SDP_TZ_Mpya
Senior Member
- Jun 21, 2013
- 166
- 77
Wakati wa uchaguzi mkuu wa CCM ngazi ya taifa mwezi Oktoba 2012, Lowassa alikuja na mkakati ambao baadhi ya wana-CCM waliukubali. Hoja ilikuwa zitenganishwe kofia ya uenyekiti wa chama taifa na Urais ili kuimarisha uwajibikaji. Kambi ya Kikwete ilimtumia vizuri mzee Yusuph Makamba kuzima 'uasi' huo hasa siku ya uchaguzi huku wazee wakitumika kumpoza Lowassa kuwa amwachie tu rafiki yake amalize salama. Hivyo mambo yakapita kwa Kikwete kupata 99% (kura 2 zilisema hapana) huku Shein na Mangula wakizoa zote. Ikumbukwe pia ni marufuku CCM kumpinga Mwenyekiti aliyeko madarakani ambaye anataka kuendelea. Pia, ni marufuku kumpinga Rais aliyeko madarakani huku bado na tamaa ya kuendelea na mhula wa pili.
Katika kesi zote mbili za uenyekiti na Urais CCM husema "fomu iko moja tu na imeshachukuliwa" - Nape.
Kwa upande wa Zitto, nae anadai Mbowe ni dhaifu sana kiuongozi na ni haki yake kugombea. Licha ya waraka kukiri kuwa Mbowe na Slaa wameingia madarakani kukiwa na wabunge 5 tu wa CHADEMA na sasa wako 49 yaani wameongeza wabunge kwa asilimia karibu 1,000% na madiwani lukuki huku kura za Urais wakifikia mamilioni.
Bila kujali ukongwe wa chama na Mazingira yanayokizunguka CDM, Zitto anaona bado haki yake ni bora hata km CDM italipa gharama kubwa kutokana na ukweli kuwa CCM inaiwinda CDM usiku na mchana.
Vyama vyote vikiwemo CCM na CDM (ingawa viko kwenye hatua tofauti sana ya uhai) vina mahitaji ya ndani yanayovifanya viwe makini kwenye kubadilisha uongozi. Sikushangaa kufa kwa "mkakati wa kofia mbili" CCM na km vile Zitto, Mwigamba na Kitila wanavyodhihirika kukihujumu chama chao cha CDM kupitia "mkakati wa ushindi 2013". Hata hivyo, CDM iko kwenye uchanga zaidi wakati CCM iko kwenye kujifufua, hali inayovifanya vyama hivi kuwa makini na kila uamuzi unaohusisha badiliko la uongozi.
Kama ambavyo Lowassa alistahili kufukuzwa CCM, CDM wamepata fursa ya kum-offload Zitto na washirika wake. Madhara ya kuunda vikundi mkakati ndani ya Chama ndiyo yatakayoleta mpasuko na kukiua CCM 2015 hasa wakati na baada ya uteuzi wa mgombea Urais. CCM wamechelewa ila CDM muwahi haraka kwani Zitto anaonekana kuyaficha mengi na tayari mtandao wao walishaujenga kila alipoenda kwenye za peke yake (km anavyokiri kufanya) na unafanya kazi.
Katika kesi zote mbili za uenyekiti na Urais CCM husema "fomu iko moja tu na imeshachukuliwa" - Nape.
Kwa upande wa Zitto, nae anadai Mbowe ni dhaifu sana kiuongozi na ni haki yake kugombea. Licha ya waraka kukiri kuwa Mbowe na Slaa wameingia madarakani kukiwa na wabunge 5 tu wa CHADEMA na sasa wako 49 yaani wameongeza wabunge kwa asilimia karibu 1,000% na madiwani lukuki huku kura za Urais wakifikia mamilioni.
Bila kujali ukongwe wa chama na Mazingira yanayokizunguka CDM, Zitto anaona bado haki yake ni bora hata km CDM italipa gharama kubwa kutokana na ukweli kuwa CCM inaiwinda CDM usiku na mchana.
Vyama vyote vikiwemo CCM na CDM (ingawa viko kwenye hatua tofauti sana ya uhai) vina mahitaji ya ndani yanayovifanya viwe makini kwenye kubadilisha uongozi. Sikushangaa kufa kwa "mkakati wa kofia mbili" CCM na km vile Zitto, Mwigamba na Kitila wanavyodhihirika kukihujumu chama chao cha CDM kupitia "mkakati wa ushindi 2013". Hata hivyo, CDM iko kwenye uchanga zaidi wakati CCM iko kwenye kujifufua, hali inayovifanya vyama hivi kuwa makini na kila uamuzi unaohusisha badiliko la uongozi.
Kama ambavyo Lowassa alistahili kufukuzwa CCM, CDM wamepata fursa ya kum-offload Zitto na washirika wake. Madhara ya kuunda vikundi mkakati ndani ya Chama ndiyo yatakayoleta mpasuko na kukiua CCM 2015 hasa wakati na baada ya uteuzi wa mgombea Urais. CCM wamechelewa ila CDM muwahi haraka kwani Zitto anaonekana kuyaficha mengi na tayari mtandao wao walishaujenga kila alipoenda kwenye za peke yake (km anavyokiri kufanya) na unafanya kazi.