Luhaga Mpina aenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC)

SULEIMAN ABEID

JF-Expert Member
Feb 26, 2013
390
385
PANGA LA NEC LAMFYEKA LUHAGA MPINA- JINA LAKE LAENGULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA NEC.

* Mambo 11 yaliyomponza yatajwa

HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imeliengua jina la Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu, Luhaga Mpina kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Chama hicho mara baada ya vikao vya Taifa vya uteuzi na kuthibitishwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mohamed Ali Khalfan alisema jina la Mpina halimo kwenye orodha ya majina ya wagombea wa nafasi ya NEC Mkoa wa Simiyu yaliyopitishwa na vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Mpina alikuwa ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua na kurejesha fomu kuomba nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na NEC Viti 15 Tanzania Bara.

Hata hivyo katibu huyo wa CCM mkoani Simiyu hakuweza kuyataja majina ya walioteuliwa kwa kuahidi kuyataja baadae kwani wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi alisema yuko kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Mkoa.

Baadhi ya makada wa CCM wamesikika wakidai huenda ikawa jina la Mpina limeenguliwa kutokana na misimamo yake anayoionyesha bungeni katika kuhoji mambo mbalimbali ya wananchi.

Makada hao wamedai miongoni mwa mambo yanayoweza kuwa yamemponza Mpina ni kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRAT.

Lingine ni kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.

Mpina pia kupitia Bunge alihoji kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.

Mbali na hilo Mpina pia alihoji bungeni kitendo cha TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.

“Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo” alisema Jumanne Mashauri

Jambo lingine ni linalodaiwa kumponza ni kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo.

Suala lingine linalodaiwa kumponza Mpina ni kitendo chake cha kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.

Jambo lingine ni kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.

Hata hivyo makada hao walisema huenda pia msimamo wake wa kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme huenda pia likawa limemgharimu kuenguliwa.

Maeneo mengine ambayo Mpina amekuwa akihoji bungeni ni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini

Pia amekuwa akihoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.

Mpina alipoulizwa kuhusiana na madai ya kuengeliwa kwenye kinyang’anyiro cha NEC Mkoa wa Simiyu simu yake iliita bila kupokelewa na baadaye alituma ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yuko kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Uongozi cha Halmashauri ya Meatu.`
Luhaga_Mpina.jpg
 
PANGA LA NEC LAMFYEKA LUHAGA MPINA- JINA LAKE LAENGULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA NEC.

* Mambo 11 yaliyomponza yatajwa

HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imeliengua jina la Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu, Luhaga Mpina kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Chama hicho mara baada ya vikao vya Taifa vya uteuzi na kuthibitishwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mohamed Ali Khalfan alisema jina la Mpina halimo kwenye orodha ya majina ya wagombea wa nafasi ya NEC Mkoa wa Simiyu yaliyopitishwa na vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Mpina alikuwa ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua na kurejesha fomu kuomba nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na NEC Viti 15 Tanzania Bara.

Hata hivyo katibu huyo wa CCM mkoani Simiyu hakuweza kuyataja majina ya walioteuliwa kwa kuahidi kuyataja baadae kwani wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi alisema yuko kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Mkoa.

Baadhi ya makada wa CCM wamesikika wakidai huenda ikawa jina la Mpina limeenguliwa kutokana na misimamo yake anayoionyesha bungeni katika kuhoji mambo mbalimbali ya wananchi.

Makada hao wamedai miongoni mwa mambo yanayoweza kuwa yamemponza Mpina ni kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRA.

Lingine ni kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.

Mpina pia kupitia Bunge alihoji kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.

Mbali na hilo Mpina pia alihoji bungeni kitendo cha TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.

“Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo” alisema Jumanne Mashauri

Jambo lingine ni linalodaiwa kumponza ni kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo.

Suala lingine linalodaiwa kumponza Mpina ni kitendo chake cha kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.

Jambo lingine ni kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.

