Lowassa - "Nguvu Kuu" nyuma ya mabadiliko?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Baada ya kutulia chini na kuangalia mabadiliko yaliyofanyika najikuta sina jinsi isipokuwa kuamini ya kuwa kuna uwezekano mkubwa kwamba Lowassa ndiye nguvu kuu ya mabadiliko ya mawaziri, kiasi cha kuhakikisha walioupande wake wanarudi na waliokuwa ni watu wa karibu wanapata uwaziri kamili.

William Ngeleja (nasikia huyu familia zao zina uhusiano wa kindoa.. sijajua)
Lawrence Masha, Chenge na Msolla - wote wana connection na Lowassa

Watu aliogongana nao vichwa kama Diallo na Meghji wamewekwa pembeni.

Naomba tuangalie kidogo Mawaziri waliorudishwa na uhusiano wao na Lowassa.
 
Baada ya kutulia chini na kuangalia mabadiliko yaliyofanyika najikuta sina jinsi isipokuwa kuamini ya kuwa kuna uwezekano mkubwa kwamba Lowassa ndiye nguvu kuu ya mabadiliko ya mawaziri, kiasi cha kuhakikisha walioupande wake wanarudi na waliokuwa ni watu wa karibu wanapata uwaziri kamili.

William Ngeleja (nasikia huyu familia zao zina uhusiano wa kindoa.. sijajua)
Lawrence Masha, Chenge na Msolla - wote wana connection na Lowassa

Watu aliogongana nao vichwa kama Diallo na Meghji wamewekwa pembeni.

Naomba tuangalie kidogo Mawaziri waliorudishwa na uhusiano wao na Lowassa.

Mkuu Mwanakijiji unataka kutuambia kuwa Lowassa kabaki? Wantisha mzee, mbona Kubenea nae kaibuka "kiupya" na "Mwanahalisi" yake!
 
Baada ya kutulia chini na kuangalia mabadiliko yaliyofanyika najikuta sina jinsi isipokuwa kuamini ya kuwa kuna uwezekano mkubwa kwamba Lowassa ndiye nguvu kuu ya mabadiliko ya mawaziri, kiasi cha kuhakikisha walioupande wake wanarudi na waliokuwa ni watu wa karibu wanapata uwaziri kamili.

William Ngeleja (nasikia huyu familia zao zina uhusiano wa kindoa.. sijajua)
Lawrence Masha, Chenge na Msolla - wote wana connection na Lowassa

Watu aliogongana nao vichwa kama Diallo na Meghji wamewekwa pembeni.

Naomba tuangalie kidogo Mawaziri waliorudishwa na uhusiano wao na Lowassa.

Kwa mtindo utaratibu huo na kwa mujibu wa "jf sources" Membe asinge rudishwa kwani kwa mujibu wa GT ni miongoni mwa "waliogongana vichwa"
 
Niliona mtu mmoja humu JF akimpigia Debe Masha...au ndio hapa JF baadhi ya wapambe wanatumwa kuja kuwauza jamaa zao?
I can Believe na hio kuwa Lowassa ni nguvu kuu ndo maana JK leo amekuwa akisema kuondoka kwa lowassa ni pigo.

Sikubaliani kuwa Muungwana anamlamba kisogo EL, walichofanya ktk Baraza ni kupunguza kelele tu...i dont see serious waziri alie na uchungu na nchi hii.
NImecheka leo asb wakati Mh. Mungai anaulizwa na BBC kuhusu kuachwa ktk Baraza la Mawazir, anasema sasa inabidi apumzike aendeshe biashara zake..kwanini alisubiri baraza kuvunjwa?

Mwanakjj kama kuna sources muhim lete...hapa tuwakome nyani 24X7
 
Nilikuwa nazungumza na mtu nyumbani aliyekuwa karibu wakati wa hotuba ya Rais Diamond Jubilee.. na nikamuuliza aliichukuliaje hotuba hiyo? Kama ilikuwa ni ya kumtetea Lowassa au ya kuonesha kuwa haki imetendeka? Na hasa kujua ule ucheleweshaji wa siku moja wa kutangaza baraza la Mawaziri ulikuwaje?

