Lori ya mafuta lateketea kwa moto, laziba barabara kutoka Kongowe kuelekea Kigamboni

Jindal Singh

JF-Expert Member
Sep 9, 2015
1,853
1,521
Lori ya mafuta jioni hii imeteketea kwa moto na kusababisha kuziba barabara kutoka kongowe kuelekea Kigamboni kufungwa kwa masaa 4. Lori la mafuta aina ya Scania limeanguka katika maeneo ya Mwembe mtengu baada ya dereva wa lori hilo kukwepa bajaji iliyoingia ghafla barabarani ikitokea mtaani.

Licha ya wasamalia wema kufanya mawasiliano na vitengo vinavyohusika na uzimaji moto lakini mpaka saa 2.00 usiku hakuna chombo chochote cha uzimaji moto kilichofika licha ya kuwepo jeshi la polisi.
20160621_174413.jpg
20160621_174521.jpg
20160621_175101.jpg
20160621_175258.jpg
20160621_193534.jpg
20160621_180556.jpg
20160621_175959.jpg
 
hivi ile hela ya fire tunayolipa wakati wa kukata motor vehicle license kazi yake ni nini?au msingi wa kukatwa ile pesa ni nini?
 
hivi ile hela ya fire tunayolipa wakati wa kukata motor vehicle license kazi yake ni nini?au msingi wa kukatwa ile pesa ni nini?
Hilo swali hata mimi nilishajiuliza kwa nini ile pesa iwe lazima kuilipia while wakati yanapotokea majanga kama hayo hizo gari za zimamoto hazitoi ushirikiano wowote.
 
Back
Top Bottom