Sophist
Platinum Member
- Mar 26, 2009
- 4,484
- 3,400
It is not a fiction we are used to like those authored by African writers; Ngugi wa Thiongo, Chinua Achebe, Ole Soyinka and other you know.. not, it is real life experience;
Kitabu cha The Dark Side of Nyerere, ni simulizi ya kweli ya masaibu aliyoata Ludovick Mwijage kwenye utawala wa Nyerere. Ludovick Mwijage alikuwa mmoja wa wakosoaji wakubwa wa mfumo wa utawala wa Mwl Nyerere ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania.
Katika kitabu hiki cha the dark side of Nyerere's legacy Mwandishi anaanza kwa kurejea Jiji la Manane huko Afrika ya Kusini,mnamo Desemba 6 mwaka 1983,akiwa amemaliza kula mlo wa mchana akiwa na rafiki yake John kutoka Kenya ambaye alikuwa fundi wa magari, na wakati fulani ndie alikuwa akatengeneza gari ya Mfalme Moshoeshoe wa Lesotho, katika mazungumzo yao huyu mkenya alimjulisha mwandishi kuwa passport yake ilikuwa imechukuliwa hotelini kutokana na kushindwa kulipa deni la hoteli.
Mwijage anasema alikimbilia Mbambane kutafuta hifadhi baada ya hali yake kuwa. mbaya Tanzania, Ludovick Mwijage alikuwa mmoja wa wakosoaji wakubwa wa mfumo wa utawala wa Mwl Nyerere ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania,mwanzoni alikimbilia Nairobi Kenya ambako aliwekwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Thika, ila baadae aliona Kenya sio salama kwake,akaamua kukimbilia Swaziland Januari 1983. Kasisi mmoja wa kanisa Katoliki kutoka Ujerumani ndie aliyempa mwandishi kiasi cha 4200 Kenya shillings, ambayo ingemtosha kulipia tiketi ya Ndege kupitia Sudan ila alilazimika kuwapa marafiki zake wawili waliokuwa wametorokea Uganda ili waingie Sudan, maana Uganda bado ilikuwa na maofisa wengi wa usalama kutoka Tanzania! hawa rafiki zake waliokuwa wanakimbia mkono wa Nyerere hawakuwa na fedha tena, aliwatumia kiasi fulani na yeye Mwijage akatafuta hela zaidi kutoka kwa rafiki zake wa ng'ambo.
Mwijage anasema wakati anaondoka Kenya kwa msaada wa rafiki zake wa Ng'ambo hasa Ujerumani Mashariki, hakuwa na chochote zaidi ya mswaki,dawa ya meno, singlend, nguo moja ya ndani ya kubadili na karatasi zilizokuwa na mawasiliano ya rafiki zake wa Tanzania na Ujerumani. Wakati huo ukiwa na pasipoti ya nchi wanachama wa jumuia ya madola hakukuwa na haja ya visa kwenye nchi wanachama! alifika Mbabane akatoka na kuanza kutafuta sehemu gesti ya kufikia. Akiwa kwenye mitaa kutafuta sehemu ya kufikia ghafla alikutana na Mtanzania ambaye alikuja kugundua ni mtabiri maarufu wa nyota Sheikh Yahya Hussein.
Alitambua Sheikh Yahya Hussein kutokana na kumwona kwenye magazeti mbalimbali akitangaza biashara yake ya utabiri. Hapa Mbabane alikuja kwa kazi hiyo ambayo alikuwa anajiita Mtabiri, Nabii, Mnajimu, Mponyaji, ukiwa na tatizo lolote yeye anasafisha nyota yako! Sheihk Yahaya alimkaribisha nyumbani na kwa kuwa alikuwa ni Sheikh Mwandishi hakuwa na wasiwasi, walipofika Yahya alimtaka Mwandishi aeleze kisa chake, hata hivo Sheikh Yahaya alikuwa anajua kisa cha Mwijage. Sheikh Yaya alijitolea kumlipia gesi kwa siku kadhaa!
Katika mazingira ambayo ni tatanishi mwandishi alijikuta baadhi ya nyaraka zake hazionekani
Hata hivo nchi ya Swaziland ilimpa hati ya mkimbizi wa kisiasa ndani ya wiki moja.Mwandishi anasema kuwa anakumbuka mazungumzo yake na yule Mkenya kuhusu siasa za Afrika na Afrika Mashariki,kwa sehemu kubwa watu wasio Watanzania walikuwa anamwona Nyerere shujaa wa Afrika hasa imani yake ya Ujamaa na kwamba Mwafrika ni socialist kwa asili!ndivo aliamini Nyerere!
Aliamini tofauti na alishangaa Afrika kuwa maskini, na ukosefu wa Demokrasia,Mwijage aliamini ukosefu wa Demokrasia na mfumo wa vyama vingi ni kinyume na haki za binadamu na kwamba ingechelewesha maendeleo ya vitu na ya watu!pia ingepelekea utegemezi wa wahisani kwa kipindi kirefu sana.
