Lukuvi ataka wamiliki wa ardhi wenye hati za miaka 33 kuzihuisha Ofisi za Ardhi za Mikoa

mkiluvya

JF-Expert Member
May 23, 2019
802
725
1593962316077.png

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amewataka wamiliki wa ardhi ambao hati zao za ardhi zinaishia miaka 33 kwenda ofisi za ardhi za mikoa zilizoanzishwa hivi karibuni kuzihuisha ili kupatiwa za miaka 99.

Lukuvi ametoa kauli hiyo jana mkoani Mara wakati akizindua ofisi ya ardhi mkoa wa Mara ambayo ni ofisi ya kumi na mbili kuzinduliwa ikiwa ni mfululizo wa kuzindua ofisi za ardhi kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Alisema, kuna baadhi ya wamiliki wa ardhi kwenye mikoa mbalimbali ambao viwanja vyao vimepimwa na michoro kuidhinishwa lakini hati zao ni za miaka 33 na wamiliki hao watakapoenda kuzichukua wanatakiwa kuziangalia ili zibadilishwe na kupatiwa hati za miaka 99.

‘’ Hati nyingi za wale wamiliki ambao hawajazichukua zimekwisha muda wake, muende kwenye ofisi za ardhi za mikoa, huko mtaelekezwa na Wasajili Wasaidzi wa ardhi katika ofisi hizo namna ya kuzibadilisha ili mpatiwe za miaka 99’’ alisema Lukuvi.

Kwa mujibu wa Lukuvi, zaidi ya wamiliki wa ardhi 50,000 kwenye mkoa Mara hawajachukua hati za ardhi wengi muda wa hati zao unaishia miaka 33 na kutaka kufika ofisi za ardhi mkoa wa Mara kurekebishiwa na kupatiwa za miaka 99 ili iwe rahisi kupata mikopo mikubwa . Akizungumzia uzinduzi ofisi ya ardhi mkoa wa Mara, Lukuvi alisema mkoa huo umekuwa na migogoro mingi ya ardhi na kubainisha kuwa uzinduzi wa ofisi hiyo utawawezesha wananchi wa Mara kumaliza migogoro kupitia ofisi hiyo badala ya kuipeleka migogoro kwake.

Waziri Lukuvi aliongeza kuwa, pamoja na Wizara yake hapo awali kushughulikia kero na migogoro ya ardhi lakini tatizo la kimfumo lilikuwa kubwa na kuweka wazi kuwa uzinduzi wa ofisi za mikoa unakomesha kero ambapo sasa hakutakiwa na gharama yoyote kwa mmiliki wa ardhi zaidi ya ile atakayolipia wakati wa kuomba hati.

‘’Mgogoro wa kimfumo ulikuwa mkubwa zaidi na leo hii tumekomesha kero na hakuna gharama yoyote mmiliki wa ardhi ataingia kufuatilia hati zaidi ya ile aliyolipa wakati wa kuomba hati, serikali ya awamu ya tano imeondoa kero zote kwa wananchi kwenye utawala wa ardhi’’ alisema Lukuvi.
 
Huu Ukomo wa Miaka sijui 33,66 na 99 ni Upuuzi......Sasa kama ardhi ni mali ya serikali ila mwananchi amekabidhiwa hayo mambo ya ku expire ya nini? Ni Utopolo na kuweka mianya ya utapeli.
 
Huu Ukomo wa Miaka sijui 33,66 na 99 ni Upuuzi......Sasa kama ardhi ni mali ya serikali ila mwananchi amekabidhiwa hayo mambo ya ku expire ya nini? Ni Utopolo na kuweka mianya ya utapeli.
kwamba miaka 99 ni midogo mkuu !
 
Ikiisha hiyo 99 unaenda ku renew hivyo ni kuwasumbua wajukuu kuanza kufatilia manispaa,shida ya nini wakati babu yao alishalipia miaka 99 iliyopita?
jukumu lao sasa unataka utumie bure ardhi ya Tanzania hapa sio Kenya Mkuu ni Tanzania ndio maana hakuna mwenye kumiliki ardhi tunapangishwa tu na Serikali. Ni mawazo ya Jioni Dukani kwa Mangi na Ka bia baridi - Uchumi wa kati
 
jukumu lao sasa unataka utumie bure ardhi ya Tanzania hapa sio Kenya Mkuu ni Tanzania ndio maana hakuna mwenye kumiliki ardhi tunapangishwa tu na Serikali. Ni mawazo ya Jioni Dukani kwa Mangi na Ka bia baridi - Uchumi wa kati
Ni usumbufu kama ni kupangisha si watupangishe tu maana kila mwaka june tunalipia viwanja.
 
Sawa lakini gharama za kulipia hati ziko juu sana tunaomba zishushwe jamani.

Hata gharama za kulipia Rent ni kubwa sana , tunaomba zipunguzwe ziwe flat rate ya Tsh 10,000 kama kodi za majengo.

Ndiyo maana swala la irasimishaji wengine hawajalipia upimaji wala hati sababu wanajua wakifanya hivyo mtihani utakuwa kwenye kulipa rent kila Mwaka ambapo gharama ni kubwa sana.

Tena kwa mwenye viwanja zaidi viwili vitatu ndiyo mtihani mkubwa zaidi.
 
Hizi ngonjera za kuombea kura zinachosha
Swala la HATI za VIWANJA halipatiwi ufumbuzi
Wizara hii watumishi wake wamejitajirisha kupitia viwanja vya watu kuna dhuluma ya kutisha
Toeni hati punguzeni porojo, ahadi na maagizo hewa kila siku
 
Mm wamenipa hati ya Miaka 66! Waniongezee tu hiyo 33 mengine
 
Back
Top Bottom