Lowassa matatani zaidi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Lowassa matatani zaidi

Waandishi Wetu Februari 27, 2008
Raia Mwema

Spika aagiza kanda za matamshi yake zitafutwe, zichunguzwe
SAKATA ya kampuni hewa ya kufufua umeme ya Richmond bado inachemka na sasa kuna uwezekano mkubwa wa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na madini, Nazir Karamagi kubanwa na Bunge kwa matamshi yao.

Raia Mwema imethibitishiwa kwamba matamshi mengine ambayo yanalianika Bunge vibaya ni ya Waziri wa Sheria, Mathias Chikawe, ambaye ameelezwa kuwa alimtetea Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika aliyetajwa kuhusika katika sakata hiyo ya Richmond.

Chimbuko la hatua hiyo ya Bunge linatokana na hatua ya Lowassa kueleza, katika vyombo vya habari na katika mkutano wake jimboni kwake Monduli, Jumamosi wiki iliyopita, kwamba hakuhusika katika mkataba wa Richmond na kwamba alilazimika kujiuzulu kwa sababu ya uwajibikaji wa pamoja yeye kama mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali.

Kwa upande wake, Karamagi amekuwa akisema kwamba yeye alipohamia Wizara ya Nishati, mkataba na Richmond ulikuwa umekwisha kukamilika na kwa ajili hiyo kueleza kwamba anahusika ni suala ambalo atalipinga kwa nguvu zake zote.

Spika wa Bunge, Samuel Sitta aliliambia Raia Mwema mwanzoni mwa wiki kwamba hakuwa amepata kwa undani kuhusu matamshi ya Lowassa, Karamagi na Chikawe na hivyo asingweza kwa hakika kusema ni hatua gani inaweza kuchukuliwa dhidi yao.

Lakini alieleza, katika mahojiano ya simu kutoka jimboni kwake Urambo kwamba kwa hakika Bunge litachunguza matamshi hayo kama hayaliondolei Bunge hadhi.

Alisema kwamba yeye pia amepewa taarifa hizo na watu mbali mbali, akiwa jimboni kwake Urambo, Tabora, na kwamba hawezi kutoa tamko kwa kuwa hana ushahidi kamili wa kuona wala kusikia yeye mwenyewe.

Alisema kwamba kutokana na kukosa ushahidi huo, ameagiza wasaidizi wake watafute vielelezo vya matamshi au maandiko yanayotolewa na Lowassa na watu wengine kuhusu Kamati Teule ya Bunge iliyoichunguza Richmond.

Raia Mwema imedokezwa kwamba kuna uwezekano mkubwa watu hao wakahojiwa katika kikao kijacho cha Bunge, kutokana na kukinzana na Azimio la Bunge kuhusu Ripoti ya Kamati Teule ya Bunge.

"Kwa mfano Lowassa alikuwa na fursa ya kupewa muda mwingi wa kujieleza bungeni kama kiongozi wa shughuli za Bunge. Alitakiwa ayaseme haya anayoyasema sasa, ndani ya Bunge. Sasa kuyasema nje kutamletea matatizo", anasema mwanasheria mmoja maarufu jijini ambaye pia ni mbunge.

Anaongeza: "Bunge limetoa Azimio. Ripoti ya Kamati Teule imepitishwa na Bunge. Suala lililobaki hivi sasa ni utekelezaji tu. Kujadili hilo nje ya Bunge ni contempt of Parliament (kuingilia shughuli za Bunge), Raia Mwema ilielezwa.

Kuhusu suala la Waziri Mkuu Lowassa kuhojiwa na Kamati ya Bunge, Raia Mwema iliambiwa kuwa nafasi ya Waziri Mkuu inapatikana kutokana na mwafaka unaopatikana kati ya pande mbili, yaani Rais na Bunge.

"Rais anapendekeza jina, Bunge linapitisha. Kwa hiyo, Bunge lingeamua kumhoji na kumwadhibu, basi, nafasi ya pili ya Rais inaweza kuingia kwenye chuki na Bunge, na hapa kunaweza kuwa na msuguano," alisema mwanasheria huyo.

Kamati teule inaundwa na chombo kimoja-Bunge. Angeitwa Lowassa, akahojiwa na kukutwa na hatia, angeadhibiwa, asipate hata mafao. Kutokana na hilo, Rais akikasirika inabidi avunje Bunge, kwa kuwa Waziri Mkuu ni sehemu ya uteuzi wake, Raia Mwema lilielezwa.

