Lubuva Mwenyekiti mpya Tume ya Uchaguzi!

Hivyo unaona ni sahihi kumteua kwa kuwa ni mwanachama wa chama kilichozoeleka! Hapo ndipo unapokosea; mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ndiye refa wa uchaguzi, akisema huyu kashinda hakuna wa kuuliza wala kukata rufaa mahakamani, sasa kama mwanaccm anataeuliwa kwa uccm wake atatoaje haki kwa cuf? - Tafakari, mnaipeleka nchi pabaya!

Kwa nchi hii kukupa Nafasi ya aina hiyo, wamepekua hadi damu yak, itikadi yako, misimamo yako, mapenzi yako kwa wakulu, mwelekeo wako wa familia, hadi unavyolala na unavyoamka. Anyway, ngoja tuone utendaji wake.
 
Halafu kwa nini hawa wenyeviti wote wanakuwa majaji?

Majaji ndio wanaonekana wana gravita katika kuamua with impartiality na wanaelewa mambo ya katiba na sheria za uchaguzi zaidi it seems.

But as long as they are chosen by the president all that aura of impartiality is tainted.
 
Majaji ndio wanaonekana wana gravita katika kuamua with impartiality na wanaelewa mambo ya katiba na sheria za uchaguzi zaidi it seems.

But as long as they are chosen by the president all that aura of impartiality is tainted.

Majaji nao huwa ni political appointees tu. Can you imagine eti Antonin Scalia ndo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi USA...lol.

Ingependeza zaidi kama hao wenyeviti wangekuwa sio political appointees kama religious leaders but then again hiyo nayo itazua zogo tu.
 
Haya ndiyo mamlaka ya Raisi kwa mujibu wa katiba iliyopo... Pengine kwa katiba mpya tunanotarajiwa kuiandika WOTE tutaainisha nini maana ya Tume huru ya uchaguzi na inapatikanaje? wenzetu walio kwenye demokrasia zilizoendelea ( za miaka mingi) tume hizi zinaongozwa na watu wasiojitambulisha na chama chochote cha siasa ili wawe kweli huru na ushawishi wa siasa za vyama!!! Si vibaya sisi tukaiga hilo..
 
haya ndiyo mamlaka ya raisi kwa mujibu wa katiba iliyopo... Pengine kwa katiba mpya tunanotarajiwa kuiandika wote tutaainisha nini maana ya tume huru ya uchaguzi na inapatikanaje? Wenzetu walio kwenye demokrasia zilizoendelea ( za miaka mingi) tume hizi zinaongozwa na watu wasiojitambulisha na chama chochote cha siasa ili wawe kweli huru na ushawishi wa siasa za vyama!!! Si vibaya sisi tukaiga hilo..
wasio jitambulisha na chama chochote = na wasio na chama chochote? Human action can not be fully understood.
 
Haya ndiyo mamlaka ya Raisi kwa mujibu wa katiba iliyopo... Pengine kwa katiba mpya tunanotarajiwa kuiandika WOTE tutaainisha nini maana ya Tume huru ya uchaguzi na inapatikanaje? wenzetu walio kwenye demokrasia zilizoendelea ( za miaka mingi) tume hizi zinaongozwa na watu wasiojitambulisha na chama chochote cha siasa ili wawe kweli huru na ushawishi wa siasa za vyama!!! Si vibaya sisi tukaiga hilo..
Thats the bottom line, so lets hope he has good intentions on the new constitution issue.
 
jaji Lubuva namuamini ila sasa huyo aliyekuwa kwenye mikataba sijui manake kilik cha nchi hii kimekuwa ni mikataba kila kukicha. sasa unapoona mtu wa mikataba anapewa rungu kubwa kama hili inabidi ujiulize maswali kidogo.
 
Hivi sifa mojawapo ya kushika hizi nafasi ni kuwa mstaafu, mm naona mtu akiwa mstaafu anaweza kutumiwa kirahisi kwa kuwa hana cha kupoteza. Hii bado ni tume ya uchaguzi ya CCM.
 
kwa mtindo wa kuajiri wababu serikali inamaanisha no rum for new blood. 10years experience ivi kwa mhitimu wa mwaka huu ataajiriwa mwaka gani?2022? mh rais ebu achana na vibabu,chagua wenye uchungu na nchi yao wala si kuchagua akina makame ambao wamefikia mwisho kwenye lifespan na hawana la kupoteza pindi wakitupeleka kwenye machafuko. tz si salama.
 
Jamani labda mie ndo sielewi!
Hivi mtu akistaafu ina maana gani? Mie nadhani ukistaafu maana yake hata uwezo wa kupambanua mambo unakuwa umeshuka kwa kiasi fulani. Haina maana kwamba huwezi kufanya kazi bali kuna mambo fulani inakuwa ngumu kuyatekeleza. Sasa hili la kuteua wastaafu kusimamia idara nyeti kama ya Tume ya uchaguzi limekaaje? Hii kwangu ni kuziba ajira kwa wengine kwani mtu akistaafu nafasi yake inachukuliwa na mwingine. Sasa hili la kutengeneza ajira mpya linakuwaje wakati waliostaafu ndo wanateuliwa upya kushika nyadhifa! Imekuwa ni jambo la kawaida raisi wetu kufanya uteuzi kwa wastaafu kwa mfano wakuu wa mikoa, jeshi, idara mbalimbali na hata baadhi ya wakuu wa wilaya!
Hivi hii imekaaje?
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Damian Lubuva kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Aidha, Rais Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Hamid Mahmoud Hamid kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Bwana Julius Benedicto Mallaba kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi.

Taarifa iliyotolewa leo, Alhamisi, Desemba 22, 2011 na Katibu Mkuu Kiongozi, Bwana Phillemon L Luhanjo mjini Dar es Salaam imesema kuwa uteuzi huo umeanza tokea Jumatatu, Desemba 19, mwaka huu, 2011.

Kabla ya uteuzi wake, Mheshimiwa Lubuva alikuwa Jaji katika Mahakama ya Rufani Tanzania na baada ya kustaafu aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili ya Viongozi.

Mheshimiwa Lubuva anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mheshimiwa Jaji Lewis Makame ambaye mkataba wake wa utumishi wa umma ulifikia mwisho Julai, mwaka huu, 2011.

Naye Mheshimiwa Hamid alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kabla ya kustaafu kwake na anachukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Mhe Jaji Omari O. Makungu. Mheshimiwa Jaji Makungu aliteuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na baadaye akateuliwa kuwa Jaji Mkuu.

Naye Bw. Mallaba, kabla ya uteuzi wake, alikuwa Mkurugenzi wa Sehemu ya Mikataba (Contracts and Treaties) katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. **Bw. Mallaba anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Rajabu Kiravu ambaye amemaliza mkataba wake wa utumishi Septemba, mwaka huu, 2011.

Imetolewa na:

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

22 Desemba, 2011
 
Naona hili la tume huru ya uchaguzi mpaka likemewe na wakubwa naona ndo viserikali vya nchi maskini kama Tz wanaweza tekeleza.
Or else tufanye kama Egypt
 
Hivi sifa mojawapo ya kushika hizi nafasi ni kuwa mstaafu, mm naona mtu akiwa mstaafu anaweza kutumiwa kirahisi kwa kuwa hana cha kupoteza. Hii bado ni tume ya uchaguzi ya CCM.

Inasadia kukuza ajira za vijana. Hata hivyo wenye "uzoefu" ni wachache .
Ndio maana kuna watu ubunge kwao ni kazi n utumishi wa umma ila wengine ubunge ni kituo cha pension. Hii tume ya uchaguzi inaonekana wazi ni kituo cha Pension kwa majaji

 
Wazee kama hawa wangetakiwa kupumzika kuwapa majukum magumu kama haya ni hasara kwao,aliyewateua,na taifa kwa ujumla coz efficient will be zero.
Kenya baada ya katiba mpya wazee kama hawa ni nadra kupata nafasi. Hakuna uteuzi unaofanywa na rais direct. Usaili unafanyika na rais anapewa jina au majina ya watu waliofanya vizuri ndipo anateua na hata akiteua hawana kazi mpaka wapitishwe na bunge. Katiba mpya ni dawa ya matatizo. Kenya itapaa kama watampata mrithi wa Kibaki aliye na msimamo. Wakijroga kuchagua wezi kama Uhuru Kenyata na kumwacha Kamanda aliyewapeleka hapo kwa kukokota mkokoteni unaoitwa Kenya yaani Raila watarudi nyuma enzi za Moi.
 
Hongera Jaji(Mst) Lubuva!
Nafasi hii ni changamoto kubwa sana kwa miaka hii, na unahitaji kuchezea kwenye fair playground, vinginevyo utakuwa KIMUNYA wa Kenya!


awe mara mbili
wasanii wa kikwete ujawajua mpaka sasa jamani
awe
 
jk anachagua wastaafu vijana wapate wapi ajira, pili hawa wazee wamefikia ukomo wa kufikiria hawawezi kufiri kisasa, wataleta mambo ya miaka 47 iliyopita

hakuna jipya nalaani kitedo hiki
 
Back
Top Bottom