Luhaga Mpina amlipua Waziri Makamba, amtuhumu kwa Uhujumu Uchumi. Atoa wito kwa TAKUKURU kumchukulia hatua

Luhaga Mpina Mbunge wa Kisesa amesema Rais Samia alitaka mawaziri wamsaidie katika kujibu hoja za wananchi, hata hivyo jambo hilo halionekani sana kwa sasa, ambapo amesema mawaziri wapo kimya katika kujibu hoja za wananchi.

Mpina amesema wapo mawaziri hawajibu hoja za wananchi au huwa wanajibu kwa hoja nyepesi malalamiko ya raia, hali ambayo ameitaja kuwa sio kumsaidia Rais kama inavyotarajiwa.

Ametoa mfano wa waziri wa Nishati alivyojibu kuhusu ucheleweshwaji wa mradi wa bwawa la Mwl Nyerere ambapo Waziri wa Nishati alianza kulaumu kuwa Wabunge hawakutaka yeye awe waziri badala ya kujibu hoja iliyokuwa mezani.

Waziri ametolea mfano suala la kufuta tozo ya Tsh. 100 katika mafuta bila kufuata utaratibu. Ambapo amesema maamuzi ya waziri kufuta tozo hiyo amekutaja ni sawa na uhujumu wa mapato ya Serikali kwa kuwa fedha ya tozo hiyo ilikuwa katika bajeti ya Serikali ya mwaka 2021/22.

Kwa kushindwa kufuata taratibu za kuondoa tozo, Luhaga Mpina amesema Waziri wa Nishati amekuwa amefanya kosa la Uhujumu Uchumi. Na ameshindwa kutafuta kukielewa chanzo cha upandaji wa bei za mafuta nchini.

Kufuta tozo ya Tsh. 100 bila kufanya tathmini kumeipotezea Serikali Tsh. Bilioni 30. Hivyo, hakuwa na nia njema, achukuliwe hatua, atoa wito kwa TAKUKURU kumchukulia hatua. Amesema suala la kumchukulia hatua sio jambo la hiari, ni kwa mujibu wa sheria.

Mambo mengine aliyoyataja katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari ametaja kuwa Waziri Makamba ameshindwa kujibu kuhusu bei za mafuta na mfumuko wa bei.
Huu mjadala ulipamba moto
 
Amejaa chuki tu dhidi ya Makamba!

Saivi Hakuna mgao na hali ya umeme umerudi kuwa kawaida! Kama kukatika umeme umeme haijaanza kukatika Leo wala jana!

Kuhusu bei ya Mafuta inabidi atuambie ni wapi duniani Mafuta hayajapanda bei!

Amejawa na chuki tu Huyu mpuuzi na mkabila! Wana hasira na Makamba wa watu Kwa kuendekeza upuuzi wao wa roho mbaya
uko tanzania kweli
 
Luhaga Mpina Mbunge wa Kisesa amesema Rais Samia alitaka mawaziri wamsaidie katika kujibu hoja za wananchi, hata hivyo jambo hilo halionekani sana kwa sasa, ambapo amesema mawaziri wapo kimya katika kujibu hoja za wananchi.

Mpina amesema wapo mawaziri hawajibu hoja za wananchi au huwa wanajibu kwa hoja nyepesi malalamiko ya raia, hali ambayo ameitaja kuwa sio kumsaidia Rais kama inavyotarajiwa.

Ametoa mfano wa waziri wa Nishati alivyojibu kuhusu ucheleweshwaji wa mradi wa bwawa la Mwl Nyerere ambapo Waziri wa Nishati alianza kulaumu kuwa Wabunge hawakutaka yeye awe waziri badala ya kujibu hoja iliyokuwa mezani.

Waziri ametolea mfano suala la kufuta tozo ya Tsh. 100 katika mafuta bila kufuata utaratibu. Ambapo amesema maamuzi ya waziri kufuta tozo hiyo amekutaja ni sawa na uhujumu wa mapato ya Serikali kwa kuwa fedha ya tozo hiyo ilikuwa katika bajeti ya Serikali ya mwaka 2021/22.

Kwa kushindwa kufuata taratibu za kuondoa tozo, Luhaga Mpina amesema Waziri wa Nishati amekuwa amefanya kosa la Uhujumu Uchumi. Na ameshindwa kutafuta kukielewa chanzo cha upandaji wa bei za mafuta nchini.

Kufuta tozo ya Tsh. 100 bila kufanya tathmini kumeipotezea Serikali Tsh. Bilioni 30. Hivyo, hakuwa na nia njema, achukuliwe hatua, atoa wito kwa TAKUKURU kumchukulia hatua. Amesema suala la kumchukulia hatua sio jambo la hiari, ni kwa mujibu wa sheria.

Mambo mengine aliyoyataja katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari ametaja kuwa Waziri Makamba ameshindwa kujibu kuhusu bei za mafuta na mfumuko wa bei.
Mimi ni CCM lakini naona kabisaa Mpina anataka kujenga hoja bila contents zenye mashiko.

Hizi za kuondoa tozo na kadhalika zipo kwenye uwezo wa yeye Mbunge kupeleka hoja binafsi bungeni....

Mengine aje na evidences
 
Back
Top Bottom