Lugha kama silaha au adui wa...

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,458
956
Je umewahi kujiuliza ni kwa jinsi gani kiswahili chetu kitamu cha Tanzania kinavyochangia kudumaza au kurudisha nyuma maendeleo au harakati za kuondoa uovu katika jamii?

Hebu angalia mifano michache:

1. Watu hawa watafikishwa mbele ya vyombo husika na kuchukuliwa hatua kali za kisheria ( Je ni vyombo gani? nani atakusika kwa minajili ya uwajibikaji? lini hatua hizo zitachukuliwa?)- kauli kama hii inajenga matumaini makubwa lakini ndani hamna kitu!

2. Jambo hili linafanyiwa kazi ( kazi gani?,nani anafanyia kazi? atafanya kazi hiyo katika timeframe gani? lini watu watarajie matokeo?)- kauli hii inanyamzisha maswali zaidi

3. Kwa sababu zisizozuilika nimechelewa kidogo (tutajuaje kweli hazikuwa zinazuilika? mtu anaweza kulala baada ya kukesha kwenye starehe akachelewa kufika sehemu husika na kutoa statement kama hii na ikawa mwisho wa mazungumzo) - kauli hii inamaanisha usiniulize wala usitake kujua zaidi...

Unaweza kuongeza mifano mingine mingi tu....

Swali:

1.Tukiendekeza misemo kama hii, hatuoni tunazidi kuwa wadanganyika maana semi kama hizi zinafunga mazungumzo, haziruhusu mijadala wala uwajibikaji/uwajibishaji?

2. Wale wataalamu wa lugha, hamuwezi kuja na lugha mbadala yenye ku leta mabadiliko na kuchagiza uwajibikaji zaidi?
 
Naendeleleza mada:

Fikiria nini kilitokea miaka ya mwisho ya sabini ( 1978-79) pale baba wa Taifa alipoamua kutumia lugha hii hii ya kiswahili na kusema..

SABABU YA KUMPIGA TUNAYO.....
NIA TUNAYO
UWEZO TUNAO......

NADHANI WANANCHI WALIOSIKILIZA HOTUBA YA MWALIMU PALE OFISI ZA CCM KIRUMBA MWANZA WATAKUJA WATUAMBIE NINI KILITOKEA BAADA YA HAPO!

IDDI AMIN DADA ALIPATA KIPONDO KUTOKA KWA WATANZANIA... WOTE BILA KUJALI MTU NI MWANAJESHI AU LA!

Simulizi zinasema kuwa hadi wanafunzi waliokuwa wamemaliza kidato cha sita na kwenda JKT waliingia vitani na kupigana kwa nia na ujasiri kabisa hadi kumtoa nduli ndani ya mipaka...

Iweje siku hizi imeshindikana kutumia maneno mazito yenye kugusa hisia za watu kupambana na maovu?

Hata mada hii hakuna anayechangia kwa maana tumeridhika kabisa na yale yanayotamkwa kutupumbuza!

UWEZO WA KUMPIGA TUNAO!!!
 
Dada nimemiss kauli moja hapo."mkubwa hatofika kwa sababu zisizozuilika" haya mambo yapo bongo sana . umenikumbusha home.
 
Kauli ambazo mimi huwa zinanikera sana zinazotumiwa na the so called "Viongozi" ni hizi inabidi tujipange upya na ukiangalia hakuna kujipanga upya kokote miaka nenda miaka rudi ni ufisadi tu na nchi haipigi hatua kimaendeleo.

Halafu kuna hii kauli nyingine
swala hili inabidi lifanyiwe mchakato wa kina lakini ukiangalia hakuna mchakato wowote unaofanyika maana kila kukicha na madudu yale yale
 
kwanza dada nataka ujue kuwa lugha ni "sauti za nasibu" hivyo hakuna mtu anaweza kukaa chini na akaja na "maneno mbadala" bali maneno ya lugha huzuka yenyewe na watumiaji hujikuta tu wameshamirisha kutumia maneno yenyewe kuwasilisha maana anuai zilizokusudiwa (na hapa sizungumzii suala zima la usanifu wa lugha)

kuna maneno yalizuka siku za karibuni na kutoa mchango mkubwa japao watu wa siku hizi tu tofauti kidoko katika kudodosa. mfan maneno "ARI MPYA, NGUVU MPYA KASI MPYA" hya yalitoka katika hotuba ya kikwete akitangaza nia yake ya kuchukua fomu kukiomba chama chake kimteue kugombea urais. toka hapo yamesikika mra nyingi na wote tunajua alifanikiwa kuteuliwa na kushinda uchaguzi, hivyo ni maneno yaliyofanikiwa lengo lake. hata wanaohoki leo utelelezaji wa ahadi zake huyarejea tene na tene manaeno yale ili kueleweka zaidi kama si kutanabaisha.

kwa maoni yangu, tusichukie maneno bali tuhoji mantiki na matumizi yake huku tukitambua kuwa watumiaji wake hawana uchaguzi bali kutumia kama hayo ndiyo yako kwenye maumizi kwa wakati huo (misimu)
 
mimi nimeipenda avator yako WOS!
it looks like ndivyo ulivyo....:D
 
Lugha za siku hizi ni porojo tu hakuna utekelezaji ndo maana ukiwa unaongea saaaaana unaitwa mwanasiasa
 
Naendeleleza mada:

Fikiria nini kilitokea miaka ya mwisho ya sabini ( 1978-79) pale baba wa Taifa alipoamua kutumia lugha hii hii ya kiswahili na kusema..

