sikiolakufa
JF-Expert Member
- Feb 1, 2010
- 411
- 54
Katika hali isiyo ya kawaida waziri wa nchi uratibu na bunge William Lukuvi jana alikwepa kutoa msaada kwa majeruhi wawili waliojeruhiwa vibaya katika ajali ya gari na pikipiki eneo la coco beach. Licha ya waenda kwa miguu kumpungia waziri huyo asimame lakini aligeuza shingo kwa dharau na kuondoka.
Mimi najiuliza hivi viongozi si wanapaswa kuwa mstari wa mbele kusaidia wananchi. Je iwapo ajali hiyo ingekuwa imetokea kwenye jimbo lake la uchaguzi angekacha. Imeniuma sana majeruhi wale walikaa takribani nusu saa bila kupata msaada huku vigogo wa oysterbay wakipita pembeni....
Ni wazungu fulani tu watu wa Mungu waliguswa wakajitolea Land cruiser yao kumpakia dereva wa pikipiki ambaye alikuwa amevunjika vibaya lakini bado alikuwa anahema.
Viongozi kama Lukuvi hawafai ni wanafikir mtu alikuwa mkuu wa mkoa anashindwa kuguswa na watu wa Dar es salaam. Angekuwa waziri mkuu sawa tungesema sababu za usalama lakini nani anamuwinda Lukuvi?
Mimi najiuliza hivi viongozi si wanapaswa kuwa mstari wa mbele kusaidia wananchi. Je iwapo ajali hiyo ingekuwa imetokea kwenye jimbo lake la uchaguzi angekacha. Imeniuma sana majeruhi wale walikaa takribani nusu saa bila kupata msaada huku vigogo wa oysterbay wakipita pembeni....
Ni wazungu fulani tu watu wa Mungu waliguswa wakajitolea Land cruiser yao kumpakia dereva wa pikipiki ambaye alikuwa amevunjika vibaya lakini bado alikuwa anahema.
Viongozi kama Lukuvi hawafai ni wanafikir mtu alikuwa mkuu wa mkoa anashindwa kuguswa na watu wa Dar es salaam. Angekuwa waziri mkuu sawa tungesema sababu za usalama lakini nani anamuwinda Lukuvi?