Lowassa amuambia Magufuli: Huwezi pambana na matajiri, hawa ndio wanaoleta viwanda na ajira

chinchilla coat

JF-Expert Member
May 16, 2016
5,107
10,961
Aliyekuwa mgombea wa urais wa CHADEMA Edward Lowassa akiongea katika mkutano wa mameya wa CHADEMA uliofanyika Arusha amesema kuwa serikali haiwezi kupambana na watu wa tabaka la kati kwa kuwa wao ndio hutoa ajira na kuanzisha viwanda kwa kuwa serikali haiwezi kufanya hivyo, amesema badala yake serikali inatakiwa kuendeleza tabaka la watu wa kati ili waweze kutoa ajira na kuanzisha viwanda na kutaka serikali isafishe hali ya hewa kuhusu suala la VAT,

Pia akiongea katika mkutano huo meya wa Arusha Kalisti Lazaro amesema kuna haja ya kuwa na mjadala wa taifa kuhusu aina ya kodi zinazotozwa nchini, ametolea mafano wa wingi wa kodi iliyopitiswa kwenye sekta ya utalii inaenda kusababisha anguko la uchumi kwa kuwa na utitiri wa kodi ambao unafikia kodi 32
Naye katibu mkuu wa CHADEMA Vincent Mashinji amesema serikali inatakiwa kutafakari ni kodi zipi ambazo ni kandamizi na ni zipi zitamletea maendeleo mwananchi

MY TAKE
Ni kweli kuwa nchi hii ilikuwa na ukwepaji kodi mkubwa ambao ulisababishwa na uongozi uliopita kufuga uozo huu, na Magufuli anataka airudishe kodina uchumi ukue kwa kasi

Lakini kwenye swala kama hili kuna hitajika umakini kwa kuwa hao wakwepa kodi hao hao ndio walioshikilia uchumi wa nchi na kuajiri watanzania wengi, na hata kodi ya sasa hivi inayokusanywa inawategemea wao kwa kiasi karibia chote.... hili halijasemwa na mimi wala Lowassa tu bali hata kada wa CCM Bernad Membe alishaonya kunatakiwa umakini kwenye kupambana na wafanyabiashara ambao ndio wameshikilia uchumi kwa kiasi kikubwa

sasa ishu kama hii inahitaji uifanye kwa process ili usilete shock kwa wafanya biashara na pia kwa wananchi na hatimae kwa serikali, huko tunakotaka kwenda tutafika tu kwa kuwekeana kanuni na sio kufanya mambo kwa pupa ili uonekane wewe ni hero wa wanyonge kumbe ndio unawatia njaa zaidi.......na bado uchumi mwenyewe ni mchanga


Kusema unawapa siku saba watu walipe kodi waliyokwepa kwa miaka karibia kumi kwa kuruhusiwa na system mbovu iliyokuwepo unaweza kushangaa unasabaisha wafanyabiashara karibia waote kupunguza wafanyakazi au kufilisika na kusababisha vilio mtaani na serikali kukosa yale mapato makubwa ya muda mrefu kama wafanya biashara hao wange survive kwa kulipishwa kidogo kidogo

Pia kulazimisha mabenki kulipa kodi ambayo kikanuni inatakiwa ilipwe na mwananchi, unatuma ujumbe mmbaya kwa potential investors waliokuwa wanafikiria kuja kuwekeza Tanzania

Kuongeza kodi ya VAT kwenye utalii na bila kukaa meza moja na wadau na hawa wenye makampuni ya utalii huku utaliiwenyewe ndio bado mchanga, pia sio busara
kupiga marufuku sukari na kutoa vitisho na kuvamia maghala ya watu ili ufurahishe wanyonge wengi ili wakushangilie pia hii ina send messge mbaya sana kwa wawekezaji waliokuwa wanai consider Tanzania kama nchi yenye mazingira mazuri ya uwekezaji,

Magufuli ana miaka 1o ya kutawala na kuleta maendeleo na asitake kufanya mambo kwa pupa na sifa kuwafurahisha watu wanyonge wasiojua kanuni za uchumi
 
Aliyekuwa mgombea wa urais wa CHADEMA Edward Lowassa akiongea katika mkutano wa mameya wa CHADEMA uliofanyika Arusha amesema kuwa serikali haiwezi kupambana na watu wa tabaka la kati kwa kuwa wao ndio hutoa ajira na kuanzisha viwanda kwa kuwa serikali haiwezi kufanya hivyo, amesema badala yake serikali inatakiwa kuendeleza tabaka la watu wa kati ili waweze kutoa ajira na kuanzisha viwanda na kutaka serikali isafishe hali ya hewa kuhusu suala la VAT,

Pia akiongea katika mkutano huo meya wa Arusha Kalisti Lazaro amesema kuna haja ya kuwa na mjadala wa taifa kuhusu aina ya kodi zinazotozwa nchini, ametolea mafano wa wingi wa kodi iliyopitiswa kwenye sekta ya utalii inaenda kusababisha anguko la uchumi kwa kuwa na utitiri wa kodi ambao unafikia kodi 32
Naye katibu mkuu wa CHADEMA Vincent Mashinji amesema serikali inatakiwa kutafakari ni kodi zipi ambazo ni kandamizi na ni zipi zitamletea maendeleo mwananchi



Hahah Mafisadi wameanza kufikiwa, hela zetu mlizoiba ni lazima zirudi kwa kodi dadadeki! Fisadi lowasa ameanza kulia lia na bado Kodi ni lazima mlipe kama hamtaki hamieni Kenya labda huko hamtalipa!
 
Back
Top Bottom