Kwa sababu Rais anasema alikuwa alifanyie baraza marekebisho baada ya mkutano huu wa Bunge lakini matukio ya Mwakyembe yamemuwahisha, sasa ilikuwa amuondoe na Lowassa pia? Nadhani bila ripoti ya Mwakyembe ingekuwa ni more dramatic kwa yeye kumuacha Lowassa kwenye Baraza jipya.

Sasa kulikuwa na conditions gani za kujiuzulu kwa Lowassa? Mwanzoni implication ilikuwa Lowassa aliamua kuweka manyanga chini. Kwa wale wanaokumbuka usiku wa Jumanne iliyopita ambapo ilidaiwa Lowassa hakuwa tayari kujiuzulu kwa vile "hajafanya kosa lolote" lazima kulikuwa na sababu kubwa ya kuweza kumshawishi kujiuzulu, vinginevyo Rais angeamua kuvunja Baraza tu na kufanya vile vile, kwanini Lowassa alijiuzulu badala ya Rais kufanya tu mabadiliko?

Katika kujumlisha moja na moja ndipo kwa mbali kama kwenye ukungu tunaweza kuona kuwa Lowassa kaondoka kwa nguvu ya Chama. Rais pia ameashiria kuwa kama ungekuwa ni uamuzi wake labda Lowassa asingetoka lakini "Kamati Kuu na wabunge wa CCM" walitaka awajibishwe na yeye "hakuweza kuwazuia".

Sasa tunajiuliza ni lini Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania akashindwa nguvu ya kushughulika ndani ya chama chake ukizingatia nguvu yake kichama bado ni kubwa mno? Tunaokumbuka historia tunakumbuka kile kilichojulikana kama "mizengwe" kule Dodoma ambayo ilitokea wakati wa Nyerere, na bila ya shaka kurudiwa kwa namna tofauti na Mwinyi na Mkapa. Je Kikwete alishindwa kufanya "mizengwe".

Kama kweli Rais Kikwete hakuweza kuzuia maporomoko ya maji ya wabunge wa CCM kiasi cha "kuzidiwa nguvu" na kulazimishwa kumuwajibisha Lowassa, hatuna kitu kingine cha kusema kuwa aidha kuna mambo makubwa mawili yanayotokea mbele ya macho yetu. Kwanza yawezekana kwa mara ya kwanza ndani ya CCM wabunge wa CCM wamejitutumia kiasi cha kumuweka Mwenyekiti wao kwenye Mizani na kumzidi uzito na hivyo kumlazimisha kutii matakwa yao. Vinginevyo, demokrasia siyo tu inazidi kukomaa ndani ya chama bali bado inathibitisha maneno ya kinabii ya Mwalimu kuwa "upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM". Je yawezekana kuwa huu ni mfano mdogo tu wa upinzani huo?

Kama wabunge wamepewa Lowassa kama walivyotaka, Rais amepewa nini toka kwa wabunge? Bila ya shaka suala la Benki Kuu lawezekana kuwa ndio itakuwa ndio ofa aliyopewa. Je Bunge litaunda Kamati Teule kuchunguza BoT? Yawezekana lakini kwa hakika Mwakyembe hatapewa nafasi hiyo!! Somo walilolipata ni ambalo watajuta kukaa darasani.

Kwa kadiri siku zinavyokwenda ndivyo tutakavyojifunza mengi zaidi na mengi zaidi yatazidi kujitokeza.

Swali la kufikiria: Itakuwaje endapo Lowassa akaamua kujivua uanachama kabla Kamati Kuu haijaamua kumchukulia hatua za kisheria na hivyo kupoteza kiti chake cha Ubunge?
 
Hivi ni kweli Kampuni ya RICHMOND NI KAMPUNI HEWA? na kuna fununu kuwa kampuni hii ni yake mwenyewe EL ndio maana akamuandikisha mwanawe aitwae RICHARD na kutumia jimbo analowakilisha Bungeni yaani MONDULI! na kutolea jina la RICH-MOND= RICHARD& MONDULI!!!
 
