Lowassa katumia muda mfupi kuufubaza upinzani

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Lowassa atumia muda mfupi kuumaliza upinzani ndio maneno mafupi unayoweza kuyatumia. Ni kama vile mbwa anavyomfuata chatu huku akilalamika kujiandaa kumezwa ndicho kinachoendelea kwa sasa. Kwani 'wanaomezwa' hawamjui adui yao, wao wanazidi kujipeleka huku wakichukiana wenyewe kwa wenyewe.

Katika kipindi cha mwaka mmoja alichokaa upinzani amefanikiwa kusambaratisha kitu kilichoitwa ukawa bila kujulikana kama yeye ndiye chanzo. Anatengeneza kitanzi anampa Mbowe amtundike Seif yeye anakaa mbali akishuhudia maangamizi bila ya kutambulika,sasa CUF taabani hawajui wanalosimamia, walitangaza kutoshiriki chaguzi zozote huku Chadema wakitumia mwanya huo kusimamisha wagombea kwa mwamvuli wa ukawa japo Prof.Lipumba kashitukia uhuni huo.

Huku akiunda safu yake ndani ya chadema anahakikisha akina Mbowe hawakai ofisini, anawapa safari za ughaibuni huku akijipanga kwenye chaguzi za uongozi wa majimbo chadema. Ni wazi wanazi wa chadema hawazungumzi lolote wametengwa huku wasijue la kufanya na mengi yataonekana kuelekea uchaguzi wa chama. Licha ya Ben Saanane kutuliwa msaidizi binafsi wa Mbowe amejikuta hana kazi ya kufanya zaidi ya kununua magazeti,kutengeneza chai na kukaribisha wageni kwani mambo yote ya kimkakati hufanywa ofisi za mikocheni. Hii tunaita kifo cha kimya kimya,Hakuna kelele.Tutashuhudia mengi sana.
 
Lowassa atumia muda mfupi kuumaliza upinzani ndio maneno mafupi unayoweza kuyatumia. Ni kama vile mbwa anavyomfuata chatu huku akilalamika kujiandaa kumezwa ndicho kinachoendelea kwa sasa. Kwani 'wanaomezwa' hawamjui adui yao, wao wanazidi kujipeleka huku wakichukiana wenyewe kwa wenyewe.

Katika kipindi cha mwaka mmoja alichokaa upinzani amefanikiwa kusambaratisha kitu kilichoitwa ukawa bila kujulikana kama yeye ndiye chanzo. Anatengeneza kitanzi anampa Mbowe amtundike Seif yeye anakaa mbali akishuhudia maangamizi bila ya kutambulika,sasa CUF taabani hawajui wanalosimamia, walitangaza kutoshiriki chaguzi zozote huku Chadema wakitumia mwanya huo kusimamisha wagombea kwa mwamvuli wa ukawa japo Prof.Lipumba kashitukia uhuni huo.

Huku akiunda safu yake ndani ya chadema anahakikisha akina Mbowe hawakai ofisini, anawapa safari za ughaibuni huku akijipanga kwenye chaguzi za uongozi wa majimbo chadema. Ni wazi wanazi wa chadema hawazungumzi lolote wametengwa huku wasijue la kufanya na mengi yataonekana kuelekea uchaguzi wa chama. Licha ya Ben Saanane kutuliwa msaidizi binafsi wa Mbowe amejikuta hana kazi ya kufanya zaidi ya kununua magazeti,kutengeneza chai na kukaribisha wageni kwani mambo yote ya kimkakati hufanywa ofisi za mikocheni. Hii tunaita kifo cha kimya kimya,Hakuna kelele.Tutashuhudia mengi sana.