Kusoma zaidi chukua kitabu kilichokuwa attached hapo chini
Kitabu cha The Dark Side of Nyerere, ni simulizi ya kweli ya masaibu aliyoata Ludovick Mwijage kwenye utawala wa Nyerere. Ludovick Mwijage alikuwa mmoja wa wakosoaji wakubwa wa mfumo wa utawala wa Mwl Nyerere ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania.
Katika kitabu hiki cha the dark side of Nyerere's legacy Mwandishi anaanza kwa kurejea Jiji la Manane huko Afrika ya Kusini,mnamo Desemba 6 mwaka 1983,akiwa amemaliza kula mlo wa mchana akiwa na rafiki yake John kutoka Kenya ambaye alikuwa fundi wa magari, na wakati fulani ndie alikuwa akatengeneza gari ya Mfalme Moshoeshoe wa Lesotho, katika mazungumzo yao huyu mkenya alimjulisha mwandishi kuwa passport yake ilikuwa imechukuliwa hotelini kutokana na kushindwa kulipa deni la hoteli.
Mwijage anasema alikimbilia Mbambane kutafuta hifadhi baada ya hali yake kuwa. mbaya Tanzania, Ludovick Mwijage alikuwa mmoja wa wakosoaji wakubwa wa mfumo wa utawala wa Mwl Nyerere ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania,mwanzoni alikimbilia Nairobi Kenya ambako aliwekwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Thika, ila baadae aliona Kenya sio salama kwake,akaamua kukimbilia Swaziland Januari 1983. Kasisi mmoja wa kanisa Katoliki kutoka Ujerumani ndie aliyempa mwandishi kiasi cha 4200 Kenya shillings, ambayo ingemtosha kulipia tiketi ya Ndege kupitia Sudan ila alilazimika kuwapa marafiki zake wawili waliokuwa wametorokea Uganda ili waingie Sudan, maana Uganda bado ilikuwa na maofisa wengi wa usalama kutoka Tanzania! hawa rafiki zake waliokuwa wanakimbia mkono wa Nyerere hawakuwa na fedha tena, aliwatumia kiasi fulani na yeye Mwijage akatafuta hela zaidi kutoka kwa rafiki zake wa ng'ambo.
Mwijage anasema wakati anaondoka Kenya kwa msaada wa rafiki zake wa Ng'ambo hasa Ujerumani Mashariki, hakuwa na chochote zaidi ya mswaki,dawa ya meno, singlend, nguo moja ya ndani ya kubadili na karatasi zilizokuwa na mawasiliano ya rafiki zake wa Tanzania na Ujerumani. Wakati huo ukiwa na pasipoti ya nchi wanachama wa jumuia ya madola hakukuwa na haja ya visa kwenye nchi wanachama! alifika Mbabane akatoka na kuanza kutafuta sehemu gesti ya kufikia. Akiwa kwenye mitaa kutafuta sehemu ya kufikia ghafla alikutana na Mtanzania ambaye alikuja kugundua ni mtabiri maarufu wa nyota Sheikh Yahya Hussein.
Alitambua Sheikh Yahya Hussein kutokana na kumwona kwenye magazeti mbalimbali akitangaza biashara yake ya utabiri. Hapa Mbabane alikuja kwa kazi hiyo ambayo alikuwa anajiita Mtabiri, Nabii, Mnajimu, Mponyaji, ukiwa na tatizo lolote yeye anasafisha nyota yako! Sheihk Yahaya alimkaribisha nyumbani na kwa kuwa alikuwa ni Sheikh Mwandishi hakuwa na wasiwasi, walipofika Yahya alimtaka Mwandishi aeleze kisa chake, hata hivo Sheikh Yahaya alikuwa anajua kisa cha Mwijage. Sheikh Yaya alijitolea kumlipia gesi kwa siku kadhaa!
Katika mazingira ambayo ni tatanishi mwandishi alijikuta baadhi ya nyaraka zake hazionekani
Hata hivo nchi ya Swaziland ilimpa hati ya mkimbizi wa kisiasa ndani ya wiki moja.Mwandishi anasema kuwa anakumbuka mazungumzo yake na yule Mkenya kuhusu siasa za Afrika na Afrika Mashariki,kwa sehemu kubwa watu wasio Watanzania walikuwa anamwona Nyerere shujaa wa Afrika hasa imani yake ya Ujamaa na kwamba Mwafrika ni socialist kwa asili!ndivo aliamini Nyerere!
Aliamini tofauti na alishangaa Afrika kuwa maskini, na ukosefu wa Demokrasia,Mwijage aliamini ukosefu wa Demokrasia na mfumo wa vyama vingi ni kinyume na haki za binadamu na kwamba ingechelewesha maendeleo ya vitu na ya watu!pia ingepelekea utegemezi wa wahisani kwa kipindi kirefu sana.
Kusoma zaidi chukua kitabu kilichokuwa attached hapo chini