Lowasa alitamka jambo hadharani ndani ya NEC je ni neno lipi ?

Mkubwa Lunyungu Leo Umetushika Pabaya Na Kwakweli Sote Tunasubiri Hekima Yako. Niseme Tu Kuwa Tumesoma Mwana Halisi Jinsi Ra Alivyomzungumza Mkapa Kiasi Cha Kumfanya Muungwana Amuangalie Kwa Kile Kinachofasiriwa Na Mwanahalisi Ni Hasira Na Kutuhumiwa Kwa Matumizi Mabaya. Ninavyofahamu El Kamwe Hawezi Kum Praise Bwm Hadharani Tena Kwa Dhati Hivyo Ni Vema Hayo Utakayotuarifu Hapa Yabebe Uhalisi Wa Hoja Yako Na Kweli Zifanane Na El Kwa Haiba Yake Vinginevyo Jf Hapatakutosha Mkuu
 
Mkuu Lunyungu anahitaji kupewa mji ndo ataje alichosema EL, kwi kwi kwi
 
Mkubwa Lunyungu Leo Umetushika Pabaya Na Kwakweli Sote Tunasubiri Hekima Yako. Niseme Tu Kuwa Tumesoma Mwana Halisi Jinsi Ra Alivyomzungumza Mkapa Kiasi Cha Kumfanya Muungwana Amuangalie Kwa Kile Kinachofasiriwa Na Mwanahalisi Ni Hasira Na Kutuhumiwa Kwa Matumizi Mabaya. Ninavyofahamu El Kamwe Hawezi Kum Praise Bwm Hadharani Tena Kwa Dhati Hivyo Ni Vema Hayo Utakayotuarifu Hapa Yabebe Uhalisi Wa Hoja Yako Na Kweli Zifanane Na El Kwa Haiba Yake Vinginevyo Jf Hapatakutosha Mkuu
jamani eeeee naombeni site ya mwanahalisi.mi niliyonayo inafungua gazeti la may 21 jamani.nisaidieni wapendwa
 
jamani eeeee naombeni site ya mwanahalisi.mi niliyonayo inafungua gazeti la may 21 jamani.nisaidieni wapendwa

Ndugu yangu MTU KWAO, nilikuwa najaribu kutafuta web ya Mwanahalisi, kwenye google wanasema hawana web ila kuna blog za Tegambwage na Kubenea
 
Wakuu,
mnatuonjesha mambo then mnakata kona inakuwaje??? au ndio ile style ya mwalimu kujibu swali kwa kuwauliza wanafunzi wake mwenyewe kuwa nani anaweza kumjibu huyu??? Msibanie data hizo wekeni mambo hadharani nchi yetu wote lazima tumulike uchafu kabla haujavunda...
 
Linyungu na mimi sasa naaza kuamini kwamba huna kitu, kama watu wanasema lowassa hakusema kitu na wewe bado unasisitiza vinginevyo tuambie basi kasema nini.Vinginevyo kaa kimya unatupotezea muda wetu bure

Ni ushauri tuu[/QUOTE

Huyu Lyunyungu anakuwa drama queen??????
 
www.halihalisi.co.tz ila hawa wana tabia ya kuchelewa ku update news zao na pengine sidhani kama wako makini na wasomaji wao wa online.

Ziada, the same story imegusiwa hata Raia Mwema -Rostam almsifia sana Mkapa na kumsihi awapuuze wote wanaomsakama kwani walio wengi ni watu wasio na upeo maana wameshindwa hata kuuona mchango wake wa miaka 10 kama vile kuacha hazina ya kutosha BOT na mengi ya namna hiyo vilivyoiwezesha awamu ya 4 kusimama kwa nguvu, wanaendelea kusema hawa mabwana kuwa baada ya hapo wajumbe wachache walimpigia makofi ya pongezi na kufuatiwa na Makamba aliyewatetea wanaopokelewa kwa nderemo makwao baada ya kukumbwa na kashfa akidai huo ndio ukuaji wa chama na alizidi kumfagilia Benjamini. Hawakuishia hapa Raia Mwema,wansema JK alipoanza kuongea akamsifu sana Rostam huku akidai eti huyu ni mtu mnyenyekevu na mwenye akili sana humu ndani- wanasema alitamka kwa maana ya kumkejeli Rostam.

Nadhani yatupasa tusome magazeti huku tukijua kila mmoja ana agenda yake ila ni vema kusoma hata kama mnatofautiana ili kujipanua kimaono.
 