Wataalam wa masuala ya Bunge na sheria wanasema kwamba kwa kawaida ripoti kama hiyo ikishawasilishwa bungeni, na kuundiwa azimio, inakuwa ni mwisho, na kinachobaki inakuwa ni utekelezaji tu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge, iliyoichunguza Richmond, Dk. Harrison Mwakyembe aliiambia Raia Mwema wiki hii kwamba yeye hakuwa na la kusema katika suala hilo kwa vile kazi waliyotumwa na Bunge ilikwisha kukamilika.

Lowassa, Karamagi na waziri mwingine ambaye naye alilazimika kujiuzulu, Dk. Ibrahim Msabaha waliipinga ripoti iliyowatuhumu ya Kamati hiyo Teule ya Bunge.

Na juzi Jumatatu, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Emmanuel ole Naiko, alisambaza taarifa kwa vyombo vya habari ikidai kwamba kuhusishwa kwake na TIC katika sakata hiyo kunatokana na njama dhidi ya wazaliwa wa Monduli.

Yeye na Lowassa ni wazaliwa wa Monduli na alipata kuwa msaidizi mkuu wa Sitta wakati Sitta alipokuwa Mkurugenzi Mkuu wa TIC.

Ole Naiko anaituhumu Kamati ya Dk. Mwakyembe kwamba ilijenga mazingira ya kuihusisha TIC na Richmond mapema.

"Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere) aliwahi kuasa kwamba chuki za namna hii ni sawa na mtu kula nyama ya mtu haishii hapo. Kama nia ni kuondoa watu wa sehemu fulani ya nchi yetu tufanye hivyo kwa kuwatendea haki na si kuwajengea mazingira ya namna hii," alisema Ole Naiko.

Baadhi ya waliozungumza na Raia Mwema wanasema maneno yanayoibuka sasa kuhusiana na Ripoti hiyo ya Bunge, ambayo tayari ina maazimio yaliyokwisha kufikishwa serikalini, ni kielelezo tu cha jinsi mgawanyiko ulivyo mkubwa serikalini na ndani ya chama tawala cha CCM.

Raia Mwema ina taarifa za vitendo vya kuchimbana kati ya makundi na wafuasi wa mawaziri waliojiuzulu na ya wale ambao wamebaki.

Habari zinasema kuchimbana huko kuna sura nyingi, lakini za dhahiri ni za kupakana matope, kwa pande zote mbili, kupitia katika vyombo mbalimbali vya habari (si Raia Mwema).

Kuna taarifa pia kwamba suala hilo la kupakana matope limemfikia Rais Jakaya Kikwete na kuna uwezekano kwamba maofisa wake wa masuala ya habari wamekuwa na mawasiliano na baadhi ya waandishi wa habari juu ya jambo hilo.
 
Inavyoelekea Spika kapania kummalizia kabisa huyu jamaa kisiasa.

1.jpg


* Utetezi wake TVT, Monduli watafsiriwa kuwa dharau kwa Bunge
* Spika aagiza kanda za matamshi yake zitafutwe, zichunguzwe

SAKATA ya kampuni hewa ya kufufua umeme ya Richmond bado inachemka na sasa kuna uwezekano mkubwa wa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na madini, Nazir Karamagi kubanwa na Bunge kwa matamshi yao.

Raia Mwema imethibitishiwa kwamba matamshi mengine ambayo yanalianika Bunge vibaya ni ya Waziri wa Sheria, Mathias Chikawe, ambaye ameelezwa kuwa alimtetea Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika aliyetajwa kuhusika katika sakata hiyo ya Richmond.

Chimbuko la hatua hiyo ya Bunge linatokana na hatua ya Lowassa kueleza, katika vyombo vya habari na katika mkutano wake jimboni kwake Monduli, Jumamosi wiki iliyopita, kwamba hakuhusika katika mkataba wa Richmond na kwamba alilazimika kujiuzulu kwa sababu ya uwajibikaji wa pamoja yeye kama mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali.

Raia Mwema
 
Jamani Siasa zilikuwa rahisi wakati wa chama kimoja, wakati ambao waTz tulikuwa tunadumisha fikra sahihi za mwenyekiti wa chama.Sasa hivi siasa ni ngumu sana jamani, mkiziendesha kwa style ya mwaka 47 matokeo ndo yanakuwa hayo jamani...
 
Mzee Six Asijiingize Ktk Matata Tena Maana Nisingependa Kupatwa Na Mshangao Ule Wa Last Kikao,akijiingiza Kichwakichwa Anaweza Akawa Ndiye Anayefuatia Kukiacha Kiti.

Nadhani Ni Haki Ya Jamii Sasa Kujipatia Habari Hii Under Freelance Mediation.

Mtangulizi Wa Speaker Wetu Anasema Hilo Linaruhusiwa Kwa Wananchi Kuikosoa Kamati Ya Mwakyembe,mwansheria Huyu Wa Zamani Ambaye Si Mzamivu Amenukuliwa Na Mageziti Yetu Ya Wagonga Urimbo Akichagiza Uwepo Wa Mwanya Huo.

