Lowassa is not opposition material

THINKINGBEING

JF-Expert Member
Aug 9, 2010
2,779
1,304
Kabla ya ujio wa Lowassa CHADEMA wapinzani walikuwa wakikishambulia sana ACT kwamba si chama halisi cha upinzani na kina mpango wa kupokea Lowassa kuwa mgombea wake.

ACT ambacho kilishajengewa sura ya usaliti kwa sababu ya kiongozi wake Zitto ambaye hapakuwa na shaka kuwa amesaliti upinzani kilikuwa kikikabiliwa na shutuma nyingine kwamba kiliandaliwa kumtengenezea njia Lowassa ambaye kwa mtazamo wa upinzani wakati huo Lowassa alikuwa nembo ya ufisadi.

Minong'ono kwamba Lowassa anakuja CHADEMA ulipokelewa kwa mtazamo hasi na wapinzani wa kweli kwa hoja kwamba alikuwa na tuhuma nyingi chafu na hakuwa material ya upinzani.

Minong'ono hiyo iliwafanya wapinzani kuzua mijadala ya wazi ndani na nje ya mitandao kujadili hatma yao.

Wakati wa kampeni kauli ya Lowassa kwamba watu wapige kura tu na wamuachie kazi ya kuzilinda iliwafanya wafuatiliaji wa siasa wapate mashaka na uelewa wa Lowassa kuhusu hali halisi ya kuendesha upinzani nchini ama huenda akawa na lengo tofauti.

Baada ya uchaguzi kufanyika na kuwa na matokeo yenye utata mkubwa Lowassa aliwashangaza zaidi wapinzani kwa staili yake ya kukaa kimya huku wapinzani wakitaka kusikia kauli yake kuhusiana na matokeo hayo.

Hata hivyo baada ya ukimya huo kiliibuka kioja kingine.Lowassa alitangazia umma kuwa jeshi la polisi litaombwa kibali yafanyike maandamano yasiyo na kikomo.Wakati wapinzani wakiwa na uzoefu wa kunyimwa vibali vya maandamano ya kawaida na hata mikutano yeye alisema yaombwe maandamano yasiyo na kikomo.

Watu wenye akili walitafsiri mpango huo wa kuomba maandamano yasiyo na kikomo kuwa ulikuwa mpango wa kuzuia maandamano kabisa.

Jeshi la polisi lilikataa maandamano hayo kama ilivotarajiwa na wengi na ndipo alipoibuka tena Lowassa na kusema hakuna maandamano kwa sababu jeshi la polisi limeamua hivyo.Wenye akili walijua hili ni changa la macho.

Hatimaye Lowassa ameamua kutoa makucha yake na kuonesha misimamo rasmi inayopingana na maazimio ya chama.Wakati BAVICHA wanasema wanaelekea Dodoma kuzuia mkutano wa CCM huyu Lowassa yeye anasema CHADEMA sasa kiachane na harakati. Anasisitiza kwa kusema hapatakiwi maandamano tena wala kuizuia serikali kufanya kazi zake.

Ni wakati sasa wakujiuliza ni nini maana ya tamko hili kutoka wakati BAVICHA wakielekea Dodoma?

Ni wakati wakujiuliza ni nini maana ya kauli hizi tatanishi za Lowassa?

Ni wakati wa kujiuliza je Lowassa ni opposition material?

Ni wakati wa kujiuliza je Lowassa ni liability ama asset?
 
Tumkabidhi chama kwanza Dikteta Uchwara kwa Mujibu wa Tindu Antipass Lisu afu tutaendelea na ya Lowassa
 
U
Kabla ya ujio wa Lowassa CHADEMA wapinzani walikuwa wakikishambulia sana ACT kwamba si chama halisi cha upinzani na kina mpango wa kupokea Lowassa kuwa mgombea wake.

ACT ambacho kilishajengewa sura ya usaliti kwa sababu ya kiongozi wake Zitto ambaye hapakuwa na shaka kuwa amesaliti upinzani kilikuwa kikikabiliwa na shutuma nyingine kwamba kiliandaliwa kumtengenezea njia Lowassa ambaye kwa mtazamo wa upinzani wakati huo Lowassa alikuwa nembo ya ufisadi.

Minong'ono kwamba Lowassa anakuja CHADEMA ulipokelewa kwa mtazamo hasi na wapinzani wa kweli kwa hoja kwamba alikuwa na tuhuma nyingi chafu na hakuwa material ya upinzani.

Minong'ono hiyo iliwafanya wapinzani kuzua mijadala ya wazi ndani na nje ya mitandao kujadili hatma yao.

Wakati wa kampeni kauli ya Lowassa kwamba watu wapige kura tu na wamuachie kazi ya kuzilinda iliwafanya wafuatiliaji wa siasa wapate mashaka na uelewa wa Lowassa kuhusu hali halisi ya kuendesha upinzani nchini ama huenda akawa na lengo tofauti.

Baada ya uchaguzi kufanyika na kuwa na matokeo yenye utata mkubwa Lowassa aliwashangaza zaidi wapinzani kwa staili yake ya kukaa kimya huku wapinzani wakitaka kusikia kauli yake kuhusiana na matokeo hayo.