Kikwete ni ***** na ****** wanataka attention kwa kutumia NEWS MANIPULATION ya tetesi za VIFO na UCHAWI wenye kuleta WOGA!
CCM wameshaulizwa kuhusu pesa za EPA walizotumia kwenye ushindi wao wa TSUNAMI?
Ndio maana hapa huyu Absalom anaonyesha mwelekeo huru ambao kama watu watasikiliza then CCM wataigundua UMAFIOSO WAO!....

Samuel John Tegeza Sitta</STRONG>
Huyu ni mwanasiasa machachari. Kitaaluma ni mwanasheria na mtu ninayeweza kusema pasipo kusitasita, kuwa ameandika historia pekee tangu akiwa kiongozi wa juu wa Bunge.
Ni ukweli usiopingika kwamba katika kipindi cha miaka miwili na nusu tangu awe Spika, Sitta amefanikiwa kulijengea Bunge heshima ya pekee kutokana na namna alivyoweza kusimamia kwa umakini mkubwa baadhi ya masuala mazito.
Kwanza Sitta anaweza akatajwa kuwa ni Spika aliyesaidia sana kuliongezea meno na nguvu Bunge, akiliweka katika mstari sahihi wa kimaamuzi na kulijengea taswira ambayo haikupata kuwapo siku zilizopita.
Uzito wa maamuzi kama lile la kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza utata katika mkataba wa Richmond, ni ushahidi mmoja tu wa mafanikio ya Uspika wa Sitta, ambao kwa kiwango kikubwa yalimjengea heshima ya pekee ndani na nje ya Bunge.
Matokeo ya Kamati hiyo Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambayo ni pamoja na kulazimishwa kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wengine wawili - Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha - yamemfanya Sitta aonekane shujaa wa kipekee ndani ya Bunge.
Richmond, kwa upande mwingine, imemfanya Sitta aonekane na achukue sura ya kuwa mpambanaji dhidi ya vitendo vya kifisadi ndani ya chama chake na pengine serikalini. Huu ni ukweli unaopaswa kuheshimiwa.
Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba ushujaa huu wa Samuel Sitta umefikia hatua ya kumvimbisha kichwa hata kumfanya aanze kutembea kifua mbele na kujiona kuwa ni mtu asiyetaka kuguswa.
Leo hii ni kosa kubwa na baya kabisa kumgusa au kumkosoa Sitta.
Ushahidi wa maandishi unaonyesha bayana kuwa wanahabari waliopata kumgusa mwanasiasa huyo tangu alipojitwalia ushujaa katika Kashfa ya Richmond, wamejikuta wakipewa majina mabaya kabisa na wakati mwingine wakihusishwa na kundi la mafisadi.
Hivi karibuni, mwandishi mmoja wa habari wa &#8216;Tanzania Daima' Jumapili; Charles Mullinda, alifanya &#8216;kosa' - kwa kujua au kutojua, kwa makusudi au kwa bahati mbaya - akamgusa Sitta sehemu mbaya kwa kuandika makala moja dhidi yake.
Kwa namna ya ajabu kabisa, ukosoaji huo dhidi ya Sitta umechukua sura ya pekee. Wabunge na waandishi kadhaa wa habari wamesikika wakieleza namna Sitta alivyoshtushwa na makala hiyo hata kuiunganisha na kile alichopata kukielezea kuwa ni &#8216;siasa za majitaka'.
Kwa namna ile ile alivyopata kufanya wakati zilipoandikwa taarifa kuhusu tuhuma za kutumia - isivyofaa - fedha na mali nyingine za Bunge, Sitta amesikika safari hii chini chini akihusisha upinzani huo wa hoja dhidi yake na ajenda ya mafisadi kumchafua. Huu ni upuuzi.
Sitta, kwa sababu ya kile kinachoweza kuonekana kuwa ni jeuri inayotokana na matokeo ya vita dhidi ya ufisadi, amegeuka na kuwa mtu anayeweza kusema lolote baya dhidi ya watu wengine na akaaminika na hata kuonekana kuwa ni msema kweli. Hali hii lazima ifikie mwisho.
Hivi sasa kwa sababu ya &#8216;jeuri' hii, maofisa wa Bunge wanaomuona Sitta kuwa shujaa wao wa vita dhidi ya ufisadi ambayo &#8216;Tanzania Daima' ina kila sababu ya kutembea kifua mbele cha kupambana na tatizo hili kabla Spika huyo hajatiwa &#8216;wakfu wa ushujaa zama za Kamati ya Mwakyembe', wamefikia hatua ya kuwaogopesha wanahabari kutomgusa mkuu wao wa kazi
 