Hata hivyo makada hao walisema huenda pia msimamo wake wa kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme huenda pia likawa limemgharimu kuenguliwa.

Maeneo mengine ambayo Mpina amekuwa akihoji bungeni ni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini

Pia amekuwa akihoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.

Mpina alipoulizwa kuhusiana na madai ya kuungeliwa kwenye kinyang’anyiro cha NEC Mkoa wa Simiyu simu yake iliita bila kupokelewa na baadaye alituma ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yuko kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Uongozi cha Halmashauri ya Meatu.`
Kipindi Cha mwendazake,huyu ni mmoja wa waliokuwa wakitamba sana,hata hayo anayoyapigia kelele yalikuwepo kipindi Cha mwendazake,lakini hakuyazaungumzia,maana alikuwa upande wa wenye asali na Ikulu,sasa baada ya kutupwa nje ya ulaji,imekuwa makasiriko!!!wacha ashikishwe adabu!!
 
PANGA LA NEC LAMFYEKA LUHAGA MPINA- JINA LAKE LAENGULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA NEC.

* Mambo 11 yaliyomponza yatajwa

HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imeliengua jina la Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu, Luhaga Mpina kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Chama hicho mara baada ya vikao vya Taifa vya uteuzi na kuthibitishwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mohamed Ali Khalfan alisema jina la Mpina halimo kwenye orodha ya majina ya wagombea wa nafasi ya NEC Mkoa wa Simiyu yaliyopitishwa na vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Mpina alikuwa ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua na kurejesha fomu kuomba nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na NEC Viti 15 Tanzania Bara.

Hata hivyo katibu huyo wa CCM mkoani Simiyu hakuweza kuyataja majina ya walioteuliwa kwa kuahidi kuyataja baadae kwani wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi alisema yuko kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Mkoa.

Baadhi ya makada wa CCM wamesikika wakidai huenda ikawa jina la Mpina limeenguliwa kutokana na misimamo yake anayoionyesha bungeni katika kuhoji mambo mbalimbali ya wananchi.

Makada hao wamedai miongoni mwa mambo yanayoweza kuwa yamemponza Mpina ni kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRA.

Lingine ni kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.

Mpina pia kupitia Bunge alihoji kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.

Mbali na hilo Mpina pia alihoji bungeni kitendo cha TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.

“Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo” alisema Jumanne Mashauri

Jambo lingine ni linalodaiwa kumponza ni kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo.

Suala lingine linalodaiwa kumponza Mpina ni kitendo chake cha kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.

Jambo lingine ni kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.

Hata hivyo makada hao walisema huenda pia msimamo wake wa kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme huenda pia likawa limemgharimu kuenguliwa.

Maeneo mengine ambayo Mpina amekuwa akihoji bungeni ni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini

Pia amekuwa akihoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.

Mpina alipoulizwa kuhusiana na madai ya kuungeliwa kwenye kinyang’anyiro cha NEC Mkoa wa Simiyu simu yake iliita bila kupokelewa na baadaye alituma ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yuko kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Uongozi cha Halmashauri ya Meatu.`
Apunguze usukuma gang na kuimba taarabu bungeni.....asipoangalia vizuri kwenye kura za maoni za kugombea nafasi ya ubunge hapiti😃
 
Kipindi Cha mwendazake,huyu ni mmoja wa waliokuwa wakitamba sana,hata hayo anayoyapigia kelele yalikuwepo kipindi Cha mwendazake,lakini hakuyazaungumzia,maana alikuwa upande wa wenye asali na Ikulu,sasa baada ya kutupwa nje ya ulaji,imekuwa makasiriko!!!wacha ashikishwe adabu!!
Huyu jamaa ni mnafiki sana Wacha wamnyooshe. Wakiwa serikalini walikopa eeh kujenga miradi sikusikia kelele eti katoka ndio anagundua mikopo ni mibaya. JPM malipo kibao alifanya nje ya bajeti iliyopangwa mfano manunuzi ya ndege ila ilionekana sio shida but ujinga ule ule ukiendelezwa na awamu hii eti ndio anapinga!!!

