Lowassa anyimwa Visa ya kuingia UK?

Kimbembe

Senior Member
May 14, 2006
122
15
Ninapewa habari muda huu kwamba ndugu aliyekuwa Waziri Mkuu asiye mstaafu kwa mujibu wa Sheria baada ya kuondoka toka Dodoma na kutulia Dar kabla ya kwenda Monduli aliomba Visa ya kwenda UK akapigwa chini.Habari za kupigwa chini kwenye maombi yake hazijajulikana lakini nadhani vyanzo vya Ubalozi wanasema hawakutaka akasemee nje na pia walikuwa na wasi wasi alikuwa anataka kuhangaika na pesa zake kwenye account za nje .

Habari zikija nitawapa na kama kuna mwenye kujau zaidi karibu uendeleze hapa .
 
Ninapewa habari muda huu kwamba ndugu aliyekuwa Waziri Mkuu asiye mstaafu kwa mujibu wa Sheria baada ya kuondoka toka Dodoma na kutulia Dar kabla ya kwenda Monduli aliomba Visa ya kwenda UK akapigwa chini.Habari za kupigwa chini kwenye maombi yake hazijajulikana lakini nadhani vyanzo vya Ubalozi wanasema hawakutaka akasemee nje na pia walikuwa na wasi wasi alikuwa anataka kuhangaika na pesa zake kwenye account za nje .

Habari zikija nitawapa na kama kuna mwenye kujau zaidi karibu uendeleze hapa .

Ungejiandaa vizuri na ukaja na habari kamili.


Mtu hawezi kunyimwa viza eti kwa sababu ataenda "kusemea nje" au "kuhangaika na pesa" zake kwenye a/c za nje.

Usigeuze jamvi hili makini kuwa kama kijiwe cha kunywa kahawa
 
Ungejiandaa vizuri na ukaja na habari kamili.


Mtu hawezi kunyimwa viza eti kwa sababu ataenda "kusemea nje" au "kuhangaika na pesa" zake kwenye a/c za nje.

Usigeuze jamvi hili makini kuwa kama kijiwe cha kunywa kahawa


Kwa kuongezea Visa yenyewe ya kunyimwa kwa sababau hizo sio ya UK...!! Labda nchi nyingine...
 
Hawa wadaku wengine kwa nini hawaziweki hizi habari kwenye udaku? mods, tafadhali pelekeni hii habari kwenye udaku, yaani inawekwa kwenye habari mpya au kwa kimombo "breaking news" na ma mods mnakubali.
 
Jamani, naona hamko fair kwa jamaa aliyeanzisha mada hii. Key word, amesema anadhani. Sasa kwa nini mseme hii ipelekwe udaku?
 
Jamani, naona hamko fair kwa jamaa aliyeanzisha mada hii. Key word, amesema anadhani. Sasa kwa nini mseme hii ipelekwe udaku?

Ndio maana nikamshauri angejiandaa kabla ya kuja na hii habari, kwa uzito wake kuimwaga hapa kwa "kudhani" si sahihi kabisa
 
Narudia kwamba tena kusema kwamba sababu kamili ya kunyimwa hazijawa clear .Bado nina ninatafuta uhalali wa hii habari .Nikiwa na habari sahihi nitasema ila ukweli wa kinyimwa Visa si udaku Lowasa kanyimwa Visa ya UK .
 
Kishoka,
Hata diplomatic passport zinahitaji visa kwa baadhi ya nchi.
 
Narudia kwamba tena kusema kwamba sababu kamili ya kunyimwa hazijawa clear .Bado nina ninatafuta uhalali wa hii habari .Nikiwa na habari sahihi nitasema ila ukweli wa kinyimwa Visa si udaku Lowasa kanyimwa Visa ya UK .

Siku nyingine jiandae kwanza kabla ya kuja na udaku kama huu hapa! Sio uje na udaku halafu ndio uende kujiandaa. Do the other way round. ok?
 
Jamani, naona hamko fair kwa jamaa aliyeanzisha mada hii. Key word, amesema anadhani. Sasa kwa nini mseme hii ipelekwe udaku?

Nakubaliana na wewe. Kuna 'udaku' mwingine unafanya vichwa vijisugue kutoa mawazo. Kwa mfano nilikuwa na wazo lifuatalo;

Kwa nini tusipetition hizi balozi zilizopo TZ ili zote ziwanyime viza washukiwa wote wa Richmond, EPA, BOT n.k. mpaka hapo ukweli utakapojulikana? Maana serikali haijali kwa vile wengi waliomo ni wahusika otherwise wangeharakisha kuwanyang'anya pass zao kama walivyokuwa na haraka ya kuwatia ndani moderators wa JF. Waungwana mnasemaje??
 
Ninapewa habari muda huu kwamba ndugu aliyekuwa Waziri Mkuu asiye mstaafu kwa mujibu wa Sheria baada ya kuondoka toka Dodoma na kutulia Dar kabla ya kwenda Monduli aliomba Visa ya kwenda UK akapigwa chini.Habari za kupigwa chini kwenye maombi yake hazijajulikana lakini nadhani vyanzo vya Ubalozi wanasema hawakutaka akasemee nje na pia walikuwa na wasi wasi alikuwa anataka kuhangaika na pesa zake kwenye account za nje .

