Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,561
- 19,056
Kuna mjadala mzuri ulikua unaendelea kwenye chanel ya UTV ambapo CAG mstaafu Bwana Ludovic Uto ameunga mkono hoja za Wabunge wanaotaka ufanyike ukaguzi kuhusu deni la taifa. Pamoja nae alikua ni Professor Ngowi na Dr Bernie.
Ludovic Uto ameenda mbali zaidi na kutaka ifanyike ukaguzi maalum(Special Audit) ili kuibua mambo kadhaa kuhusiana na deni la Taifa.
Wamesema Bunge ni vizuri likaiandikia ofisi ya CAG na kuitaka ifanye ukaguzi huo na Bunge litengeneze Hadidu za rejea maalum kwa ukaguzi huo ili kuibua mambo yote yanayotakiwa kujulikana na kuwekwa wazi kwa walipaji wa deni hilo ambao ni wananchi.
Wote wamesama kimsingi Wananchi ndio wamekasimu mamlaka ya kukopa kwa serikali na wanahaki ya kujua pesa zilizokopwa zimefanyia nini na kwa kiasi gani.
Wote wameipongeza hatua ya serikali ya awamu ya sita kwa uwazi wa kuwataarifu wananchi kua wamekopa na kuweka mchanganuo wa matumizi ya pesa hizo mpaka senti ya mwisho.
Maoni yangu ni kwamba, hatua hiyo ni muhimu na nzuri ila inabidi kuchukua tahadhari kwani kuna uwezekano wa kuleta mpasuko baina ya waungaji mkono wa serikali ya awamu ya tano na hii ya Mama Samia.
Ludovic Uto ameenda mbali zaidi na kutaka ifanyike ukaguzi maalum(Special Audit) ili kuibua mambo kadhaa kuhusiana na deni la Taifa.
Wamesema Bunge ni vizuri likaiandikia ofisi ya CAG na kuitaka ifanye ukaguzi huo na Bunge litengeneze Hadidu za rejea maalum kwa ukaguzi huo ili kuibua mambo yote yanayotakiwa kujulikana na kuwekwa wazi kwa walipaji wa deni hilo ambao ni wananchi.
Wote wamesama kimsingi Wananchi ndio wamekasimu mamlaka ya kukopa kwa serikali na wanahaki ya kujua pesa zilizokopwa zimefanyia nini na kwa kiasi gani.
Wote wameipongeza hatua ya serikali ya awamu ya sita kwa uwazi wa kuwataarifu wananchi kua wamekopa na kuweka mchanganuo wa matumizi ya pesa hizo mpaka senti ya mwisho.
Maoni yangu ni kwamba, hatua hiyo ni muhimu na nzuri ila inabidi kuchukua tahadhari kwani kuna uwezekano wa kuleta mpasuko baina ya waungaji mkono wa serikali ya awamu ya tano na hii ya Mama Samia.