Mkuu kwa maneno yako upinzani umekufa baada ya kuja lowassa, sasa mbona kila siku mnaleta mabandiko ya upinzani uliokufa?, au hapo lumumba wamewaambia kuwa bila kuisema Chadema posho haiingii?, kama upinzani umekufa kaeni kimya endeleeni Kula hela za rambirambi
 
Lowassa atumia muda mfupi kuumaliza upinzani ndio maneno mafupi unayoweza kuyatumia. Ni kama vile mbwa anavyomfuata chatu huku akilalamika kujiandaa kumezwa ndicho kinachoendelea kwa sasa. Kwani 'wanaomezwa' hawamjui adui yao, wao wanazidi kujipeleka huku wakichukiana wenyewe kwa wenyewe.

Katika kipindi cha mwaka mmoja alichokaa upinzani amefanikiwa kusambaratisha kitu kilichoitwa ukawa bila kujulikana kama yeye ndiye chanzo. Anatengeneza kitanzi anampa Mbowe amtundike Seif yeye anakaa mbali akishuhudia maangamizi bila ya kutambulika,sasa CUF taabani hawajui wanalosimamia, walitangaza kutoshiriki chaguzi zozote huku Chadema wakitumia mwanya huo kusimamisha wagombea kwa mwamvuli wa ukawa japo Prof.Lipumba kashitukia uhuni huo.

Huku akiunda safu yake ndani ya chadema anahakikisha akina Mbowe hawakai ofisini, anawapa safari za ughaibuni huku akijipanga kwenye chaguzi za uongozi wa majimbo chadema. Ni wazi wanazi wa chadema hawazungumzi lolote wametengwa huku wasijue la kufanya na mengi yataonekana kuelekea uchaguzi wa chama. Licha ya Ben Saanane kutuliwa msaidizi binafsi wa Mbowe amejikuta hana kazi ya kufanya zaidi ya kununua magazeti,kutengeneza chai na kukaribisha wageni kwani mambo yote ya kimkakati hufanywa ofisi za mikocheni. Hii tunaita kifo cha kimya kimya,Hakuna kelele.Tutashuhudia mengi sana.


Hichi ulichokiandika nakifananisha na mwanaume anayepigwa na mkewe ndani halafu anapiga kelele "naua nauaa majirani njoo muone huku nammaliza mke wangu huwa sitaki ujinga," lakini majirani kuja wanamkuta yeye ndiyo kapigwa kabali inaitwa "usimwongeze utamuua"
 
Kila mtu anayo namna yake ya kufikiri na hiyo ndiyo namna yako. Lowasa amesaidia sana upinzani kutumia njia za kidiplomasia kufanya siasa na kusukuma hoja zao kuliko kutumia nguvu. Upinzani Lowasa akiwepo una nguvu na mwelekeo wa nguvu kuliko kabla ya Lowassa! Nami hiyo ndiyo namna yangu ya kufikiri.
 
Nilisema siku moja kipindi cha boys two men kimepita..lowasa na kikwete wastaafu siasa. Jk ameshastaafu mbn lowasa hataki kustaafu..!!tatzo lowasa anapenda kuwa relevant kila siku. !

Tunakata damu mpya wazee watupishe..
 
Ingekuwa imefubaa usingekuwa unashinda JF kila siku kuanzisha thread za Chadema.
 
Una hoja gani wewe unayolazimisha watu wajadili? Hizo ni ndoto zako za usiku ukiwa na mumeo hupaswi kuzileta jukwaani. Wewe kaa chini subiri kivumbi cha kata 22 ndio upate cha kusema au kulia. Hata hiyo kazi yako uliyokabidhiwa na chama (au kujikabidhi) utaiona chungu kama una mshipa wa aibu, lakini kama huna basi utaona ni kawaida tuu
safari hii mtakimbiana humu.
 
Huelewi maana ya upinzani.. Naona uandhani upinzani ni kuandamana daily kudindishiana na mapolisi daily.. Lowassa ana siasa safi sana toka ajiunge chadema na Ukawa ushasikia nani kakimbizana na police kwenye mikutano yake we mwenyewe uliona watu walivyokua na umoja.. Tunapinga kimya kimya ikifika 2019 ndio utajua kaja kuufubaza au kuezeka
 
Back
Top Bottom