Kwa mtindo utaratibu huo na kwa mujibu wa "jf sources" Membe asinge rudishwa kwani kwa mujibu wa GT ni miongoni mwa "waliogongana vichwa"

Mwanakijiji,
I think you have a point. Mimi nilijua Membe atarudi. Huyu ni rafiki mkubwa sana wa Kikwete. Lakini kuna kitu ambacho tunapuuza hapa. In politics there are no permanent friends. Ilifikia wakati JK alianza kumwogopa EL. Alishauriwa kuwa huyu alikuwa anafanya njama za kichinichini kumwangusha in 2010. Nasikia na yeye (EL) alitaja waziwazi kuwa he was ready to go for the big post come 2010. Wewe ungekuwa Ikulu ungefanya nini? JK alikuwa na kila uwezo wa kunyamazisha ripoti ya Mwakyembe kama alivyofanya ripoti ya BOT au kama Mkapa alivyoweka kabatini ripoti ya Warioba. But he refused to do that and he refused to meet with EL. There is more to come.
 
..
William Ngeleja (nasikia huyu familia zao zina uhusiano wa kindoa.. sijajua)
Lawrence Masha, Chenge na Msolla - wote wana connection na Lowassa

Watu aliogongana nao vichwa kama Diallo na Meghji wamewekwa pembeni.

Naomba tuangalie kidogo Mawaziri waliorudishwa na uhusiano wao na Lowassa.

...Mwanakijiji hivi una maana gani unaposema kuwa hawa jamaa wana uhusiano na lowasa??? Hawa jamaa wote wamefanya kazi na lowassa, sasa ulitegemea wasiwe na mahusiano kweli??? Au ni mahusiano gani unayotaka kuongelea??? Mahusiano yanaweza kuwa ni ya ki-bailojia, kikazi, kibiashara, etc. yote ni mahusiano. Inategemea unazungumzia mahusiano yepi na katika hadhira ipi!!.
 
Mwanakijiji,
I think you have a point. Mimi nilijua Membe atarudi. Huyu ni rafiki mkubwa sana wa Kikwete. Lakini kuna kitu ambacho tunapuuza hapa. In politics there are no permanent friends. Ilifikia wakati JK alianza kumwogopa EL. Alishauriwa kuwa huyu alikuwa anafanya njama za kichinichini kumwangusha in 2010. Nasikia na yeye (EL) alitaja waziwazi kuwa he was ready to go for the big post come 2010. Wewe ungekuwa Ikulu ungefanya nini? JK alikuwa na kila uwezo wa kunyamazisha ripoti ya Mwakyembe kama alivyofanya ripoti ya BOT au kama Mkapa alivyoweka kabatini ripoti ya Warioba. But he refused to do that and he refused to meet with EL. There is more to come.

Jasusi, JK asingeweza kumuondoa Membe sasa hivi wala kumpangia wizara nyingine. Ziara ya Rais Bush siku chache zijazo inahitaji coordination ya hali ya juu sana hivyo kumuondoa miamba masaa machache siyo tu ingeleta usumbufu usio wa lazima ingewapa wakati mgumu watu wa Marekani kuelewa mambo yanayoendelea tanzania hasa wakilazimika kuanza kumbrief mtu mwingine.

kwa upande wa Chenge nadhani sababu kubwa ya yeye kubakia ni mambo yanayoendelea ATC na hasa ujio wa dege kubwa la Airbus (ile mbovu na hiyo mpya). Kama mnavyofahamu Rais wa Zanzibar anaanza ziara ya Ujerumaini na atatembelea (unless wabadili) jiji la Hamburg ambapo tuna order moja ya ndege aina ya Airbus. Hata hivyo matukio ya wiki hizi mbili vimesababisha JK asitishe ziara hiyo na kumpa Karume ili yeye aendelee na mambo ya serikali na ujio wa Bush.

Hivyo binafsi sitashangaa kuwa baadhi ya mabadiliko makubwa yanakuja baada ya ziara ya Bush.
 
Kwa taarifa yenu baraza la mawaziri huchaguliwa na CC ya chama.... hapo kila mtu ana kipenzi ama mtu wake wa kazi.. Mkapa, Mwinyi, Rashid Kawawa, KIngunge wote hawa wana watu wao ndani ya serikali hii..kama zilivyo serikali zote zilizopitia Ujamaa..

