Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Habari nilizipata hivi punde kutoka kwa jamaa yangu ambaye ni askari pale Arusha anasema kuwa hadi jana saa 2 asubuhi matokeo ya jimbo la Arusha Mjini yalikuwa tayari, lakini Batilda alikuwa anakataa kusaini akimwambia msimamizi anamsubiri Lowassa aje kwanza kwani kulikuwa kuna kasoro nyingi za kuhesabu.
Alimpigia simu Lowassa ambaye alifika hapa saa 5 na dakika 40 na kuingia ndani ya chumba cha kuhesabu kura huku akipigiwa saluti na askari.
Anasema Batilda na Lowassa walikuwa wanamshinikiza Lema apewe Sh 300 milioni ili atoke nje awaambie wafuasi wake kwamba ameshindwa.
Wawili hao walikuwa wanambana sana Lema akubali lakini yeye alikuwa anakataa ndiyo akampigia simu Mbowe na Ndesamburo wakaja pale na kufika takriban saa sita unusu hivi.
Huku nje vijana karibu 6,000 wa Chadema wako nje wakingojea matokeo. Hali ilikuwa mbaya sana na akina Mbowe wakawa adamant, wakasema NO. Iliposhindikana ndiyo matokeo yalitangazwa.
Hata hivyo RPC Basilio Matei aliingilia kati kwamba matokeo yatangazwe haraka ama sivyo ikiingia usiku kunaweza kuwa ghasia kubwa na askari wake hawawezi kumudu.
Hatimaye Batilda akanywea na matokeo yakatangazwa.
Habari zingine zinasema kwamba akina Mbowe watalipeleka mbele suala hili la Lowassa.