Nasema hivi anyooshwe na 2025 afyekwe kabisa kura za maoni. Hawa wanafiki tumewachoka, kesho akipewa uwaziri utashangaa anaanza kumpamba Tena Mama.
 
Siku tutakapoacha kujadili watu na kujadili issues hii inchi itapiga hatua sana...Until then wacha tuendelee kua kichwa cha wendawazimu kila kinyozi anajifunzia kushona...
Issues zinatoka kwa watu sio miti!!! Hivi shetani akikwambia kitu utamuamini kisa tu ni "issues"?

Credibility Ina matter kwenye siasa haiwezekani mtu yule yule aliyesupport JPM kukopa Ili tujenge miradi eti ndio huyo huyo anatoa povu Samia akikopa!!

Mnafiki tu huyu hana credibility yoyote tena
 
PANGA LA NEC LAMFYEKA LUHAGA MPINA- JINA LAKE LAENGULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA NEC.

* Mambo 11 yaliyomponza yatajwa

HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imeliengua jina la Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu, Luhaga Mpina kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Chama hicho mara baada ya vikao vya Taifa vya uteuzi na kuthibitishwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mohamed Ali Khalfan alisema jina la Mpina halimo kwenye orodha ya majina ya wagombea wa nafasi ya NEC Mkoa wa Simiyu yaliyopitishwa na vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Mpina alikuwa ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua na kurejesha fomu kuomba nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na NEC Viti 15 Tanzania Bara.

Hata hivyo katibu huyo wa CCM mkoani Simiyu hakuweza kuyataja majina ya walioteuliwa kwa kuahidi kuyataja baadae kwani wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi alisema yuko kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Mkoa.

Baadhi ya makada wa CCM wamesikika wakidai huenda ikawa jina la Mpina limeenguliwa kutokana na misimamo yake anayoionyesha bungeni katika kuhoji mambo mbalimbali ya wananchi.

Makada hao wamedai miongoni mwa mambo yanayoweza kuwa yamemponza Mpina ni kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRA.

Lingine ni kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.

Mpina pia kupitia Bunge alihoji kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.

Mbali na hilo Mpina pia alihoji bungeni kitendo cha TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.

“Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo” alisema Jumanne Mashauri

Jambo lingine ni linalodaiwa kumponza ni kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo.

Suala lingine linalodaiwa kumponza Mpina ni kitendo chake cha kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.

Jambo lingine ni kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.

Hata hivyo makada hao walisema huenda pia msimamo wake wa kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme huenda pia likawa limemgharimu kuenguliwa.

Maeneo mengine ambayo Mpina amekuwa akihoji bungeni ni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini

Pia amekuwa akihoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.

Mpina alipoulizwa kuhusiana na madai ya kuungeliwa kwenye kinyang’anyiro cha NEC Mkoa wa Simiyu simu yake iliita bila kupokelewa na baadaye alituma ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yuko kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Uongozi cha Halmashauri ya Meatu.`
Wakati wa ujanani tulikuwa tunacheza karata mtindo wa arubastini. Unagawa karata 6 kila mtu, mnaotea, moja ikilala ndiyo mchezo wa Raunds hiyo, BWANA ni A na BIBI ni 7. Then kuna K na Q na J zingine zote ng'anda ingawa ng'anda za aliyelala ni mali kuliko K au hata A isiyolala. Kulikuwa na shupaza (jembe); kisu (diamonds), karanga (clubs) na moyo (hearts). Tulikuwa tunakaa wawili wawili au watatu watatu kutegemea idadi. Katika nyie inabidi muelewane sana, lenu liwe moja. Luhaga Mpina nadhani hakucheza karata ila atakuwa amekulia wapi hapa TZ? In my view, tabia yake yanishangaza sana kwa vile anachofanya sasa ni sawa na kumsaliti mkeo. It cannot get worse than that, can it? Yaani mkiwa msitari wa mbele, na kundini kwetu kuna watu kama hawa, they don't deserve to survive.
 