Kwa hiyo basi mkae mkijua kuwa serikali ya Tanzania ni CCM, maslahi ya CCM mbele ya maslahi ya Taifa.. na kinachotangulia yote ni maslahi ya vigogo wa CCM....

Kidumu chama cha Mapinduzi (Revolution party) na zidumu fikra za mwenyekiti Mao tse Tung!
 
JK amekuwa na wakati mgumu kutokana na ukweli kwamba hali ya Tanzania kisiasa inabadilika. Hawa akina EL, Mramba, Karamagi et al ni wezi wakubwa wa mali ya walalahoi ambao wamekuwa wanalipa kodi kila siku. Ni wahujumu wa uchumi, JK anatafuta jinsi ya kuweza kurudisha imani ya wananchi kwa CCM. Matukio ya Kenya yamewashitua sana kwa hiyo mkakati wao ni kuona wanaendelea kubaki madarakani 2010.

Na wanafahamu wakifanya mchezo wapiga kura watawatema kwa hiyo wanajaribu kupooza mambo; lakini Je, wataweza kurudisha mali walizowauzia wageni kwa bei ya peremende? Wanaweza kuwatosa MAFISADI wote ndani ya CCM?
 
Niliona mtu mmoja humu JF akimpigia Debe Masha...au ndio hapa JF baadhi ya wapambe wanatumwa kuja kuwauza jamaa zao?
I can Believe na hio kuwa Lowassa ni nguvu kuu ndo maana JK leo amekuwa akisema kuondoka kwa lowassa ni pigo.

Sikubaliani kuwa Muungwana anamlamba kisogo EL, walichofanya ktk Baraza ni kupunguza kelele tu...i dont see serious waziri alie na uchungu na nchi hii.
NImecheka leo asb wakati Mh. Mungai anaulizwa na BBC kuhusu kuachwa ktk Baraza la Mawazir, anasema sasa inabidi apumzike aendeshe biashara zake..kwanini alisubiri baraza kuvunjwa?

Mwanakjj kama kuna sources muhim lete...hapa tuwakome nyani 24X7

Biashara ? Ipi?
Hana Biashara yeyote ile labda aende kuwa HM wa ile shule ya English Media.

Walikuwa wakifungua biashara hewa kuendelea kuiba fedha za serikali sasa muda umefika waende wakawe wakurugenzi wa Hewa.

Mbona mwanae karudi last year toka hapa USA akiwa na MBA hakwenda endesha hiyo biashara ya baba yake?

Kaenda kufanya kufanya kazi kwa wahindi vikamshinda,sasa naye kaunga list ndefu ya watoto wa waheshimiwa kufanya kazi BOT.

Anachekesha kweli.
 
Jasusi, JK asingeweza kumuondoa Membe sasa hivi wala kumpangia wizara nyingine. Ziara ya Rais Bush siku chache zijazo inahitaji coordination ya hali ya juu sana hivyo kumuondoa miamba masaa machache siyo tu ingeleta usumbufu usio wa lazima ingewapa wakati mgumu watu wa Marekani kuelewa mambo yanayoendelea tanzania hasa wakilazimika kuanza kumbrief mtu mwingine.

kwa upande wa Chenge nadhani sababu kubwa ya yeye kubakia ni mambo yanayoendelea ATC na hasa ujio wa dege kubwa la Airbus (ile mbovu na hiyo mpya). Kama mnavyofahamu Rais wa Zanzibar anaanza ziara ya Ujerumaini na atatembelea (unless wabadili) jiji la Hamburg ambapo tuna order moja ya ndege aina ya Airbus. Hata hivyo matukio ya wiki hizi mbili vimesababisha JK asitishe ziara hiyo na kumpa Karume ili yeye aendelee na mambo ya serikali na ujio wa Bush.

Hivyo binafsi sitashangaa kuwa baadhi ya mabadiliko makubwa yanakuja baada ya ziara ya Bush.

mwana jiji

una mawazo kama yangu,nimekuwa nahisia kuwa muungwana atafanya mabadiliko ndani ya serikali yake mara tu baada ya mzeee kichaka kuondoka,hivi unaona hayo mabadiliko yatahusisha watu kutoka nje ya baraza au ni ya humo humo ndani?
 