Last edited by a moderator:
Lowassa si alishasema mbele ya kikao chao cha KIMAFIA kuwa alimshauri TOP ******* KUWA RICHMOND NI UTAPELI?
Kwanini Kikwete hakusimamisha mkataba wa RICHMOND licha ya kwamba alikuwa anajua?
Kwanini hakusimamisha malipo HEWA ya EPA ambayo kutokana na wingi wake ni LAZIMA ALIKUWA NA TAARIFA?
KWANINI BALLALI HAKUWAHI KUTAJWA KAMA MTUHUMIWA LICHA YA KWAMBA ALIHUSIKA DIRECTLY NA HUKU AKIJIGAMBA NI PESA ZA IKULU?
Wapi hao wasaidizi wao ambao walisaini documents wakampelekea na yeye kusaini na kuwarudishia huku kukiwa na udhibitisho wa saini na barua kuwa serikali ilitaka pesa hizo ziltolewe KIMAFIA? Kina DEP,DDDD,DF, Director of Supervisions...HAWA MAFIA WANAWAACHA MAFIOSO MAFISADI WENZAO KWENYE KAZI ILI WAWAUWE WATU,KUWATISHA NA KUHARIBU USHAIDI!
JOHNSON MWANYIKA ambaye ni kinara wa UMAFIA wa RICHMOND NDIYE ALIYEWEKWA KUWACHUNGUZA WALIOHUSIKA NA EPA...Wanafikiri sisi ni wajinga kiasi hicho?
Wakamweka Zitto ndani ya KAPU LA UFISADI na sasa shombo EVERYWHERE!
JE TUTAFIKA?
 
Last edited by a moderator:
mkuu nimesoma hisia zako
inauma sana na ipo siku shetani atajiumbua mwenyewe very soooon
 
Lunyungu,
Sema tu mzee maana kwa kweli yaelekea hakuna mwenye data hizo. Tukupe mji?
 
mkuu nimesoma hisia zako
inauma sana na ipo siku shetani atajiumbua mwenyewe very soooon

Kikwete kama ni chakula anapika basi kishakuwa sumu kutokana na hiyo michanganyiko!

Sitta ni shujaa kwasababu alipigania kuwepo uchunguzi wa RICHMOND.
Johnson Mwanyika akawa ni mmoja wapo wa watuhumiwa wa RICHOMD...MKATABA AMBAO HATA LOWASSA ALISHAMWAMBIA YEYE NA MWANYIKA PAMOJA NA DON MAFIOSO TOP MWENYEWE KUWA NI MBOVU NA HAUFAI!

Kikwete akaona ataumbuka hivyo akamuweka Mwanyika kwenye kamati haraka haraka ya kuwachunguza mafisadi wengine ili sasa waje pamoja na kunegotiate namna ya kuua noma pande zote za EPA na RICHMOND...Na huku akimwambia LOWASSA KUWA BADO ANAWEZA KUJITETEA NA KUBAKI KAZINI...

Akageuka upande wa PILI akam TAP Zitto ambaye naye alikuwa akiwaumiza huko Bungeni....Wakamweka kapu moja na MAFISADI kwenye kamati ya MADINI.

Walichozungumza humo ndani ya kamati anayejua ni MKUU MAFIOSO NA SINCLAIR pamoja na Hao kina ZITTO na wanakamati wengine.

Sasa wakaanza kuwazuga wananchi kuwa tusubiri BUNGE likianza kwani watayazungumzia yale ambayo wananchi wanayoyapigia kelele kuwa SASA MAFIA WAWEKWE NDANI...

Kumbe Mafioso ni WOTE na sasa woga ni UCHAWI BUNGENI NA HAKUNA ANAYETAKA KUKAA BUNGENI NA KUJADILI ISSUES ZA WANANCHI.
Baada a kurudi BUNGENI...

Wameanza upya eti wanazungumzia mambo ya ufisadi na namna rasimali za Taifa zitakavyoendelea kutumika ili kuwanufaisha wananchi!?

KUNA MWANANCHI ASIYEJUA KUWA MAFIOSO NI CCM NA SERIKALI YAKE NA KWAMBA HAWAWEZI KUJIKAMATA AMA KUJICHUNGUZA?

Kuna asiyejua kuwa hata wale tunaowaona kama ni wakombozi wetu bado wana maswali ya kutujibu?
 
Ndugu zangu sera za CCM nyingine ni nzuri tu...Ila MAFIOSO WAMEKITEKA CHAMA NA KINAKWENDA NA MAJI....
Ona sera ya madini waliyoinadi mwaka wa uchaguzi wa 2005!
Iko safi tu tena yenye kuonyesha kuwajali wananchi...SASA HIYO KAMATI YA MAPENDEKEZO YA MADINI ILIKUWA YA NINI?
NANI ASIYEKUMBUKA KUWA KAMATI YA MADINI ILITAKIWA KUFANYA KAZI YA UCHUNGUZI NA WATU KUWEKWA NDANI?
NI MAPENDEKEZA GANI CCM NA WAKONGWE HAO MAFIOSO MAFISADI WASIOYAJUA KUANZIA RIPOTI ZOTE ZA KINA WARIOBA NA MITUME MINGINE KIBAO JUU YA MITUME?