Hata hivyo baada ya ukimya huo kiliibuka kioja kingine.Lowassa alitangazia umma kuwa jeshi la polisi litaombwa kibali yafanyike maandamano yasiyo na kikomo.Wakati wapinzani wakiwa na uzoefu wa kunyimwa vibali vya maandamano ya kawaida na hata mikutano yeye alisema yaombwe maandamano yasiyo na kikomo.

Watu wenye akili walitafsiri mpango huo wa kuomba maandamano yasiyo na kikomo kuwa ulikuwa mpango wa kuzuia maandamano kabisa.

Jeshi la polisi lilikataa maandamano hayo kama ilivotarajiwa na wengi na ndipo alipoibuka tena Lowassa na kusema hakuna maandamano kwa sababu jeshi la polisi limeamua hivyo.Wenye akili walijua hili ni changa la macho.

Hatimaye Lowassa ameamua kutoa makucha yake na kuonesha misimamo rasmi inayopingana na maazimio ya chama.Wakati BAVICHA wanasema wanaelekea Dodoma kuzuia mkutano wa CCM huyu Lowassa yeye anasema CHADEMA sasa kiachane na harakati. Anasisitiza kwa kusema hapatakiwi maandamano tena wala kuizuia serikali kufanya kazi zake.

Ni wakati sasa wakujiuliza ni nini maana ya tamko hili kutoka wakati BAVICHA wakielekea Dodoma?

Ni wakati wakujiuliza ni nini maana ya kauli hizi tatanishi za Lowassa?

Ni wakati wa kujiuliza je Lowassa ni opposition material?

Ni wakati wa kujiuliza je Lowassa ni liability ama asset?
UMEULIZWA? I
 
Tumkabidhi chama kwanza Dikteta Uchwara kwa Mujibu wa Tindu Antipass Lisu afu tutaendelea na ya Lowassa
Ya CCM hayanihusu.Hata wakimkabidhi chama Snura watajua wenyewe.Mimi najadili ya chama changu.
 
Mzee wa watu anawafahamu vizuri CCM na mifumo ya kikatiba hivyo ameona kutumia nguvu haito saidia.
 
Kuna MTU nilimwambia kwamba kumteua Lowassa ni karata kwa upinzani,ambapo akishinda itakuwa nafuu lakini akishindwa italeta usumbufu sana kwa Upinzani hasa CDM.Kwanza ni MTU ambaye ni rahisi sana Kumprovoke,afu ni mkimya sana sio MTU wa kuweza kukuaminisha jambo/kujibu jambo kwa hoja.Ila kinachosaidia upinzani ni mapungufu ya CCM,watu wengi wanaichukia CCM na bado wao wenyewe hawajagundua makosa yao wanayarudia kila kukicha.
 
Kuna MTU nilimwambia kwamba kumteua Lowassa ni karata kwa upinzani,ambapo akishinda itakuwa nafuu lakini akishindwa italeta usumbufu sana kwa Upinzani hasa CDM.Kwanza ni MTU ambaye ni rahisi sana Kumprovoke,afu ni mkimya sana sio MTU wa kuweza kukuaminisha jambo/kujibu jambo kwa hoja.Ila kinachosaidia upinzani ni mapungufu ya CCM,watu wengi wanaichukia CCM na bado wao wenyewe hawajagundua makosa yao wanayarudia kila kukicha.
Mkuu una tstizo la kimsingi kabisa.
Ati watu wanaichukia CCM , alafu huku wanaichagua kuongoza nchi?

Sema wewe unaichukia, na isemee nafsi yako!

Juu ya Lowassa, alipojiondoa CCM kwa uchu wake wa madaraka mlifikiri mmelamba dume, kumbe garasa!
And mind you Lowasa yuko hapo si kwa vile ameitwa, kaja kwa hela yake na hamna ubavu wa kumtosa.
 
Mkuu una tstizo la kimsingi kabisa.
Ati watu wanaichukia CCM , alafu huku wanaichagua kuongiza nchi?
Sema wewe unaichukia, na isemee nafsi yako!

Juu ya Lowassa, alipojiondoa CCM kwa uchu wake wa madaraka mlifikiri mmelamba dume, kumbe garasa!
And mind you Lowasa yuko hspo si kwa vile ameitwa, kaja kwa hela yake na hamna ubavu wa kumtosa.
Mimi nimetoa maoni yangu na sijasema Niko upande gani!!BTW nimesema watu wengi(hasa wanaojielewa) wanaichukia CCM coz ndio wapo madarakani but so far hawajaonyesha nia ya dhati ya kuwasaidia wananchi,kidogo mwanzoni kwa Magufuli waliona kunaweza kukawa na mwanga lakini naye kila siku anarudia makosa yaliyofanyika huko nyuma na hata kuonesha makosa zaidi ya yaliyofanyika.
 
chama amekiua mbowe na anazidi kuiua.luwasa na cdm niwapinawapi?siasa za nch km hzi zakwetu inahitaji uwanaharakati zaidi kuliko anayotaka kufanya luwasa.cdm ingefanya makubwa hata kuchukua dola km c tamaa ya mbowe.anyway tumerudi tna miaka kumi tna nyuma kujenga upinzani
 
Back
Top Bottom