wawili, machale yakanicheza nikaenda chukua grasi ingine kumimina chini kukawa na settlements za mavi ya kunguru, nikamwaga maziwa yote, ila kama nisingeona ilikuwa nikute settlements kwenye tone la mwisho kuelekea tumboni sijui ingekuwaje. Kuna issue kama kuchangia nao supu ukienda kunawa, au hata kukuchafulia nguo kwa vinyesi.
Ila naona suala la hawa kunguru limekuwa out of control. Kwa mkuu wa mkoa kutangaza watu waanze kuwaua naona kama hayupo practical hivi. Nakumbuka huko nyuma amri ya kuwauwa kunguru ilikuwepo na hata kutangaza dau la shs 50 kwa mzoga wa kunguru. Kwa kumsaidia mkuu wa mkoa zoezi hili haliwezi kufanikiwa kwa agizo alilotoa. Ili afanikiwe kuna njia kuu mbili za kufuatwa ili kuwaangamiza hawa kunguru.
1. Njia ya kwanza ni mkoa kutangaza kununua mzoga wa kunguru kwa shs 200 tu, yaani mtu akiua kunguru mmoja akimpeleka Ilala Boma anapata shs 200. Ninakuhakikishia baada ya mwezi mmoja watabaki kunguru kumi tu Dar nzima, maana dili hili litachamkiwa kweli kweli badala ya watu kupiga debe vituoni. Ila ubaya wa njia hii ni ufisadi wa watendaji wetu,ni dhahiri watakula dili na wawindaji ku-overstate namba ya kunguru waliouwawa ili baadae wagawane malipo na wawindaji, hii sii-recommend kwa mazingira ya Bongo.
2. Njia ya pili ni kutumia SCIENTIFIC METHODS. Hizi zipo nyingi kama mitego, kudiscourage mazalia kwa bongo itakuwa ngumu sana kwani minazi ni mingi. Ila kuna njia moja "OVOCONTROL" hutumia dawa za majira kuwawekea ndege kwenye chakula ili kufanya mayai yao yasianguliwe. Hii imetumika sana katika kudhibiti ongezeko la njiwa na gees kwenye nchi zilizoendelea.
Ila agizo la kutaka watu wawauwe tu ndugu mkuu wa mkoa bado utakuwa hujafanya kitu kwani, mkono mtupu haulambwi. kama serikali imeamua kuwaangamiza kunguru ifanye campaign kama ya Malaria ambayo huhitaji pesa na si maneno matupu
Ila naona suala la hawa kunguru limekuwa out of control. Kwa mkuu wa mkoa kutangaza watu waanze kuwaua naona kama hayupo practical hivi. Nakumbuka huko nyuma amri ya kuwauwa kunguru ilikuwepo na hata kutangaza dau la shs 50 kwa mzoga wa kunguru. Kwa kumsaidia mkuu wa mkoa zoezi hili haliwezi kufanikiwa kwa agizo alilotoa. Ili afanikiwe kuna njia kuu mbili za kufuatwa ili kuwaangamiza hawa kunguru.
1. Njia ya kwanza ni mkoa kutangaza kununua mzoga wa kunguru kwa shs 200 tu, yaani mtu akiua kunguru mmoja akimpeleka Ilala Boma anapata shs 200. Ninakuhakikishia baada ya mwezi mmoja watabaki kunguru kumi tu Dar nzima, maana dili hili litachamkiwa kweli kweli badala ya watu kupiga debe vituoni. Ila ubaya wa njia hii ni ufisadi wa watendaji wetu,ni dhahiri watakula dili na wawindaji ku-overstate namba ya kunguru waliouwawa ili baadae wagawane malipo na wawindaji, hii sii-recommend kwa mazingira ya Bongo.
2. Njia ya pili ni kutumia SCIENTIFIC METHODS. Hizi zipo nyingi kama mitego, kudiscourage mazalia kwa bongo itakuwa ngumu sana kwani minazi ni mingi. Ila kuna njia moja "OVOCONTROL" hutumia dawa za majira kuwawekea ndege kwenye chakula ili kufanya mayai yao yasianguliwe. Hii imetumika sana katika kudhibiti ongezeko la njiwa na gees kwenye nchi zilizoendelea.
Ila agizo la kutaka watu wawauwe tu ndugu mkuu wa mkoa bado utakuwa hujafanya kitu kwani, mkono mtupu haulambwi. kama serikali imeamua kuwaangamiza kunguru ifanye campaign kama ya Malaria ambayo huhitaji pesa na si maneno matupu
Dar es Salaam kuanza kuangamiza kunguru weusi
Na Zaina Malongo
MKUU wa Mkoa Dar es Salaam, William Lukuvi imewataka wananchi kutoa ushirikiano wa serikali katika kuwaangamiza kungururu weusi waliotapakaa jijini na kuhatarisha maisha ya binadamu na wanyama.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana alisema kunguru hao ambao awali waliletwa Zanzibar kwa lengo la kula wadudu waliokuwa wanaharibu zao la karafuu visiwani humo; wanazaliana haraka na sasa wanafanya uharibifu katika maeneo mbalimbali.
Alisema kunguru hao hivi sasa mbali na kusumbua wananchi wanakula ndege wa asili na kuharibu kizazi chao.
Kwa upande wa binadamu, alisema kunguru hao wanavamia vyakula pamoja na kuharibu mazingira.
"Kunguru hawa wameshakuwa hatari kwa maisha ya wanyama na binadamu, kwani wamekuwa wakila ndege wetu wa asili na wanaharibu mazingira na mali mbalimbali kikiwemo chakula na makazi ya watu,"alisema Lukuvi.
Lukuvi alisema lengo la kuwaleta kunguru hao wakati huo lilikuwa zuri kwa ajili ya kudhibiti wadudu waliokuwa wanaharibu zao la karafuu na walisaidia, lakini baada ya kuzaana kwa wingi walianza kuzagaa kila mahali hadi huku bara na kuwa hatari kwa maisha ya ndege na binadamu nchini.
Aliongeza kuwa Mwananchi yeyote aliye na uwezo ajitolee kuwaangamiza kunguru hao hatari kwa kuzingatia sheria za nchi, lakini bila kusababisha madhara yoyote kwa binadamu.
Ombi hilo la mkuu wa mkoa limetolewa kutokana na athari zinazosababishwa na kunguru ikiwemo kudokoa chakula sokoni au mahali popote kinapowekwa hata kama watu wapo,pamoja na kushika vifaranga. Mbali na Dar es Salaam ndege hao wameripotiwa wanaendelea kuenea hadi mikoa mingine kama Tanga, Pwani na Morogoro na inawezekana wakafika mikoa mingine kama hawatadhibitiwa.
source: Mwananchi
Last edited: