Lowassa tena Yumo: Ufisadi Madawa MSD

Kubwajinga

JF-Expert Member
Jan 23, 2008
2,194
297
Ufisadi mkubwa tena: Dawa hizi ni hatari kwa Binadamu

-----------------------------------------------------------------

Hiki ni kipindi pekee cha vugu vugu la kuhanika ufisadi. Hivi mtumishi wa serikali anapoagiza nje na kuuza dawa kwa wananchi za kuhatarisha maisha ya wanawake wakati wa kujifungua , eti kwa kuwa kapewa dau kubwa toka kwa Mhindi(mtengenezaji), huo ni ufisadi au ufirauni?

Mambo haya yanafanyika Medical Stores Department (MSD). Krugenzi ya ununuzi imekuwa inafanya mambo yasiyo ya kibinadamu kwa Watazania, kwa kuingia mikataba yenye maslahi yao tu, na hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa dawa katika Zahanati na vituo vya afya. Ni asilimia 60% tu upatikana kwa wananchi na si kwa wakati muafaka.

Mkurugenzi Mkuu ambaye alipatiwa kazi hiyo akitokea Marekani ambako aliishi kwa miaka mingi, hana ufahamu mzuri juu ya shughuli zote za MSD, na hivyo anapodanganywa chochote hawezi kujinasua. Amekubali ushauri mwingi potofu, na hivo manunuzi mengi yanafanywa kwa matakwa ya mkurugenzi wa ununuzi na maofisa wake! Director General(DG) wa MSD ambaye ni mototo wa aliyekuwa IGP, Phillemon Mgaya alibebwa sana na fisadi wa kimataifa Mh. Edward Lowasa( Lowasa ni rafiki wa karibu wa Phillemon Mgaya) ili kuogezewa mkataba wa miaka miwili tangia Januari 2008.
Manuanuzi ya ajabu yaliyofanyika:

  1. Maji ya uchungu(Oxytocin Injection) ambayo ni dawa ya kuongeza uchungu kwa kinamama wakati wa kujifungua, ilinunuliwa kwa wingi na ki maajabu toka India kwa Vital Healthcare(mojawapo ya batch ni V7137). Zilinunuliwa container 3. Dawa hii hivi sasa ni sumu, maana zimetunzwa kwenye joto la kawaida la 30oC badala ya 2-8oC, hii ni kutokana na kwamba MSD ina uwezo wa kutunza vitu katika ubaridi si zaidi ya robo container. Hata hivyo wafisadi wa krugenzi ya ununuzi walimshauri Vital healthcare afute (kwa mark pen) kwenye kasha la nje, maagizo juu ya utunzaji katika ubaridi. Dawa hizi sasa hivi zinauzwa kwa vituo vyote vya serikali, zinatunzwa katika joto la Dar, ila chupa za ndani zinaonyesha mahitaji kamili ya joto la 2-8oC. Ubadhilifu huu ulimwingizia mkurugenzi wa ununuzi dolla za marekani 27,000.
  2. Mwishoni mwa Mwaka jana zilinunuliwa container 150 za futi 40 za maji ya kuwawekea wagonjwa mwilini. Ujazo huu unazidi uwezo wa MSD kutunza mizigo hii kwa asilimia 100, na unazidi mahitaji ya nchi kwa miaka mine.Maji haya yalikaa juani kwenye ma container kwa miezi kadhaa baada ya bohari zote kujaa sana na mengine yalilazimishwa kwenda kanda zote za MSD bila mafanikio.Inakisiwa maji haya yataisha mwaka 2010, ingawaje muda wake wa kuisha matumizi ni 2009. Fununu zilizopo ni kwamba ufirauni huu ulifanywa baada ya kampuni inayotengeneza maji hayo kutoa dau la dolla za marekani 120,000 kwa mkurugenzi na ofisa wa ununuzi. Mwenyekiti wa MSD tender bodi ambayye si mtaaluma kabisa wa madawa au manunuzi yalimpita pembeni.
  3. Madawa ya kupunguza makali ya virus ya ukimwi(ARVs imekuwa chanagmoto mpya kwa DG na MSD. Mpaka leo hii DG ajui kwamba kukosekana kwa dawa hizi ni kazi ya ufirauni wa krugenzi ya ununuzi . Dawa hizi zimepungua sana tangia November 2007, hadi leo hii, Global Fund na PEPFAR wanajua fika kinachotokea MSD , ila DG haelewi kuwa anaingizwa mtatani. Tender na mikataba vinatolewa kwa watu waliokwisha jijenga kwa Krugenzi ya Ununuzi. Mikataba ikishatolewa na maofisa uchukua chao, na kwaida mtu akisha kupa ongo ataleta dawa kwa wakati anapotaka na quality anayotaka. Sababu hiyo imesababisha dawa kutokuja kwa wakati. Imefikia wakati wanapigwa vita vikali sana watengenezaji wa dawu hizi wa hapa nchi wasiuze dawa zao katika soko la nchi hii. Mfano mzuri ni Kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical industries (TPI) ambacho licha ya kupewa changamoto na serikali kuanza kuzalisha dawa hizi hapa nchini ili kuuwanusuru wananchi, kimekuwa kikiwekewa vikwazzo vingi sana na krugenzi ya ununzi.
Je tutafika kama afya ya mtu inawekwa rehani?






NB: Hii posting imetoka kwa pntimba ambaye bado ni jr member. Ilikuwa misplaced.
 
Inawezekana Ni Marafiki Tu Na Hawahusiani Chochote Katika Utendaji Wa Shirika Hilo

Mleta Hoja Unaweza Kutueleza Lowassa Anahusika Vipi Katika Uendeshaji Wa Shirika Hilo ? Na Wwewe Ulifanya Jitihada Gani Za Kuhakikisha Taarifa Ulizoleta Ni Ukweli Hazina Chembe Yoyote Ya Uwongo ?

Kama Ni Ukweli Je Utakuwa Tayari Kwenda Kula Kiapo Kusema Ukweli Zaidi Wa Yale Unayoyajua ?
 
Zilinunuliwa container 3. Dawa hii hivi sasa ni sumu, maana zimetunzwa kwenye joto la kawaida la 30oC badala ya 2-8oC, hii ni kutokana na kwamba MSD ina uwezo wa kutunza vitu katika ubaridi si zaidi ya robo container. Hata hivyo wafisadi wa krugenzi ya ununuzi walimshauri Vital healthcare afute (kwa mark pen) kwenye kasha la nje, maagizo juu ya utunzaji katika ubaridi. Dawa hizi sasa hivi zinauzwa kwa vituo vyote vya serikali, zinatunzwa katika joto la Dar, ila chupa za ndani zinaonyesha mahitaji kamili ya joto la 2-8oC. Ubadhilifu huu ulimwingizia mkurugenzi wa ununuzi dolla za marekani 27,000.


KubwaJINGA nashauri ufanye ziara MSD head office kule keko siku moja. Ukiongelea miundo mbinu, MSD ni moja ya idara za serikali zenye high quality of storage facilities. Miundo mbinu ya kuhifadhia dawa imeboreshwa kiasi cha kutosha. Madawa yanatunzwa kwatika joto la aina tofauti kutokana na mahitaji yake.

Point yako haipo clear sana, labda ufafanue kuhusu ufisadi hapo?!!

MSD ninayoifahamu ina wataalamu wa kutosha wa madawa na wa warehousing. Sidhani kama wanaweza kuhifadhi dawa kama ulivyosema! Pale wana idara ya ukaguzi wa quality madawa na vifaa vinavyoingia na wanafanya kazi hii kwa kushirikiana na mamlaka ya chakula na madawa.

Kwenye quality inspection mara nyingi kinachopimwa ni sample, sasa uwezekano wa udanganyifu kufanywa na suppliers ni mkubwa.
Kuna madawa mengi sana pale yanarudishwa kwa manufacturers. Lakini ikitoke quality control wakashindwa kugundua tatizo, Kinachotakiwa watumiaji wa madawa wakikutana na tatizo ni vizuri kupeleka taarifa MSD au TFDA haraka.
 
Shy,
Lowassa hakuna alipokuwa kaacha kutafuta maslahi, kwa hiyo isikupe shida siku yakifika mahakamani mashahidi watakuwepo. Hata hivyo nimeipost hii article kwa niaba ya contributor mpya, pntimba.
 
KubwaJINGA nashauri ufanye ziara MSD head office kule keko siku moja. Ukiongelea miundo mbinu, MSD ni moja ya idara za serikali zenye high quality of storage facilities. Miundo mbinu ya kuhifadhia dawa imeboreshwa kiasi cha kutosha. Madawa yanatunzwa kwatika joto la aina tofauti kutokana na mahitaji yake.

Point yako haipo clear sana, labda ufafanue kuhusu ufisadi hapo?!!

Green29,
Nashukuru kwa mwaliko. Lakini ningekushauri na wewe ukaangalie yaliyoandikwa ili na wewe utupe picha utakayoina.
 
Mkuu Green29,

Ahsante kwa kuiweka ishu inapotakiwa, yaani kwenye ukweli, JF kweli haijawahi kupungukiwa na vichwa, labda itakuwa fundisho kwa wanaotuvami hapa na kuokota okota ishus bila ya ukweli na kuzitupia tu hapa, zitarekebishwa tu hapa!

Ubarikiwe mkuu Green29, hii ishu originally na ya mtu mwingine labda tumsubiri.
 
Inawezekana Ni Marafiki Tu Na Hawahusiani Chochote Katika Utendaji Wa Shirika Hilo

Mleta Hoja Unaweza Kutueleza Lowassa Anahusika Vipi Katika Uendeshaji Wa Shirika Hilo ? Na Wwewe Ulifanya Jitihada Gani Za Kuhakikisha Taarifa Ulizoleta Ni Ukweli Hazina Chembe Yoyote Ya Uwongo ?

Kama Ni Ukweli Je Utakuwa Tayari Kwenda Kula Kiapo Kusema Ukweli Zaidi Wa Yale Unayoyajua ?

Shy Bwana siku hizi kaibuka na kamtindo ka kujipendekeza kwa wakubwa. Anyway haina haja ya yeye kwenda kula kiapo kwa hilo. kama ni ukweli aujua yeye na alichofanya ni kuweka hapa jamvini ili hizi taarifa zifikie mamlaka husika, kama kuna ukweli basi hatua zaidi zitachukuliwa. Mambo ya kula kiapo nadhani ni out of pint. Watakuja watu wanaoijua MSD vizuri na watatueleza sisi tusiyoifahamu. Shy kama wewe unafahamu ukweli mwingine tupatie mkuu Maro.
 
hii issue ni very serious......................wana JF tusiichukulie kirahisi rahisi..................something physically need to be done and/or established to counter/support the arguments za ndugu yetu pintimbi......

.....kusema MSD kuna watu makini na eti they do their job hakutoshi.....pintimbi katoa data za purchased madawa ziko ndani ya containers.................yes MSD wanweza wakawa na very good facility ya kuhifadhi madawa.....Swali ni je for the quantity mentioned.........are the facilities capable in handling/storing??

.....Duniani sasa ivi kuna suala serious sana la madawa FEKI which is another issue....suala la kufuatilia ni je ni kweli watu wameagiza madawa kw akiwango ambacho hawawezi ku-handle?.......

....kusema eti tusubiri feedback ya wagonjwa kama wanaathirika na madawa yaliyo-expire au yaliyoathirika quality yake au yaliyo feki........tuitasubiri mpaka kiama hapa

....tunahitaji watu wa MSD waje publicly CLEAN na hizi allegations....and not otherwise
 
hii issue ni very serious......................wana JF tusiichukulie kirahisi rahisi..................something physically need to be done and/or established to counter/support the arguments za ndugu yetu pintimbi......

.....kusema MSD kuna watu makini na eti they do their job hakutoshi.....pintimbi katoa data za purchased madawa ziko ndani ya containers.................yes MSD wanweza wakawa na very good facility ya kuhifadhi madawa.....Swali ni je for the quantity mentioned.........are the facilities capable in handling/storing??

.....Duniani sasa ivi kuna suala serious sana la madawa FEKI which is another issue....suala la kufuatilia ni je ni kweli watu wameagiza madawa kw akiwango ambacho hawawezi ku-handle?.......

....kusema eti tusubiri feedback ya wagonjwa kama wanaathirika na madawa yaliyo-expire au yaliyoathirika quality yake au yaliyo feki........tuitasubiri mpaka kiama hapa

....tunahitaji watu wa MSD waje publicly CLEAN na hizi allegations....and not otherwise

Ogah,
Nakubaliana na wewe mkuu. Kama mtu ametumia muda wake kutengeneza article yenye data kibao, hatutakiwi kumpuuza hivi hivi unless mwingine alete convincing data za ku-counter.
 
nafikiri mtoa hoja ana jambo ambalo analifahamu na huu ni mwanzo wa kutupa taarifa hiyo.wanaomshambulia na hoja yake nadhani hawamtendei haki kwa kuwa, kwa kuwa alichofanya ni kutupa habari kama kuna mwenye kupinga alete ushahidi wa kuthibitisha vinginevyo(jamaa ametupa majina ya dawa,batch no etc)
Naomba nikubaliane naye kuwa MSD kuna matatizo makubwa mno, na la hatari linalo endelea sasa ni upungufu mkubwa wa ARVS ulioanza kujitokeza mwezi wa Oktoba 2007.Hii imepelekea wagonjwa kushindwa kuanzishiwa dawa baadhi ya kliniki,na wengine kupewa dawa mbili(duo therapy)tofauti na utaratibu ambapo mgonjwa hupewa dawa tatu(triple therapy.hali hii imewatia hofu CDC(center for disease control) ambao ndio wafadhili wakubwa wa US govt, partners wanaosaidia miradi yote ya utoaji wa ARV nchini,kiasi sasa wameanza kufanya tathini ya dawa nchini ili waweze ku initiate emergency procurement kuziba upungfu huu ambao huenda hali ya kawaida ikarejea mapema May 2008.
 
uoza umezidi mno tanzania. sishangai hata kidogo kusikia mtu ananunua dawa zaidi ya uwezo wa kuzihifadhi, as long as anapata milioni zake 50 anatia mfukoni.
ufisadi upo kila stage na wafanyakazi wa tz wengi wanaufanya.
mtu anaagizia land cruiser hybrid badala ya kulipa milioni 70 zinazotakiwa, inatengenezwa voucher ya milioni 150 watu wanagawana na mkurugenzi. aibu. hatuoneani huruma hata kidogo1
 
Jamani kila ukipita ufisadi jina la Luwasa halikosi, pia ninajiuliza haiwezekani akawa peke yake. Hivi kama Lowassa ni rafiki yake JK, watu wakasema hafai yeye akamteua PM, alisema ni rafiki yake, sasa kweli mambo yote haya JK hausiki? Au ndiyo ile methali ya "nani atamfunga paka kengere"? JK is playing very low but................
 
Wanaharakati wa haki za binadamu wanatetea adhabu ya kunyongwa kwa wahalifu ifutwe.Nashauri ingefutwa baada ya Lowasa kunyongwa.Lowasa hatufai hata kidogo + JK.Kimsingi JK alitakiwa ndio awe wa kwanza kujiuzulu kabla ya ENL lakini woga wa Spika wetu jamani kuanzisha hii move anajua Uspika ndio itakua basi.

Kiasi cha sh.milioni 152kwa siku ni kiasi kikubwa ambacho eti JK alikua hajui hili mimi silikubali hata kidogo.JK hawezi kujinasua ktk hili.Aombe kung'atuka mapema kabla mambo hayajaharibika na kama anadhani hapa JF tunacheza basi aendelee na huo urais lakini asije kutuchukua wana JF kwamba tulisema.
LOWASA NA KIKWETE WANASTAILI KUPEWA ADHABU YA KUNYONGWA HADHARANI HADI WAFE kwa kuliingizia taifa hasara ya mabilioni na kuwabebesha wananchi mzigo ambao sio wakwao.

Hizo sh.152 milioni kwa siku hadi kufikia leo hii nadhani barabara yenye urefu wa km hata 100 zingewekwa lami lakini zinaishia ktk matumbo ya watu wenye tamaa kama L na JM.

JK kuweni makini na maneno haya tunayosema kwamba ipo siku bubu atasema na viziwi watasikia msije mkadhani ni kelele za chura,wana JF tumedhamiria.

MWAKYEMBE HEBU CHUKUA FORM ZA URIS 2010,JK anatuwekea usiku hapa.
 
Jamani kila ukipita ufisadi jina la Luwasa halikosi, pia ninajiuliza haiwezekani akawa peke yake. Hivi kama Lowassa ni rafiki yake JK, watu wakasema hafai yeye akamteua PM, alisema ni rafiki yake, sasa kweli mambo yote haya JK hausiki? Au ndiyo ile methali ya "nani atamfunga paka kengere"? JK is playing very low but................

Mkuu Jafar,
Huyu jamaa ana historia ndefu ya ufisadi tokea alipokuwa bwana mdogo pale AICC na ana kawaida ya kuwafanya wengine (asioshirikiana nao au wanaompinga), kuonekana wabaya au hata kuwafukuza kazi, ndio maana mambo yake yanaliki kirahisi, japokua pia maufisadi yake yako mengi kuzidi rafikize.
 
KubwaJINGA nashauri ufanye ziara MSD head office kule keko siku moja. Ukiongelea miundo mbinu, MSD ni moja ya idara za serikali zenye high quality of storage facilities. Miundo mbinu ya kuhifadhia dawa imeboreshwa kiasi cha kutosha. Madawa yanatunzwa kwatika joto la aina tofauti kutokana na mahitaji yake.

1.Hapa point sio quality ya storage,nilivyoelewa mimi tatizo si quality tatizo ni capacity.

2.Pili suala jingine liloongelewa kuonyesha harufu ya ufisadi ni kuagizwa dawa nyingi kuliko uwezo wa kuzihifadhi,hili haliwezi kutokea katika hali ya kawaida sababu hao wanaosimamia uagizaji wanajua capacity yao ya kuzitunza

3.Kuhusu wataalamu ni kweli wapo,naamini hivyo lakini kwa tanzania tatizo si utaalam,tatizo ni ufisadi.Sehemu zote ambako kumetokea ufisadi kuna wataalam wa kutosha.

Mwisho natoa rai kuwa hili linahitaji kufuatiliwa zaidi kuthibitisha pasi shaka,ila kwa sasa kulingana na matukio kadhaa yaliyopita na yanayoendelea hapa Tz nazichukulia taarifa hizi kuwa ni kweli hadi hapo nitakapothibitisha vinginevyo.
 
kwa Tanzania ilipokuwa ilipokuwa imefikia hata sishangai kusikia haya.
muhimu tuu tuache ushabiki wa mambo haya yanaosadikiwa kuhatarisha maisha ya wengi. uchunguzi ufanyike kuanzia hukohuko MSD na wahusika ikibainika wajitathmini kabla hata ngosha Magu hajalisikia. "usithubutu kukutwa na Magufuli"
 
Pamoja na hayo yote madhara yapo hadi hivi leo.
Swali la kujiuliza hivi hicho kitengo cha ukaguzi wa ndani kazi yake nini, ni vyema wangewajibika, kwani baadhi ya hizo dawa zimekwisha expire na uongozi wa sasa unazitetea kwa nguvu zote.
 
Inawezekana Ni Marafiki Tu Na Hawahusiani Chochote Katika Utendaji Wa Shirika Hilo

Mleta Hoja Unaweza Kutueleza Lowassa Anahusika Vipi Katika Uendeshaji Wa Shirika Hilo ? Na Wwewe Ulifanya Jitihada Gani Za Kuhakikisha Taarifa Ulizoleta Ni Ukweli Hazina Chembe Yoyote Ya Uwongo ?

Kama Ni Ukweli Je Utakuwa Tayari Kwenda Kula Kiapo Kusema Ukweli Zaidi Wa Yale Unayoyajua ?

Mleta mada ni marehemu maana kwa binadamu hai hawezi kuwa mfitini na juha kama huyu lazima yuko kuzimu huyu
 
Back
Top Bottom