Habari zikija nitawapa na kama kuna mwenye kujau zaidi karibu uendeleze hapa .


niliposema kuwa tuachane na mambo ya kucopy news from magazeti yetu a,bayo hayana credibility nilimabisha kuwa tuwe makini kwenye sources na hata kama source ikiwa makini basi tuwe tunachambua news kbla ya kuimwaga humu

thatsa what i meant by setting the agenda
 
Taratibu za kuomba Viza kwa Diplomatic passport-holders ni tofauti na za akina sie. Hawa wanaombewa na foreign na hawalipii viza fees na incase watanyimwa viza balozi husika hutoa maelezo kwa maandishi kwenda foreign office.
 

niliposema kuwa tuachane na mambo ya kucopy news from magazeti yetu a,bayo hayana credibility nilimabisha kuwa tuwe makini kwenye sources na hata kama source ikiwa makini basi tuwe tunachambua news kbla ya kuimwaga humu

thatsa what i meant by setting the agenda

I beg to differ.​
Sio kila nyuzi lazima sosi yake ijulikane. Lakini ni uzito wa suala ndio unaosababisha iwe news au la. Ni vema imeletwa hii ya huyu fisadi mkuu ili wenye masikio makubwa zaidi kuliko Bw. Kimbembe nao wajaribu kudadisi zaidi. Tusimkatishe tamaa ila tuendelee kum-mminya ili atuletee zaidi vile anavyozipata hizi nyeti bubu.
 
Kichwa cha habari ni: Lowasa anyimwa Visa ya kuingia UK.

Inaonekana mleta habari anao uhakika na hilo. Asilo kuwa na uhakika nalo ni sababu zilizofanya anyimwe visa.

Hili jambo la kunyima visa viongozi wanaoshukiwa kujihusisha na rushwa ni la kawaida kabisa siku hizi kwa ubalozi wa UK.
Kenya yamekwishawapata wengi; kama vile Chris Murungaru na the 'Total Man' wa kule Keito.

Wakenya wanayajua sana haya, na yanawaogopesha sana.

Sitashangaa hata kidogo kama UK sasa wameamua kuishushia ngoma hiyo ngoma Bongo.
 
I beg to differ.​
Sio kila nyuzi lazima sosi yake ijulikane. Lakini ni uzito wa suala ndio unaosababisha iwe news au la. Ni vema imeletwa hii ya huyu fisadi mkuu ili wenye masikio makubwa zaidi kuliko Bw. Kimbembe nao wajaribu kudadisi zaidi. Tusimkatishe tamaa ila tuendelee kum-mminya ili atuletee zaidi vile anavyozipata hizi nyeti bubu.

Nina fuatilia issue hii yote mie nitakuja na habari kamili za Visa na Lowasa kutoswa sijakurupuka ila nimewahi kupakua kabla hakijaiva .
 
He has our diplomatic passport, does he still needs a Visa to enter UK?
ILE YA WEAZIRI MKUU KASHANYANG'ANYWA kwa sasa anayo passport ya kidiplomasia ya kawaida tu kama wabunge wengene nadhani ya waziri mkuu ni no 4 so hawezi kuwanayo tena
 
Huyu mwenzetu maesikia tetesi (kumbukeni Richmond nayo ilianza kama tetesi) na ameiweka hapa akisema bayana kuwa kama kuna mtu mwenye data zaidi aongezee.Sasa kosa lake liko wapi?How many times watu wamekuja hapa na mawazo yao binafsi ambayo definitely source ni wao wenyewe (holders wa mawazo hayo).

Udaku ni kusema Lowassa kajiunga na chadema but kusema "kuna habari/etetsi kuwa lowassa ana mpango wa kujiunga na chadema" sio udaku.Ni muhimu kila habari iwe na chanzo lakini vp kuhusu tetesi kwa mfano hiyo ya dude liitwalo AGENDA 21?Au vipi kitu kitwacho "MTANDAO" ambacho licha ya kutajwa sana hakuna mahala popote panapozungumzia dude hilo lilivyoundwa,lilikuwa/lina members wa ngapi,etc.

Tukitaka source kwenye kila posts,then hii itageuka kuwa sehemu ya ku-copy na ku-paste tu ilhali kuna habari lukuki za mtaani (na tusisahau kuwa hatuna transparent media inayoweza kuandika kila kitu).Naamini kwamba iwapo tetesi hii ingepostiwa na "jina linaloaminika" wala isingeshutumiwa namna hii.Let's be fair for our own JF's benefits.
 
jamanieee huyu ELnimebahatika kupanda nao ndege moja leo yeye na mkewe na wanaelekea israel kuhiji tumeachana nao addis ababa airport kwa kweli nimeshangaa kuwaona wanaenda hija kweli watu wakipatwa na matatizo sijui ndio wanamkumbuka mungu au?
 
Back
Top Bottom