Niliona mtu mmoja humu JF akimpigia Debe Masha...au ndio hapa JF baadhi ya wapambe wanatumwa kuja kuwauza jamaa zao?

Mkuu chuma mbona na wewe umetuambia jinsi Msabaha alivyo kichwa, sasa ina maana umetumwa naye kuja kumpigia debe?

I know Masha, so far ameonyesha uwezo mkubwa wa kazi na sio mwizi maana ripoti nzima ya Richimonduli hakutajwa hata mara moja, pmaoja na kwamba yeye ndiye aliyekuwa waziri mdogo wa Msabaha, mpaka katibu ametajwa kuwahusika lakini sio waziri mdogo,

kuna kumpigia debe mtu na kusema ukweli, huwezi kumpigia debe kiongozi ambaye ni waziri tayari, unampigia debe Msabaha, aliyejipumzisha, Masha ni mfano wa kuigwa na hasa ukitilia maanani umri wake, ambao ni mdogo sana kwake kuweza kufanya anyoyafanya as far as uongozi is concerned.

Masha ni mfano wa kuigwa kwetu wote kijana mdogo, msomi, ex-wakili wa binafsi, tena very successful, sasa na uwaziri ndio hivyo anazidi kuonyesha kipaji alichopewa na Mwenyezi Mungu, mtoto mdogo amweza kuishinda tamaa, watu wazima kina lowassa, Msabaha, Karamagi wameshindwa, mkuu toa pongezi kwa kijana maana anatuwakilisha wote wale wenye uchungu na nchi.

Ahsante Mkuu Chuma.
 
Kwa taarifa yenu baraza la mawaziri huchaguliwa na CC ya chama.... hapo kila mtu ana kipenzi ama mtu wake wa kazi.. Mkapa, Mwinyi, Rashid Kawawa, KIngunge wote hawa wana watu wao ndani ya serikali hii..kama zilivyo serikali zote zilizopitia Ujamaa..

Kwa hiyo basi mkae mkijua kuwa serikali ya Tanzania ni CCM, maslahi ya CCM mbele ya maslahi ya Taifa.. na kinachotangulia yote ni maslahi ya vigogo wa CCM....

Kidumu chama cha Mapinduzi (Revolution party) na zidumu fikra za mwenyekiti Mao tse Tung!

Mkuu huenda maoni yako yakawa ni kweli lakini naamini kabisa kuwa BWM hana mkono ktk baraza la mawaziri la JK this time,walioshiriki unawaona hata ktk hadhara za chama sasa na hata wanapoongea they do sound serikali.Alichofanya JK ni kurejea ushauri wake 2005 kuhusu PM,yuko Kenya anapigwa baridi na harufu za damu za wakikuyu na waruo.No sign of him ndani ya Tanganyika,hili ni kundi lake JK linaloongozwa na mtoto wa Mkulima
 
William Ngeleja (nasikia huyu familia zao zina uhusiano wa kindoa.. sijajua)

Mheshimiwa William Mganga Ngeleja(MB) ni nani?
Niseme wazi kwamba namfahamu Mheshimiwa Ngeleja kwa Takribani Miaka 25 hivi,Ni Mzaliwa Wa Bitoto Sengerema na Ana Shahada Ya Sheria kutuoka Chuo kikuu cha Dar es salaam,pia an Stashahada hiyo hiyo kutoka chuo hicho cha Mlimani.Ameoa na Ana Mtoto mmoja tu.Mkewe ni Mtu wa Ukerewe na anafanya Kazi katika Benki moja jijini Dar es salaam,na hana uhusiano wowote wa kindoa kati yake na Mheshimiwa Lowassa.

Kuhusu Mheshimiwa Ngeleja kufahamiana na Lowassa,yawezekana wanafahamiana kikazi tu wakati Mhemiwa Ngeleja akiwa Mwanasheria Wa Vodacom,kama ujuavyo Alphatel ni mmoja wa Mawakala wa Vodacom na kutokana kna kazi aliyokuwa nayo Mhe. Ngeleja ya Mwanasheria wa Vodacom(yaani Regulatory and Legal Manager) ni rahisi kufahamiana na Bwana Lowassa kwasababu ya kupitia Mikataba yote ya Kampuni ya vodacom ambayo ilikuwa ikiingiwa na kampuni zingine.

uhusiano uliopo ni ule Naibu Waziri na Waziri Mkuu,na ikumbukwe Ngeleja alianaza kuwa Naibu waziri wa Nishati wakati suala la RDC lilishafanyika,aliingia sababu ya utendaji kazi wake,ni watu wa style ya Mheshimiwa Waziri Mkuu Mpya Mizengo Pinda.aliachwa tu 2005 ila ni watu waliotakiwa kuwmo katika Baraz ala Mawaziri toka Mwaka huo.

