Lowassa amfunika Pinda: Makampuni yapitia kwake

Paparazi Muwazi

JF-Expert Member
Dec 23, 2007
310
79
Pinda awafunika Lowassa Pinda na Ole Sendeka-Makampuni yapitia kwake

MBUNGE wa Monduli mkoani Arusha, Edward Lowassa pamoja na marafiki zake na kampuni binafsi, wamechangisha Sh milioni 34.5 kwa Kamati ya Maafa ya Mererani ifanye kazi yake ya uokoaji kwa uhakika na kuwa na vifaa vya kisasa.

Lowassa alizitaja kampuni zilizochangia ni MMT Ltd ambayo ilichangia Sh milioni tano, Kampuni ya simu ya Vodacom ilitoa Sh milioni 20, Kampuni ya mafuta ya Oil Com ilitoa Sh milioni mbili, Kampuni ya Utalii ya Muyomba ilitoa Sh milioni mbili na Kampuni ya Caspian ilitoa Sh milioni tatu.


Mbunge huyo ambaye juzi alitembelea mafuriko katika jimbo lake, katika maafa hayo ya Mererani alichangia Sh milioni mbili na kuwataka viongozi wa Kamati ya Maafa kuhakikisha fedha hizo zinazochangwa na kampuni na watu binafsi zinafanya kazi iliyokusudiwa.


Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu hadi Februari mwaka huu alipojiuzulu, alisema serikali pekee isiachiwe katika masuala ya fedha kwani ina majukumu mengi ya kitaifa, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuchangia maafa hayo.


Katika kuboresha kamati hiyo, serikali imetoa Sh milioni 49.9 kutoka katika mfuko wake wa maafa kwa ajili ya kusaidia shughuli za uokoaji miili ya watu waliokumbwa na mafuriko katika machimbo ya madini ya tanzanite yaliyopo Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Henry Shekifu, alisema fedha hizo zimeshafika mikononi mwake na tayari zimewasilishwa katika akaunti maalumu iliyofunguliwa katika Benki ya NMB tawi la mjini Arusha.


Shekifu ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa, alisema bajeti kamili ya fedha kwa shughuli za uokoaji miili hiyo ni Sh milioni 128, hivyo amezitaka taasisi, kampuni na watu binafsi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha wanachangia mfuko huo ili shughuli hizo zifanyike kwa urahisi na haraka.


Alisema fedha ni muhimu katika shughuli hiyo kwani katika bonde lililopitisha maji bajeti yake pekee inahitaji Sh milioni 25 ili kuweka mtaro wa kuzuia maji kutoingia kirahisi katika machimbo hayo ya kitalu B na bila kufanya hivyo maafa yatakuwa yakitokea kila mara.


Mfuko huo kwa sasa una fedha taslimu Sh milioni 27 na hundi Sh milioni mbili na kutokana na msaada kutoka Serikali Kuu, huenda kwa kiasi fulani zoezi la uokoji litafanikiwa. Alizipongeza Benki za NMB na Standard Chartered kwa pamoja kwa kila benki kutoa Sh milioni 10, alisema.
 
Sorry for the asking ..... how is the headline related to the story, I couldnt find Pinda in the story. And what is the source for this?
 
Mbona kichwa cha habari na story haviendani?
kama vichwa vya habari vya magazeti ya ijumaa,kiu n.k
 
Mbunge huyo ambaye juzi alitembelea mafuriko katika jimbo lake, katika maafa hayo ya Mererani alichangia Sh milioni mbili na kuwataka viongozi wa Kamati ya Maafa kuhakikisha fedha hizo zinazochangwa na kampuni na watu binafsi zinafanya kazi iliyokusudiwa.

Kama hii habari ni ya kweli, Do these people think before they speak! ni mapesa kiasi gani hayakuwafikia walengwa wakati ulipopewa dhamana ya kutetea na kusimamia maslahi ya wananchi? leo hii umetoa vimilioni viwili unangangania ziwafikie walengwa. please kama mtu hana kitu cha kusema ni heri anyamaze tu.

Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu hadi Februari mwaka huu alipojiuzulu, alisema serikali pekee isiachiwe katika masuala ya fedha kwani ina majukumu mengi ya kitaifa, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuchangia maafa hayo.

hapa umekosea kidogo ulitakiwa useme serikali ina majukumu mengi yasiyo na umuhimu wa kitaifa Kama vile kuilipa richmond.
 
Paparazi muwazi your cridibilty is getting worse as day goes on, hueleweki kaka umetumwa nini? Nani kamfunika mwenzake? PINDA yeye kachangisha KIASI gain?
 
Headline = UDAKU
Main Story = Looks like ok though i don't find Pinda in it!!
Amazing spin!
Duh!!!?
 
Hapa hakuna mantik! Ugetaka kueleweka ugesema Lwassa, Rostam Azizi na kampuni zao za kifisadi wapunguza deni lao la Richmond kwa kuchangia maafa mererani.
 
Mambo mperampera, unaposhindwa kujieleza ukafahamika unachokisema hapo ndipo tunasema wewe huwezi kumsafisha Lowasa na mafisadi wenzake, wewe kama hauna story ongelea hata majanga ya mvua hapa Tanzania.
 
Back
Top Bottom