EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Ilikuwa kama vile Morata asajiliwe na Man Utd na Lakaku asajiliwe na Chelsea. Lakini imekuwa kinyume chake. Man Utd wamemsajili Lakaku na Chelsea wanamsajili Morata.
Wapo wanaodai kuwa Lakaku ni striker mzuri zaidi kuliko Morata. Pia wapo wanaodai Morata ni mkali zaidi kuliko Lakaku.
Arsenal nao wamevunja rekodi yao kwa kumsajili Lacazette. Wako wanaodai kuwa Lacazette ni mkali zaidi ya Lakaku, au zaidi ya Morata au zaidi ya wote wawili.
Lakini nani alifunga magoli mengi zaidi msimu uliopita? Nani alifanya kazi kubwa kwa ajili ya timu yake. Nani atafanikiwa zaidi kwenye timu zao mpya? Kwa kifupi klabu ipi imepata dili nzuri?
Bado ni mapema sana kujua nani mkali zaidi, lakini siyo vibaya kutoa maoni yako juu ya nani aliye mkali zaidi japokuwa muundo wa timu nzima nao unachangia kwa striker kucheza vizuri zaidi na kufunga magoli ya kutosha.