PANGA LA NEC LAMFYEKA LUHAGA MPINA- JINA LAKE LAENGULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA NEC.

* Mambo 11 yaliyomponza yatajwa

HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imeliengua jina la Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu, Luhaga Mpina kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Chama hicho mara baada ya vikao vya Taifa vya uteuzi na kuthibitishwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mohamed Ali Khalfan alisema jina la Mpina halimo kwenye orodha ya majina ya wagombea wa nafasi ya NEC Mkoa wa Simiyu yaliyopitishwa na vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Mpina alikuwa ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua na kurejesha fomu kuomba nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na NEC Viti 15 Tanzania Bara.

Hata hivyo katibu huyo wa CCM mkoani Simiyu hakuweza kuyataja majina ya walioteuliwa kwa kuahidi kuyataja baadae kwani wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi alisema yuko kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Mkoa.

Baadhi ya makada wa CCM wamesikika wakidai huenda ikawa jina la Mpina limeenguliwa kutokana na misimamo yake anayoionyesha bungeni katika kuhoji mambo mbalimbali ya wananchi.

Makada hao wamedai miongoni mwa mambo yanayoweza kuwa yamemponza Mpina ni kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRA.

Lingine ni kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.

Mpina pia kupitia Bunge alihoji kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.

Mbali na hilo Mpina pia alihoji bungeni kitendo cha TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.

“Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo” alisema Jumanne Mashauri

Jambo lingine ni linalodaiwa kumponza ni kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo.

Suala lingine linalodaiwa kumponza Mpina ni kitendo chake cha kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.

Jambo lingine ni kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.

Hata hivyo makada hao walisema huenda pia msimamo wake wa kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme huenda pia likawa limemgharimu kuenguliwa.

Maeneo mengine ambayo Mpina amekuwa akihoji bungeni ni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini

Pia amekuwa akihoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.

Mpina alipoulizwa kuhusiana na madai ya kuengeliwa kwenye kinyang’anyiro cha NEC Mkoa wa Simiyu simu yake iliita bila kupokelewa na baadaye alituma ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yuko kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Uongozi cha Halmashauri ya Meatu.`
Kuna watu watasikitika...

Kataa CCM uliokoe Taifa
 
PANGA LA NEC LAMFYEKA LUHAGA MPINA- JINA LAKE LAENGULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA NEC.

* Mambo 11 yaliyomponza yatajwa

HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imeliengua jina la Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu, Luhaga Mpina kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Chama hicho mara baada ya vikao vya Taifa vya uteuzi na kuthibitishwa pia na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mohamed Ali Khalfan alisema jina la Mpina halimo kwenye orodha ya majina ya wagombea wa nafasi ya NEC Mkoa wa Simiyu yaliyopitishwa na vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Mpina alikuwa ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua na kurejesha fomu kuomba nafasi ya MNEC Mkoa wa Simiyu na NEC Viti 15 Tanzania Bara.

Hata hivyo katibu huyo wa CCM mkoani Simiyu hakuweza kuyataja majina ya walioteuliwa kwa kuahidi kuyataja baadae kwani wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi alisema yuko kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa UWT Mkoa.

Baadhi ya makada wa CCM wamesikika wakidai huenda ikawa jina la Mpina limeenguliwa kutokana na misimamo yake anayoionyesha bungeni katika kuhoji mambo mbalimbali ya wananchi.

Makada hao wamedai miongoni mwa mambo yanayoweza kuwa yamemponza Mpina ni kuhoji bungeni kuhusu madai ya fedha za makinikia Trilioni 360 akitaka kujua nani alisamehe na kama ana mamlaka kisheria kusamehe madai halali ya watanzania ya kiasi cha shilingi Trilioni 5.5 kama ilivyoamuliwa na Mahakama za rufani za Kodi za TRAB na TRA.