CCM Kuongeza kiwango cha MadiniBy Mike Mushi | Published 11/26/2005 | Habari Mpya |
CCM Kuongeza kiwango cha Madini


shein-2005-52.jpg

Chama Cha Mapinduzi kinakusudia kuongeza kiwango cha thamani ya madini kutoka asilimia 0.3 ya hivi sasa hadi kufikia asilimia 3 iwapo chama hicho kitashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk Ali Mohamed Shein amesema pamoja na kuongeza viwango vya madini hayo pia serikali ijayo itahakikisha inatengeneza vito vya madini hapa hapa nchini ili kuweza kuuza madini kwa tija.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Londoni wilayani Manyoni.

Amesema suala la madini limepewa kipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005-2010 kutokana na ukweli kwamba sekta ya madini inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua uchumi wa nchi.

Amewaambia wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa ili kufanikisha azma hiyo serikali itatoa mikopo na elimu kwa wachimbaji wadogo wadogo kwa njia ya semina na mikutano ili waweze kujua namna ya kuchimba madini hayo kitalaam.

&#65533;Baada ya kupewa mikopo, mpewe elimu kwa njia ya semina, mikutano au warsha mjue namna ya kuchimba madini hayo kitalaam&#65533;. Aliwaeleza wananchi hao ambao wengi wao ni wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu katika eneo hilo.

Dk. Shein amethibitisha kuwa serikali ya awamu ya nne itaendelea kukaribisha wawekezaji wakubwa katika sekta ya madini na pia itaangalia upya sera yake ya madini ili iweze kuwanufaisha wadau wote.

Amesisitiza wananchi wakichague Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndio chama pekee kinachoonyesha jitihada za kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kuweza kupambana na umasikini hali ambayo hatmae itawafanya kuwa na maisha bora.

Katika hatua nyingine Mgombea Mwenza huyo amewataka wachimbaji wadogo wa madini nchini kutumia fedha wanazozipata kwa kujijenga kimaisha kwa kuwa na nyumba bora, kutunza afya zao na kusomesha watoto na sio kwa anasa.

&#65533;Fedha ni fedheha, zikiwa nyingi zinachanganya kidogo hujui utazifanyia nini, unaishia sehemu ukiulizwa wewe nani na wewe unauliza pia wewe nani. Huo si utumiaji mzuri wa fedha&#65533;. Alisema Dk Shein

&#65533;Hata hivyo starehe zikizidi inachangia maambukizi ya ukimwi hilo nalo ni tatizo tukitambua ukimwi sasa ni janga la kitaifa. Hivyo hamna budi kuwa waangalifu na matumizi ya fedha&#65533;. Aliongeza.
 
Jmushi samahani kama ntakukwaza ila tunaelimishana tu, kama inawezekana jaribu kua short and straight to the point, maana unaandika maneno mengi hata kuyasoma inakua inatia uvivu japo you have a lot of points, samahani lakini
 
jmushi Samahani Kama Ntakukwaza Ila Tunaelimishana Tu, Kama Inawezekana Jaribu Kua Short And Straight To The Point, Maana Unaandika Maneno Mengi Hata Kuyasoma Inakua Inatia Uvivu Japo You Have A Lot Of Points, Samahani Lakini

Press Fast Forward!
 
Kamanda Lunyungu huna dataz... Pengine dataz ulizonazo hadi sasa ni idadi ya Tigo ulizonunua...
 
Kamanda Lunyungu huna dataz... Pengine dataz ulizonazo hadi sasa ni idadi ya Tigo ulizonunua...

Kamanda Kibunango uwe unajaribu kuchangia mara moha badala ya kupita kutafuta vijineno .Maneno aliyo yasema Lowasa ni mazito nayamepelekea CCM kuanza wenyewe kwa nguvu ya Mwenyekiti wao kuongeza kasi ya kuwa safisha Lowasa na kundi lake .Chenge kwenye hili kundi yeye bado hayumo.Sasa tulia mimi nitapasua japokuwa kuna mahala kuna mtu amesha sema .natafuta mbunge wa pili ambaye ataweza kutoa the same statement maana haya hayatoki mtaani .So sitaki kuwa kituko japokuw akuna mtu kesha sema lakini nafanya lile nadhani ni sahihi .

Wakati unanojea Kibunango jenga hoja tafadhali badala ya vijineno .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom