Subira the princess
JF-Expert Member
- Mar 3, 2018
- 2,424
- 2,587
Wasalaam, tumebakisha takribani miaka 2 kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu 2020. Naona mzee Lowassa anaendelea kufanya siasa za kistaarabu na kizalendo. Tuliona mh Lowassa akienda ikulu, alienda ktk uzinduzi wa maktaba UDSM, na leo kuna taarifa kamili kwamba yupo Zanzibar kwa mwaliko wa katibu mkuu wa CUF mh Maalim Seif.
Kwa mlolongo wa matukio haya ni wazi mzee Lowassa anajipanga kwa ajili ya uchaguzi 2020 kwa kutumia akili nyingi na saikolojia ya hali ya Juu, wakijakustuka itakua kumepambazuka ni asubuhi. Usimdharau mtu aliepata kura mil6 + za watanzania, inawezekana Lowassa yupo mioyoni mwa watanzania wengi. Ukiangalia hali ya siasa kwa sasa CCM inahali mbaya Sana, sote tujiulizie ikitokea timu ya Membe ikatoka CCM na kuungana na upinzani chini ya comredi Lowassa unafikiri CCM itapona? Maana itakua CCM +ACT+CDM+CUF+NCCR+NLD+ vs CCM awamu ya tano.
CCM wamelala, wakistuka picha limekwisha wanaona ni fahari kudili na Mbowe na viongozi wa CHADEMA wamemsahau comredi anachanja mbuga mbele kwa mbele.
Kwa mlolongo wa matukio haya ni wazi mzee Lowassa anajipanga kwa ajili ya uchaguzi 2020 kwa kutumia akili nyingi na saikolojia ya hali ya Juu, wakijakustuka itakua kumepambazuka ni asubuhi. Usimdharau mtu aliepata kura mil6 + za watanzania, inawezekana Lowassa yupo mioyoni mwa watanzania wengi. Ukiangalia hali ya siasa kwa sasa CCM inahali mbaya Sana, sote tujiulizie ikitokea timu ya Membe ikatoka CCM na kuungana na upinzani chini ya comredi Lowassa unafikiri CCM itapona? Maana itakua CCM +ACT+CDM+CUF+NCCR+NLD+ vs CCM awamu ya tano.
CCM wamelala, wakistuka picha limekwisha wanaona ni fahari kudili na Mbowe na viongozi wa CHADEMA wamemsahau comredi anachanja mbuga mbele kwa mbele.