Luhanjo atoa ripoti, Jairo arudishwa kazini

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo,ametoa ripoti na kusema Jairo anarudishwa kazini kuanzia kesho.
===========
UPDATES:

Luhanjo anasema tuhuma zilikuwa za uwongo
Anasema taasisi za Wizara hazizidi 7 na si zaidi ya 20 kama ilivyodaiwa
Taasisi nne tu ndizo zilizochangia na zilichanga karibu TZS 500mil na si zaidi ya 1bil kama ilivyodaiwa
Pesa zilichangwa ili kuwawezesha watendaji watakaoenda kwenye bunge la bajeti
REA walichangia 50mil
TANESCO walichangia 40mil
EWURA waliombwa 40mil lkn hawakutoa, walichangia gharama za chakula na malazi kwa watendaji wa Wizara

Idara ya Uhasibu ya Wizara ilitoa 150mil
Idara ya mipango ya Wizara ilitoa 278mil

More updates to follow...
 
Sasa source wako nani??? Na kwanini unaongea issue sensitive namna hiyo kwa ufupi kiasi hicho bila details? Yaani umeniharibia siku yangu leo mara mbili, kwanza kwa kuandika jambo zito kwa ufupi sana, pili kama ni ukweli basi siku yangu leo ndo imekuwa mbaya zaidi!
 
Tanzania ni zaidi ya uijuavyo tukazeni buti tu tutafika but not with these bunch of leaders.
 
Hii serikali inatupeleka wapi sasa. Mtu ambaye ametuhumiwa kwa uwazi kabisa anarudishwaje tena kazini. It beats me!

jamani kwani kutuhumiwa ni kukutwa na hatia? si alituhumiwa, akawekwa kando kupisha uchunguzi huru na umekamilika na kuonekana hana hatia (kama ndivyo alivyoonekana)

mi nafikiri kwa mchakato wa utawala bora wako sawa, ila wasiwasi wangu ni sawa na wa wengine, kama suala la jairo halikuwa la rushwa/ufisadi, sasa suala la rushwa/ufisadi ni la aina gani? kama hata jairo kapenya, atakayenaswa ni nani tena?

kwa kweli mi naona kama serikali inaji-disqualify yenyewe katika ku-lead hii vita ya rushwa/ufisadi

bado nasubiri kupata taarifa kamili kabla siaongeza maoni yangu mengine

mbarikiwe sana
 
Preta ndo maana sijagi huku maana unaweza haribu keyboard kwa hasira ukijua unapigana na Luhamjo

bora niende zangu kwenye thread yangu ya Ileje kule......khaaa.......kweli nahitaji fresh air......
 
Sasa source wako nani??? Na kwanini unaongea issue sensitive namna hiyo kwa ufupi kiasi hicho bila details? Yaani umeniharibia siku yangu leo mara mbili, kwanza kwa kuandika jambo zito kwa ufupi sana, pili kama ni ukweli basi siku yangu leo ndo imekuwa mbaya zaidi!

Mkuu hii issue ina u-senstive gani? what more details do you want to hear. Habari hii ni pande mbili tu, moja ameadhibiwa kutokana na makosa, na ya pili hajachukuliwa hatua zozote. Tuombe Mungu tu kuwa hii si kweli..
 
Na bado....

Inabidi madudu yaendelee hivi hivi mpaka ifike 2015 ndo watanzania wataamka kuona kuwa kweli CCM imeoza na haifai!!!!
 
Back
Top Bottom