Uadilifu Mheshimiwa William Ngeleja(WAZIRI)
Mhemiwa Ngeleja ni Mwadilifu,mchapa kazi na Mpole anayechukia Rushwa,na hata ukiuliza wafanyakazi walioko pale Waizara ya Madini watakueleza jinsi ya utendaji wake,amekuwa akifanya kazi mpaka Siku za Jumapili ili kuhakikisha shughuli zinaenda vizuri.na hata kama uakumbuka wakati dr. Mwakyembe anafunga semina ambayo wabunge walikataa mswaada wa Madini alisema,"naomba nimuite Naibu waziri aje afunge Mkutano huu,wabunge wakasema hapana..akawajibu hata huu ambaye mlikuwa naye kipindi chote mkiwasiliana vizuri".ina maanisha Dr. Mwakyembe alimwaamini Mhe. Ngeleja ni Mwadilifu.Hata kamati ya Mwakyembe haikuonesha kwamba yeye ni mtu Fisadi.

Ripoti ya Mwakyembe haikumhusiha na suala la RDC kwenda Dowans,hii inaonesha kwamba yeye si mmoja wa waliliingiza taifa katika matatizo ya kupand akwa Umeme.

Utendaji kazi wa Mheshimiwa Ngeleja(Mbunge)
Mheshimiwa Ngeleja amekuwa akitoa misaada mbalimbali katika Jimbo lake,na imefikia hata kuacha familia yake kuwatumikia wananchi wake.Mfano wakati wa sikukuu ya Krismasi nna Mwaka Mpya alikuwa jimboni kwake akitatua matatatizo ya wanajimbo lake na akiacha familia yake.hii inaonesha anavyojali matatizo ya wananchi wake.Ameweza kuhakikisha kivuko cha kigongo feri ambacho kimekuwa kero kwa muda wa miaka 15 kinaleta na kufungwa,na hivi karibuni kitafunguliwa na Mhe. Rais,amweza kuhakisha anasomesha wanafunzi wasiojiweza kuendelea na Elimu ya juu hasa sekondari natayari kuna mfuko wa kuendeleza suala hilo unaosimamiwa na wananchi wenyewe.


Hitimisho
Aliyekupa habari hizo,kwa namna moja ama nyingine ana lengo la kumchafua Mheshimiwa Ngeleja kisisasa,na wameamua kukutumia Mzee Mwanakijiji kwasababu wamejua una sauti mbele ya watanzania na si jambo zuri kuchafua Wanasiasa vijana wa Umri wetu amabo wana lengo la kuondoa kero na matatizo ya wananchi wake,Mhe. Ngeleja ni mwanasheria na nina uhakika atashughulikia kwa makini suala linalohusika mikataba mibovu ambayo serikali imeingia kipindi cha nyuma.na hana uhusiano wa kifamilia na Mhe. Edward Lowassa.Nataka kusema Hivi Mheshimiwa Ngeleja hana Mahusiano yoyote na Lowassa zaidi ya Mahusiano ya kikazi tu.!

"Kama tukianza kuchafuana ,sidhani kama kuna mwanasiasa yoyote ambaye anayeweza kubaki.."Lowassa

Naomba kutoa hoja.
 
Mwanakijiji,wakati mwingine hisia hujenga mambo fulani yakafanyiwa uchunguzi na yakawa ya kweli. kuondoka kwa Lowassa sio kwamba mizizi yake nayo imeondoka hata JK jana alituambia ilikuwa vigumu kumuondoa ila ilikuwa hana jinsi. Hivyo mie sishangai huyu jamaa akiwa anaendesha mambo yake japo hayupo tena serikalini tena
 
Back
Top Bottom