Ni Vema Pande Zote Zikaangalia Maslahi Ya Nchi Hii Kwanza Na Mengine Ni Neema Ya Mungu Baada Ya Hapo.

Nimuombe Tu Mmeru Lowassa Na Kambi Yake Kuwa Na Subira Kama Binadamu,nirejee Quote Za Raia Mwema Toka Hayati Theodore Roosevelt" Asiyefanya Kosa Ni Yule Tu Asiyefanya Kitu"

Jk Chapa Kazi,chama Kinakuhitaji Na Nchi Inakutaka Uiendeshe Kwa Kasi,ari Na Nguvu Ya Ujasiri; Jasiri Haachi Asili.
 
Mzee Six Asijiingize Ktk Matata Tena Maana Nisingependa Kupatwa Na Mshangao Ule Wa Last Kikao,akijiingiza Kichwakichwa Anaweza Akawa Ndiye Anayefuatia Kukiacha Kiti.

Nadhani Ni Haki Ya Jamii Sasa Kujipatia Habari Hii Under Freelance Mediation.

Mtangulizi Wa Speaker Wetu Anasema Hilo Linaruhusiwa Kwa Wananchi Kuikosoa Kamati Ya Mwakyembe,mwansheria Huyu Wa Zamani Ambaye Si Mzamivu Amenukuliwa Na Mageziti Yetu Ya Wagonga Urimbo Akichagiza Uwepo Wa Mwanya Huo.

Ni Vema Pande Zote Zikaangalia Maslahi Ya Nchi Hii Kwanza Na Mengine Ni Neema Ya Mungu Baada Ya Hapo.

Nimuombe Tu Mmeru Lowassa Na Kambi Yake Kuwa Na Subira Kama Binadamu,nirejee Quote Za Raia Mwema Toka Hayati Theodore Roosevelt" Asiyefanya Kosa Ni Yule Tu Asiyefanya Kitu"

Jk Chapa Kazi,chama Kinakuhitaji Na Nchi Inakutaka Uiendeshe Kwa Kasi,ari Na Nguvu Ya Ujasiri; Jasiri Haachi Asili.

Mkuu, tatizo la kuongea nje ya bunge ni ku "dilute" maamuzi ya bunge, na hatimaye kuyayumbisha kabisa. Huku nje, hawa wanaleta hoja kwa kuzipandikiza, kwa kuwa hakuna mtaalamu wa kuwa hoji juu ya utetezi wao. Tunaishia kuwasikiliza tu na sana sana kuwaonea huruma. Hili lingekuwa murua kama wangaliamua kujitetea bungeni, na bahati wengi ni wabunge.

Mtu kama Edo alikacha kutoa utetezi huu bungeni, anakuja kulia lia huku nje, maana yake nini? Rostam naye hakwenda bungeni wakati wa zogo lile, sasa anavizia kupandikiza utetezi huku nje, sisi tufanyeje? Huko ni kuwahadaa wapiga kura, na ni utapeli wa kisiasa. hawataki credibility yao ishuke kwa makosa waliyoyafanya, na bunge ndo chombo pekee cha wao kujidai nacho, wanaogopa nini?

Bunge ni la wawakilishi wetu, wanajua sheria ikoje. Watatusaidia kuweka sawa mambo. Hakuna haja ya kutulilia huku nje kumbe wanatuhadaa tu, waende bungeni mwezi April. Bunge lina priveleji, haki na kinga, Sitta anachambua ni yepi yamedhulumu haki za bunge, na tutayaona. Msekwa ana haki ya kusema, lakini sasa yeye si spika. Umahiri wa kuchambua sheria unatofautiana pia.
 
Jamani Siasa zilikuwa rahisi wakati wa chama kimoja, wakati ambao waTz tulikuwa tunadumisha fikra sahihi za mwenyekiti wa chama.Sasa hivi siasa ni ngumu sana jamani, mkiziendesha kwa style ya mwaka 47 matokeo ndo yanakuwa hayo jamani...

unajua wakati ule wa chama kimoja,kulikuwa hakuna suala la kuhoji. Ole wako raia uthubutu kuhoji,utaishia jela. Maana hata zile fikira za mwenyekiti wa chama hata kama zilikuwa za kipumbavu,zilirasimishwa zidumu. Wakati huu ambapo watu wana hoji,mambo yamewakalia kooni
Hawa watu,EL,Yona na Rostam,walipewa nafasi ya kutoa maelezo yao.EL pale bungeni,badala ya kueleza kilichokuwa kinaendelea,akakimbilia kutafuta ushajaa ambao leo ndiyo anautumiwa kulialia huku nje kwa raia wamonee huruma.
Mzee Six naye,awe makini,tutahoji uhalali wa hawa watu kijitetea nje ya kamati ya bunge,kama wanaruhusiwa au la.
 