Lingine ni kuhoji bungeni juu ya Serikali kushindwa kudai madai halali ya Shilingi Trilioni 1.5 kwa ucheleweshaji wa mradi na CSR kutoka kwa Kampuni ya Arab Contractors ya Misri inayojenga mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere. Lakini pia Serikali kuendelea kutoa taarifa zinazokinzana juu ya ukamilishaji wa mradi huo.

Mpina pia kupitia Bunge alihoji kuhusu kupaa kwa Deni la Taifa kutoka wastani wa kukua kwa asilimia 4 hadi asilimia 13 na kutojulikana zilipo shilingi Trilioni 5 zilizokopwa nje ya bajeti kwa mwaka 2022.

Mbali na hilo Mpina pia alihoji bungeni kitendo cha TRA kushindwa kukusanya malimbikizo ya kodi yasiyo na kesi mahakamani kiasi cha shilingi Trilioni 7.5 na ucheleweshaji wa maamuzi ya mapingamizi ya kodi katika mahakama za rufani za kodi kiasi cha shilingi Trilioni 5 bila kuwepo sababu za msingi.

“Kuhoji bungeni uhalali wa malipo yaliyofanywa na Serikali kwa Kampuni ya Symbion LLC ya shilingi Bilioni 350 nje ya bajeti na bila kuzingatia madai halali ya Serikali ikiwemo kodi na gharama nyinginezo” alisema Jumanne Mashauri

Jambo lingine ni linalodaiwa kumponza ni kukataa bungeni juu ya uamuzi wa Serikali kujenga Bandari ya Bagamoyo bila kuwepo tathmini ya kina juu ya uwezo wa kiuchumi kugharamia mradi huo.

Suala lingine linalodaiwa kumponza Mpina ni kitendo chake cha kuhoji bungeni kuhusu Serikali kuingia mikataba mibovu, kushindwa kurejesha ngombe 6,000 za wafugaji walioshinda kesi mahakamani, kushindwa kudhibiti tembo wanaovamia mashamba na makazi ya wananchi na kusababisha vifo na majeruhi.

Jambo lingine ni kuhoji bungeni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta kwa kisingizio cha vita ya Urusi na Ukraine hali iliyoilazimu Serikali kuweka ruzuku ya shilingi bilioni 100 kila mwezi bila kuwepo unafuu wowote kwa wananchi.

Hata hivyo makada hao walisema huenda pia msimamo wake wa kuhoji bungeni suala la katakata ya umeme na migao ya umeme isiyoisha nchini iliyopelekea kuathiri uchumi na utoaji wa huduma zinazotegemea nishati ya umeme huenda pia likawa limemgharimu kuenguliwa.

Maeneo mengine ambayo Mpina amekuwa akihoji bungeni ni kuhusu suala la usimamizi mbovu na kupanda kiholela kwa bei ya mbolea na namna ilivyowaathiri uzalishaji na upatikanaji wa chakula nchini

Pia amekuwa akihoji bungeni juu ya kupanda kiholela kwa bei za bidhaa na gharama za maisha hali iliyopelekea mfumko mkubwa wa bei nchini huku Serikali ikishindwa kudhibiti hali hiyo.

Mpina alipoulizwa kuhusiana na madai ya kuengeliwa kwenye kinyang’anyiro cha NEC Mkoa wa Simiyu simu yake iliita bila kupokelewa na baadaye alituma ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yuko kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Uongozi cha Halmashauri ya Meatu.`
Kama haya ndio yalimponza na kufutwa kugombea Nafasi ya NEC chombo cha juu cha kuisimamia Serikali nafikirisha sana. Kwani msingi wa CCM ni kutetea nini? Mbona ni mambo ya kawaida kwa CCM kuwa na mawazo kinzani katika kuimarisha Chama nakumbuka zama za kina
Tuntemeke Nnun'gwa SANGA akina Dkt. Chrissant Majiyatanga Mzindaya Mzee wa Mabomu walivyokuwa wanaikosoa Serikali bungeni.
 
Back
Top Bottom