Soma kwanza uelewe alichoeleza mkuu, soma soma soma kwanza kabla ya maoni yako! Labda kama utahitaji ufafanuzi juu ya maelezo yake
Suala la sheikh farid wa uamsho liko mahakamani anaposema atamwachia hapo anaingilia uhuru wa mahakama. Kuna tatizo gani sheria kuchukua mkondo wake?
Inamaana akiwa rais hakuna haja ya kuwa na mhimili wa mahakama na ofisi ya DPP? Kwani mashauri atakuwa anaamua sebuleni kwake! Utakuwa utawala wa hovyo sana.
Wakuu Salaam!
Napenda kunukuu neno kwa neno kadri nilivyosikia Mzee Lowassa akielekeza maneno yake kwa Mzee Kinana.
"Kuna mtu mmoja mwenye mamlaka kwenye Chama, tena Muislam, akaandika barua kwenye gazeti moja nchini MAREKANI, gazeti maarufu kidogo." Akasema 'LOWASSA ANAPENDA MAGAIDI NA ATAENDELEZA MAGAIDI, na AKICHAGULIWA kuwa RAIS ATALETA UGAIDI NCHINI'.
Lowassa anaendelea...Sasa nataka nirudie majibu yangu kwake na kwa waTanzania...nilisema 'NITAZINGATIA SHERIA KUCHUNGUZA KAMA WALE MA - SHEIKH WAMEONEWA na KAMA TARATIBU ZA KISHERIA ZILIFUATWA na KAMA HAZIJAFUATWA NITAWATOA NJE mara MOJA , sasa NAMRUHUSU HUYO ANAETAKA KUSHTAKI DUNIANI AKASHTAKI KOKOTE, angojee TU NIWE RAIS.
Anaendelea Lowassa...Nchi hii ina AMANI kwa sababu TUNAHESHIMIANA hakuna watu wenye HATIMILIKI wa nchi hii kwamba wanachosema wao ni sawa. Mimi nimesema jamani nitachunguza upungufu wa sheria na nitachukua hatua wala SIOGOPI NG'O. kamaliza
MY TAKE:wiki kazaa zilizopita Mzee KINANA aliandika article katika blog ya The HILL tukasoma, Mzee LOWASSA nae kasoma kisha akakaa kimya lakini jana akiwa Pemba hayo ndio majibu yake! Aksante.
Pamoja na madhaifu yake, ndugu yangu hayo makundi ni hatari kwa usalama wa nchi na utawala wowote. Ni mabomu yaliyotegwa na yanaweza kulipuka muda wowote. Hakuna mgombea wa urais anayeyakashifu au kuyaweka pembeni. Nafikiri kikubwa unachoweza kumsifia Lowassa ni uwezo aake wa kuvumilia na kukaa kimya bila kuropoka anapochokozwa au kutukanwa. Binafdi siwezi.hamjitambui, anatumia kutokumfaham kwenu na udhaifu wetu kuwatumia kama daraja la kutimiza yake. Kashakwambia akishinda yy atashugurika na mama lishe na bodaboda je na ww mama lishe au bodaboda? Huyu mtu tapeli hana maono ya kulifikisha taifa hili ktk maendeleo endelevu, akataliwe kwa njia yoyote ile
Kila nikimuwazia Lowassa sipati jibu,zaidi natamani kila mtu awe kama mimi.
Yaani tumchague ashinde kwa kishindo...naiona Tanzania mpya chini ya Lowassa.
huyu mzee jamani..au ndo katumwa na Mungu kuja kutuokoa watanzania..
alaf tizama wale wote wanaomtukana wanatangulia mbele za haki
Subirini kipigo cha Oktoba 25. Hayo mengine sijui ana busara mtayajua wakati huo. Busara hizo kazipata UKAWA?
huyu mzee jamani..au ndo katumwa na Mungu kuja kutuokoa watanzania..
alaf tizama wale wote wanaomtukana wanatangulia mbele za haki