Lowassa and Co., waliteka Bunge; Sitta, Mwakyembe kudhibitiwa

January Makamba hata kabla ya barua yake haijajibiwa anawekwa mwenyekiti kamati ya Nishati!!!!!!!! au ile barua ilikuwa danganya toto?
 
Hivi kwa nini Watu wazima na akili zao wanakuja humu bodini kuongea damu, kufa, kujitoa mhanga, makaburi n.k

Haya mambo ya kufa kufa yote yanatoka wapi...!!!!
 
Kuchaguliwa kwa Edward Lowassa, waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond/Dowans kuwa mwenyekiti wa the most powerful committee in the National Assembly -- Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, ina maana kuu zifuatazo:

1. Anajitengenezea CV ya kuwa mgombea Urais wa CCM 2015. Moja ya vigezo vikubwa vya CCM ni mgombea wa Urais kuwa na uzoefu wa mambo ya nje. Hapa Lowassa anajipatia CV hiyo kupitia kamati hii ya Bunge.

2. Akiwa mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje, ulinzi na usalama, atakuwa anapata security briefings na issue zote nyeti, kama Meremeta, rada, Kagoda, usalama wa taifa, Takukuru, polisi, jeshi, nk, vinapitia kwake. Anakuwa na powers ku-summon wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama hapa nchini.

3. Anapata meno ya kumshuhulikia adui wake mkuu kwenye mbio za urais, Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, kwani kamati ya mambo ya nje ndiyo inayosimamia wizara ya Membe. Pia Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, naye ayakuwa anasimamiwa na kamati hiyo ya Lowassa.

4. Mpambe wa Lowassa, Peter Serukamba, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ili awashuhulikie kina John Magufuli na Dk. Harisson Mwakyembe wa wizara ya ujenzi.

5. Mpambe mwingine wa Lowassa na Rostam Aziz, January Makamba, amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini ili amfukuze kazi Ngeleja na kumuweka waziri wao mwingine na azime issue za Dowans/Richmond.

6. Zitto Kabwe, ambaye ni mtu wa CCM kabaki kamati ya mashirika ya umma kama kanyaboya. Kamati za PAC na local government wamepewa CUF na UDP ambao ni vibaraka wa CCM.

Lowassa, January na Serukamba wanaingia kwenye kamati ya uongozi wa Bunge wakiwa wenyeviti wa kamati ya Bunge. Hii ina maana kuwa watakuwa wana influence shuhuli za Bunge, kanuni, miswada na hoja mbali mbali.

Anne Makinda ndiyo aliyewateuwa kina Lowassa, January, Serukamba kuwa kwenye kamati hizi kwa maelekezo ya Rostam Aziz aliyemuweka kuwa Spika. Amewateuwa wajumbe wachovu kwenye kwenye kamati hizi ili watu hawa wakamate uongozi wake.

Ni dhahiri kuwa mafisadi sasa wameliteka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!

Mwaka huu tutapona ??????? Hatari tupu, KUJIPANGA 2011 ni mbali , sijui ni vipi tena. TUMEKWISHA, kama mafisadi ndo wamepewa marungu tutatokea wapi?????
 
Hivi kwa nini Watu wazima na akili zao wanakuja humu bodini kuongea damu, kufa, kujitoa mhanga, makaburi n.k

Haya mambo ya kufa kufa yote yanatoka wapi...!!!!


Usichokijua ni kama usiku wa giza,saa yaja ukweli utabaki kuwa ukweli.
 
He who has the gold, makes the rules wakuu!
R.A Anachezesha mchezo!
 
jamaan ccm wapo wengi bungen but maamuzi ya sawa wendawazimu!! wanaweza wakamchagua hata RA one the post just because RA hapendi vyeo anapenda wizi2.
 
Ningependa kujua hizo posts ndio zingeenda CHADEMA zote kama ile kanuni isingebadilishwa au ndio ingekua hivyo hivyo?
 
Hata hhao waliotuma hawajui virefu vyake.
Si kwamba hawajui, matarajio yao ni kwamba kamati hizo zinahitaji akili ya kawaida tu ya kuzijua hasa kama mtu anafuatilia siasa za Tanzania na kwingineko. Ok
1. LAAC- LOCAL AUTHORITIES ACCOUNTS COMMITTE (KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA)
2. POAC-PUBLIC ORGANIZATION ACCOUNTS COMMITTE (KAMATI YA HESABU ZA MASHIRIKA YA UMMA)
3.PAC- PUBLIC ACCOUNTS COMMITTEE (KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI)

Hizo ndizo kamati nyeti ambazo CCM hawataki ziangukie mikononi mwa CDM kwani ndizo zilizowamaliza kwaenye uchaguzi uliopita. LAAC iliongozwa na Dr. Slaa, POAC -Zitto kabwe na PAC na John Cheyo. Hope tupo pamoja mpaka hapo
 
Enzi nikiwa shule ya msingi nakumbuka tuliimba mara nyingi wimbo wa Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote.... Niliipenda Tanzania, Naendelea kuipenda Tanzania lakini mwenendo wa viongozi wangu unanifanya kuwa nchi yangu ninayoipenda kuwa iko kwenye ukoloni mbaya zaidi ya ule tuliokuwa nao wakati wa waingereza na wajerumani. Kazi kubwa niliyo nayo kama mwanajamii ninayeipenda tanzania ni kuipatia uhuru wake kutoka ktk ukoloni huu mbaya usiokuwa na chembe ya ubinadamu hata chembe. Ee Mungu nisaidie.
 
Halijaaribika jambo, mlongo mmoja ukifungwa mingine 10 inafunguliwa!!
Ni just wanatuchelewesha kufika tunapotaka kufika, lkn tutafika tu !!

People's power is god's power!! Hakuna wa kuizuia
 
Asante Kiranja, ushindi wa Zitto POC ni uthibitisho kuna wana CCM wameamua kuachana na unazi na kuchagua mtu. Jana usiku kucha wamekuwa wakitumiana sms za msisitizo PAC -Cheyo, LAC- Mrema na POC- CUF.
acha fiksi....
 
Ningependa kujua hizo posts ndio zingeenda CHADEMA zote kama ile kanuni isingebadilishwa au ndio ingekua hivyo hivyo?
Zingeenda Chadema bila shaka kwa sababu wagombea wangekuwa toka kambi rasmi ya upinzani bungeni. CCm wasingekuwa na namna zaidi ya kupiga kura kuwachagua CDM
 
Samora10, EL is much better person than all those other guys you may see them there. He took nothing out of Dowans and Slaa confirmed in a public meeting in Arusha the same day they were attached by police!
Tuacha chuki binafsi, EL is clean in terms of Dowans. But for sewage politics, you can call him whatever, but the fact is he is clean on Dowans/Richmond perspective.
Even Sitta himself he cleared him in a rally.
I like EL he can perform and he is a follow through leader!
 
Nguvu ya umma ni kubwa kuliko hilo Bunge mshenzi. Tujipange tuangalie namna ya kuwatia adabu mafisadi na vibaraka wao wote. Tusifanye makosa, la sivyo tumekwisha.
 
Back
Top Bottom