Lugola : Tangu nimeteuliwa sijawahi kupokea malalamiko ya vyama vya siasa kuzuiwa kufanya mikutano

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
W aziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Kangi Lugola amesema hajawahi kupokea barua yoyote kutoka chama cha siasa kulalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara au maandamano.


Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Septemba 26, 2019 baada ya kuzindua ofisi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) mjini Dodoma.


Amesema sheria inawataka watu wanaotaka kukusanyika kulipa taarifa Jeshi la Polisi, wakiona kimya wanaendelea ila wakipewa barua ya zuio wanatakiwa kusitisha shughuli hizo na kukata rufaa kwa waziri mwenye dhamana ya wizara hiyo.


"Tangu nimeteuliwa sijawahi kupokea hata rufaa kulalamika kuwa wamenyimwa haki badala yake wanakurupuka na kulalamika sasa mimi nifanyeje," amesema Lugola.
Amesema wanaolalamika na kuanza kufanya wanachokitaka wao lazima wakutane na mkono wa sheria kwani polisi iko imara na hawawezi kuachwa.



"Tunao polisi imara, hakuna polisi anayeweza kuwakimbia watu hata kidogo lazima wasonge mbele, sasa hapo ndio mtasikia huyu kaumia au kaumizwa yote ni kwa sababu hawafuati sheria," amesema Lugola.


Amesema sheria zikifuatwa hakuna shida itakayotokea lakini kinyume na hapo mambo yanakuwa tofauti.
lugola1%2Bpic.jpeg
 
Amenikumbusha yule Jaji wa kesi ya Tundu Lissu, ambae Mawakili wa Lissu walimuomba atoe amri ya kusimamisha kuapishwa kwa yule "mbunge" kutoka jimbo la Lissu.. Jaji akasema mwache aapishwe, maana haitakuwa na impact kwenye maamuzi yake atakayoyatoa.. Ajabu baadae kaja kutoa maamuzi hawezi kuingilia maamuzi ya muhimili mwingine..

Kama wasingetoa ombi mapema, katika hukumu Jaji angesema wangeomba atoe amri ya kusimamisha kuapishwa kwa asieshtahili kuwa mbunge..
 
Hawa viongozi wanatafutia watu sababu ya kwashughulikia kwa kauli zao za dhihaka
 
W aziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Kangi Lugola amesema hajawahi kupokea barua yoyote kutoka chama cha siasa kulalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara au maandamano.


Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Septemba 26, 2019 baada ya kuzindua ofisi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) mjini Dodoma.


Amesema sheria inawataka watu wanaotaka kukusanyika kulipa taarifa Jeshi la Polisi, wakiona kimya wanaendelea ila wakipewa barua ya zuio wanatakiwa kusitisha shughuli hizo na kukata rufaa kwa waziri mwenye dhamana ya wizara hiyo.


"Tangu nimeteuliwa sijawahi kupokea hata rufaa kulalamika kuwa wamenyimwa haki badala yake wanakurupuka na kulalamika sasa mimi nifanyeje," amesema Lugola.
Amesema wanaolalamika na kuanza kufanya wanachokitaka wao lazima wakutane na mkono wa sheria kwani polisi iko imara na hawawezi kuachwa.



"Tunao polisi imara, hakuna polisi anayeweza kuwakimbia watu hata kidogo lazima wasonge mbele, sasa hapo ndio mtasikia huyu kaumia au kaumizwa yote ni kwa sababu hawafuati sheria," amesema Lugola.


Amesema sheria zikifuatwa hakuna shida itakayotokea lakini kinyume na hapo mambo yanakuwa tofauti.
View attachment 1216445

Je alisha wahi sikia kuwa kuna watu wasijulikana wanafanya kazi zakuwateka watu, kwatesa na pia kuwapoteza, na wakibanwa wanasema ni askari polisi?
 
W aziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Kangi Lugola amesema hajawahi kupokea barua yoyote kutoka chama cha siasa kulalamika kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara au maandamano.


Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Septemba 26, 2019 baada ya kuzindua ofisi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) mjini Dodoma.


Amesema sheria inawataka watu wanaotaka kukusanyika kulipa taarifa Jeshi la Polisi, wakiona kimya wanaendelea ila wakipewa barua ya zuio wanatakiwa kusitisha shughuli hizo na kukata rufaa kwa waziri mwenye dhamana ya wizara hiyo.


"Tangu nimeteuliwa sijawahi kupokea hata rufaa kulalamika kuwa wamenyimwa haki badala yake wanakurupuka na kulalamika sasa mimi nifanyeje," amesema Lugola.
Amesema wanaolalamika na kuanza kufanya wanachokitaka wao lazima wakutane na mkono wa sheria kwani polisi iko imara na hawawezi kuachwa.



"Tunao polisi imara, hakuna polisi anayeweza kuwakimbia watu hata kidogo lazima wasonge mbele, sasa hapo ndio mtasikia huyu kaumia au kaumizwa yote ni kwa sababu hawafuati sheria," amesema Lugola.


Amesema sheria zikifuatwa hakuna shida itakayotokea lakini kinyume na hapo mambo yanakuwa tofauti.
View attachment 1216445
LHRC mmeniudhi, kwanini mnamualika huyu muuaji? Mvunja sheria? Wewe Dada Mkuu wa LHRC hapo umepotea njia kabisa. Afadhali kuacha kufanya huo uzinduzi kuliko kumwalika huyu mtu!
 
Back
Top Bottom