SABABU YA KUMPIGA TUNAYO.....
NIA TUNAYO
UWEZO TUNAO......

NADHANI WANANCHI WALIOSIKILIZA HOTUBA YA MWALIMU PALE OFISI ZA CCM KIRUMBA MWANZA WATAKUJA WATUAMBIE NINI KILITOKEA BAADA YA HAPO!

IDDI AMIN DADA ALIPATA KIPONDO KUTOKA KWA WATANZANIA... WOTE BILA KUJALI MTU NI MWANAJESHI AU LA!

Simulizi zinasema kuwa hadi wanafunzi waliokuwa wamemaliza kidato cha sita na kwenda JKT waliingia vitani na kupigana kwa nia na ujasiri kabisa hadi kumtoa nduli ndani ya mipaka...

Iweje siku hizi imeshindikana kutumia maneno mazito yenye kugusa hisia za watu kupambana na maovu?

Hata mada hii hakuna anayechangia kwa maana tumeridhika kabisa na yale yanayotamkwa kutupumbuza!

UWEZO WA KUMPIGA TUNAO!!!

Maneno hayo pamoja na mengine ni namna ya kuwapumbaza audience wanaosilikiliza ili wawe wapole.

Lakini viongozi haohao utaona wanavyohaha kwa mfano wakiandikwa kwenye vyombo vya habari.

Kuna WAKATI taasisi ninayofanyia kazi iliandikwa vibaya kwenye gazeti, basi tulipelekwa mchakamchaka ofisi nzima. Mabosi walituendesha ka vishada.

Wengine walitumwa kwa Mkuu wa Mkoa, wengine kwenye NYUMBA ZA Media, wengine kwa wauza magazeti, na wengine mawizarani- yaani siku 3 ni balaa ofisini.


Basi masuala yote yangekuwa yanashughulikiwa kama hivi huku maofisini, tungekuwa mbele kama CHINA, TAIFA NINALOLIADMIRE SANA(SIONGELEI BIDHAA FEKI).
 
kwanza dada nataka ujue kuwa lugha ni "sauti za nasibu" hivyo hakuna mtu anaweza kukaa chini na akaja na "maneno mbadala" bali maneno ya lugha huzuka yenyewe na watumiaji hujikuta tu wameshamirisha kutumia maneno yenyewe kuwasilisha maana anuai zilizokusudiwa (na hapa sizungumzii suala zima la usanifu wa lugha)

kuna maneno yalizuka siku za karibuni na kutoa mchango mkubwa japao watu wa siku hizi tu tofauti kidoko katika kudodosa. mfan maneno "ARI MPYA, NGUVU MPYA KASI MPYA" hya yalitoka katika hotuba ya kikwete akitangaza nia yake ya kuchukua fomu kukiomba chama chake kimteue kugombea urais. toka hapo yamesikika mra nyingi na wote tunajua alifanikiwa kuteuliwa na kushinda uchaguzi, hivyo ni maneno yaliyofanikiwa lengo lake. hata wanaohoki leo utelelezaji wa ahadi zake huyarejea tene na tene manaeno yale ili kueleweka zaidi kama si kutanabaisha.

kwa maoni yangu, tusichukie maneno bali tuhoji mantiki na matumizi yake huku tukitambua kuwa watumiaji wake hawana uchaguzi bali kutumia kama hayo ndiyo yako kwenye maumizi kwa wakati huo (misimu)
Tuko pamoja Mkuu!
Hii mada inalenga haswa kuuliza/kuhoji misemo isiyoleta tija.Ile ambayo ina mashiko tuiendeleze.
Tuendelee kuainisha -
 
Nafikiri mada yako iko sahihi lakini ndio muundo wa lugha na ukitaka kuondoa haya hakika utapoteza ladha na chachu ya lugha yeyote ile. Kumbuka sio Kiswahili tu kina stahili hizi ila ni lugha zote. Wazo langu ni kuwa kinachohitajika ni nidhamu ya kila mtu kutokana a kile anachiotakiwa kukisema na kukitenda lakini sio kuiondolea lugha utamu na uhalisia wake
 
Nafikiri mada yako iko sahihi lakini ndio muundo wa lugha na ukitaka kuondoa haya hakika utapoteza ladha na chachu ya lugha yeyote ile. Kumbuka sio Kiswahili tu kina stahili hizi ila ni lugha zote. Wazo langu ni kuwa kinachohitajika ni nidhamu ya kila mtu kutokana a kile anachiotakiwa kukisema na kukitenda lakini sio kuiondolea lugha utamu na uhalisia wake
Sipo
Asante kwa mchango wako ndugu yangu.
Naomba unisome katikati ya mistari..... simaanishi kuondoa utamu kwenye lugha au maneno ya kiswahili.
 
kwa mtazamo wangu hapa hakuna tatizo na lugha wala lugha bali ni kauli za kisiasa ndizo zilizojaa katika kila idara iwe ya serikali au binafsi na kauli hizi zinalenga kuficha dhana nzima ya uwajibikaji ukizingatia hatujaweka chombo cha kufuatilia uwajibikaji na ndio maana zimekuwa ni kauli za msingi hasa muhusika anapokuwa hana jibu la msingi au maelezo thabiti kwa wahusika.
Kauli hizi kwa sasa zinapitiliza mpaka kwenye vyombo vya dola mfano kila siku utasikia Msako mkali umeanzishwa/unaendelea lakini usitarajie kupata mlisho nyuma baada ya kauli hiyo kupita.
Kwa ujumla ni kauli za funika kombe mwanaharamu apite.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom