Luku iNAIBIWA Hivi

BABA JUICE

JF-Expert Member
Sep 5, 2010
426
52
Hapa nipo njia panda,jana nilienda kununua umeme wa elfu ishirini mlimani city,nikapata unity 105.1. VAT 18%, EWURA 1%, REA 3% julma 3,606.56(kodi)...leo nimenunua katika sheli ya BIG BON hapa mwenge umeme wa shilingi elfu ishirini na tano nikapata unity 131.4 VAT 18%, EWURA 1%, REA 3% julma 4,508.20(kodi), wataalamu waliosoma hesabu percentage zipo pale pale lakini kodi inaongezeka naomba ufafanuzi kama ww ni mjuzi wa mambo haya.....huu unaweza ukawa ndio wizi wa kitabu tusipofuatilia.
 
Zote mbili, ya kwanza na ya pili wamekata VAT tu. Inaelekea ulinunua ndani ya mwezi ule ule.
Cha kushangaza sehemu zote mbili wameweka VAT kama 18.0328% badala 18%.
Iliyozidi ni 0.0328%.
Kuna mwenye wazo hiyo ni ya nini? Au ndio faida ya muuzaji?
 
kwani faida ya muzaji unakatwa kwenye unit zako jmani si wanalipwa na tanesko
 
20,0000 / 25,000 the ratio is 4/5

3,606.56 /4,508.20 ratio ni 4/5

They are right on the money, down to the cent. Kodi imebadilika kwa kiwango kile kile cha pesa ulichotumia, maana yake, kiwango cha kodi kwa asilimia kipo pale pale.

Ukitumia hela zaidi, ingawa kiwango cha kodi kwa asilimia kipo pale pale, utachajiwa kodi zaidi kulinganisha na ukitumia pesa kidogo.
 
Hapa nipo njia panda,jana nilienda kununua umeme wa elfu ishirini mlimani city,nikapata unity 105.1. VAT 18%, EWURA 1%, REA 3% julma 3,606.56(kodi)...leo nimenunua katika sheli ya BIG BON hapa mwenge umeme wa shilingi elfu ishirini na tano nikapata unity 131.4 VAT 18%, EWURA 1%, REA 3% julma 4,508.20(kodi), wataalamu waliosoma hesabu percentage zipo pale pale lakini kodi inaongezeka naomba ufafanuzi kama ww ni mjuzi wa mambo haya.....huu unaweza ukawa ndio wizi wa kitabu tusipofuatilia.

Baba Juice nawe mara ya kwanza umetumia 20,000 mara ya pili 25,000 hivyo kodi laziam iongezeke! tena wamekuhurumia EWURA NA REA hawachukua kitu, btw REA ndio watu gani?
 
Hakuna wizi wowote hapo.

20000/1.22 = 16,393 ndio gharama halisi ya umeme ulionunua. Tofauti 20,000-16393 = 3606.56 ni kodi.

25000/1.22 = 20491.80. Tofauti (difference) i.e. 25000 - 20491.80 = 4508.20 ni kodi (VAT 18%, EWURA 1% ,REA 1%)
 
Hakuna wizi wowote hapo.

20000/1.22 = 16,393 ndio gharama halisi ya umeme ulionunua. Tofauti 20,000-16393 = 3606.56 ni kodi.

25000/1.22 = 20491.80. Tofauti (difference) i.e. 25000 - 20491.80 = 4508.20 ni kodi (VAT 18%, EWURA 1% ,REA 1%)
Mkuu hii EWURA na REA ndio kitu gani?
 
Hapa nipo njia panda,jana nilienda kununua umeme wa elfu ishirini mlimani city,nikapata unity 105.1. VAT 18%, EWURA 1%, REA 3% julma 3,606.56(kodi)...leo nimenunua katika sheli ya BIG BON hapa mwenge umeme wa shilingi elfu ishirini na tano nikapata unity 131.4 VAT 18%, EWURA 1%, REA 3% julma 4,508.20(kodi), wataalamu waliosoma hesabu percentage zipo pale pale lakini kodi inaongezeka naomba ufafanuzi kama ww ni mjuzi wa mambo haya.....huu unaweza ukawa ndio wizi wa kitabu tusipofuatilia.

Ebu ziweke izo karatasi zote mbili ulizonunulia huo umeme wa LUKU hapa jf tuweze kuona mtiririko wake la cvyo tutashindwa kuchangia thread yako.
 
Ebu ziweke izo karatasi zote mbili ulizonunulia huo umeme wa LUKU hapa jf tuweze kuona mtiririko wake la cvyo tutashindwa kuchangia thread yako.

mtiririko gani tena wakati ameshatoa kila kitu, hakuna wizi hapo kodi imeongezeka kutokana kuongezeka kwa fedha aliyotoa. 25000 itakatwa kodi kubbwa kuliko 20000.
 
Mkuu hii EWURA na REA ndio kitu gani?

EWURA ni mamlaka iliyowekwa kisheria kushughulikia mambo yote ya nishati na maji kama ilivyo TCRA ambayo inasimamia mawasiliano au SUMATRA inayosimamia shughuli zote za usafiri.

Sasa, according to Ministry of Energy & Natural Resources, REA is

" The Rural Energy Agency (REA) was established by the Act of Parliament No.8 of 2005 as an
autonomous institution to administer the Rural Energy Fund (REF). REA is governed by the Rural
Energy Board (REB). The main function of REA is to promote investment in modern energy services by
working with key partners and collaborators from the private sector, NGOs, CBOs, and Government
agencies to mobilize resources in order to achieve its objectives.".

http://www.rea.go.tz/LinkClick.aspx?fileticket=fvs3xjo68ts=&tabid=144&mid=554

Katika maisha ya kila siku sijasikia hawa REA wanafanya nini. Hivyo hiyo 3% ya mauzo yote ya LUKU/nishati, ambazo ni hela nyingi sana, hatusikii miradi yoyote ambayo REA imefanya au inataka kufanya. Tofauti na VETA ambayo kwa miaka mingi ilikuwa inapata fedha kutokana na makato kwa waajiri.

Hawa REA need to come out and explain where they take our money into....
 
Back
Top Bottom