Ndg Spika Sitta naomba uwachukulie hatua wale wote wanaoidhihaki report ya bungue ili iwe fundisho kwa wengine wote.

Kwa sababu haya ni masihara"ukicheka na kima utaambulia mabua" hawa watu nivyema wakashughulikiwa mapema
 
I found this massage very funny

Naye Lowassa akawaambia mawaziri wengine"
KESHENI mkiomba kwani hamjui siku wala saa atakayokuja Dr
Mwakyembe.Nami naenda mtaani kuwaandalia kijiwe ili
nitakapokuwa nanyi muwepo.Nanyi muonapo tume zaundwa
basi mtambue muda wa mavuno ya MAFISADI umekaribia". Kisha akakwea tena Ikulu kuomba Rais asimfilisi. Lakini RICHMOND akatokea na jeshi la Mwakyembe na kusema " Nitakayembusu huyo ndie....!".Mara Chenge akatoa Upanga alani na kumkata mfuasi wa Mwakyembe(Anna Kilango) sikio .Lowassa akamwambia Chenge "rudisha upanga wako alani,Kikombe nilichotupiwa na Kikwete Sina budi Kukinywa"


Moja kati wa mayahudi wale aitwaye Selelii hakuamini kama Lowasa Kajiuzuru,akatwaa mkuki akamchoma ubavuni na tazama...Ikatoka gas ya songosongo na nati ya mitambo ya umeme...Siku ya tatu wakaenda pale ofisini kwake..Lakini wakakuta wingu la Mvi limetanda na Suti ya mistarimistari pale kitini walipomweka..yule morani waliyemkuta getini akawaambia mnayemtafuta hayupo.....Ameshapaa kwenda Monduli na yupo kuume kwa Laiboni..Wakasema..."Hakika huyu alikuwa Fisadi.
 
I found this massage very funny

Naye Lowassa akawaambia mawaziri wengine"
KESHENI mkiomba kwani hamjui siku wala saa atakayokuja Dr
Mwakyembe.Nami naenda mtaani kuwaandalia kijiwe ili
nitakapokuwa nanyi muwepo.Nanyi muonapo tume zaundwa
basi mtambue muda wa mavuno ya MAFISADI umekaribia". Kisha akakwea tena Ikulu kuomba Rais asimfilisi. Lakini RICHMOND akatokea na jeshi la Mwakyembe na kusema " Nitakayembusu huyo ndie....!".Mara Chenge akatoa Upanga alani na kumkata mfuasi wa Mwakyembe(Anna Kilango) sikio .Lowassa akamwambia Chenge "rudisha upanga wako alani,Kikombe nilichotupiwa na Kikwete Sina budi Kukinywa"


Moja kati wa mayahudi wale aitwaye Selelii hakuamini kama Lowasa Kajiuzuru,akatwaa mkuki akamchoma ubavuni na tazama...Ikatoka gas ya songosongo na nati ya mitambo ya umeme...Siku ya tatu wakaenda pale ofisini kwake..Lakini wakakuta wingu la Mvi limetanda na Suti ya mistarimistari pale kitini walipomweka..yule morani waliyemkuta getini akawaambia mnayemtafuta hayupo.....Ameshapaa kwenda Monduli na yupo kuume kwa Laiboni..Wakasema..."Hakika huyu alikuwa Fisadi.
Tanieni imani hii tuu..nyingine msijaribu
 
Hiv sikuiz JF imenunuliwa na CCM. Mnatengeneza post den mnazipa tarehe ya nyuma ili iweje. Post kama hizi ya 2008 haiwezi kuwa na comments zisizozidi hta page moja. JF moderator acheni uhuni hata jana mlitoa post kama hiiii. Tumeisha washtukia tafta njia nyingine.
 
Hiv sikuiz JF imenunuliwa na CCM. Mnatengeneza post den mnazipa tarehe ya nyuma ili iweje. Post kama hizi ya 2008 haiwezi kuwa na comments zisizozidi hta page moja. JF moderator acheni uhuni hata jana mlitoa post kama hiiii. Tumeisha washtukia tafta njia nyingine.
Wewe ni mbumbu tu
 
Huyu BAK sasa hivi ndio mtetezi mkubwa wa Lowasa..hahaha mnafiki sana huyu njaa inamsumbua
Acha kabisa, siasa sio mchezo mzuri. Juzi walimtukana mzee Lowassa, leo amevalishwa ngozi ya kondoo.
 
Back
Top Bottom