London Terror Attacks: 6 people killed 20 Injured

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Police are responding to reports that a van has hit a number of pedestrians on London Bridge in central London.

Witnesses have said that armed officers are understood to be at the scene after a white van mounted the pavement before driving into people. The Metropolitan Police say they are dealing with an incident on the bridge.

Transport for London said the bridge has been closed in both directions due to a "major police incident". Bus routes were being diverted.

BBC reporter Holly Jones, who was on the bridge at the time of the incident, said the van was driven by a man and was "probably travelling at about 50 miles an hour".

About five people were being treated for injuries after the vehicle mounted the pavement and hit them, she said.

She said the van, which was travelling from the direction of central London, headed towards the south side of the river.

Ms Jones later reported seeing a man being arrested by police. She said he was handcuffed and had his shirt off.

SOURCE: BBC
--------

>>Kwa Kiswahili

Washambuliaji watatu, ambao walikuwa wamevalia mikanda ya bandia ya miripuko , pia walipigwa risasi na polisi na wamefariki, polisi ya mjini London imesema.

39110450_404.jpg

Majeruhi wakipelekwa hospitali baada ya tukio la kigaidi
mjini London

"Katika wakati huu, tunaamini kwamba watu sita wameuwawa pamoja na washambuliaji watatu waliopigwa risasi na polisi," amesema kamishna msaidizi Mark Rowley , ambae pia ni mkuu wa kitengo cha kupambana na ugaidi.

Washukiwa waliwagonga wapita njia katika daraja la London kabla ya kuwashambulia watu katika baa za karibu na migahawa, Rowley alisema. Polisi wenye silaha waliwapiga risasi washambuliaji watatu katika muda wa dakika nane baada ya polisi kupokea siku ya kwanza ya kuhusiana na mashambulio hayo ya kigaidi katikati ya London usiku wa Jumamosi, amesema.

Simu ya kwanza ilipokelewa baada ya washambuliaji kuendesha gari yao na kuwagonga wapita njia katika daraja la London kabla ya kuwachoma visu watu katika soko la karibu la Borough, Rowley amesema.

39110508_404.jpg

Polisi wakilinda usalama katika eneo la tukio la kigaidi
mjini London

Watu walioshuhudia waliliambia gazeti la Guardian waliwaona watu wawili wakiwachoma visu watu nje ya mgahawa maarufu wa Roast katika soko la Borough. "Niliwaona watu wawili wakiwa na visu vikubwa nje ya mgahawa huo wa Roast," mpishi kutoka katika mgahawa wa karibu aliliambia gazeti hilo.

Polisi wachukua hatua ya haraka

Walikuwa wakiwachoma visu watu , tulikuwa tunapiga kelele "acha, acha" na watu walikuwa wakiwatupia viti," mpishi huyo alisema. "polisi walikuja na kuwapiga risasi watu hao moja kwa moja."

39110373_404.jpg

Watu ambao walipata mshituko baada ya tukio la kigaidi
mjini London

Waziri mkuu Theresa May aliliita shambulio hilo kuwa "tukio la kigaidi" na alieleza "shukrani zake nyingi" kwa polisi na huduma za dharura. Meya wa London Sadiq Khan amesema anapanga kuhudhuria mkutano mapema leo Jumapili (04.06.2017) wa kamati ya dharura ya serikali inayojulikana kama cobra, ambayo inatarajiwa kuongozwa na waziri mkuu May.

"Mpaka sasa hatufahamu maelezo zaidi, lakini hili lilikuwa shambulio la makusudi na la waoga dhidi ya wakaazi wa London ambao hawana hatia na watu wanaotembelea mji wetu wakifurahia usiku wao wa Jumamosi," Khan alisema.

Trump azungumza na May

Rais donald Trump amempigia simu waziri mkuu wa Uingereza Theresa May na kumpa rambi brambi zake kufuatia tukio la kigaidi mjini London.

39110274_404.jpg

Watu wakikimbia kutoka eneo la tukio mjini London

Rais Trump alizungumza na waziri mkuu May leo na alitoa rambi rambi zake kwa shambulio hilo la kinyama la kigaidi katikati ya London.Trump aliahidi msaada kwa Uingereza kutokana na mashambulio hayo mawili ya kigaidi ambapo watu sita waliuwawa, baada ya gari kuwagonga wapita njia na washambuliaji hao kuwachoma visu watu kadha.

Katika mazungumzo yao ya simu Trump aliahidi kwamba Marekani itatoa ushirikiano kamili kwa Uingereza katika uchunguzi wa tukio hilo na kuwafikisha watu wanaohusika na tukio hilo la kiuwoga mbele ya sheria.

39110597_404.jpg

Waziri mkuu wa Canada Justin Trudeau

Waziri mkuu wa Canada Justin Trudeau amesema kwamba wacanada , "wanasimama pamoja na Waingereza" baada ya washambuliaji kuwachoma visu holela watu na kuwagonga wapita njia kwa gari na kuuwa watu sita.
 
Source from the ground at London Bridge
Van veered off road and hit about five to six people..
 
UK soft targets ni nyingi mno.

Faala kama huyo aliyekuwa anaendesha van ingekuwa ni US hususan kwenye southern states angekuwa keshakula shaba!

UK polisi wengi hata hawabebi silaha....sijui hata ni kwa nini.
 
Police are responding to reports that a van has hit a number of pedestrians on London Bridge in central London.
Witnesses have said that armed officers are understood to be at the scene after a white van mounted the pavement before driving into people.
The Metropolitan Police say they are dealing with an incident on the bridge.
Transport for London said the bridge has been closed in both directions due to a "major police incident". Bus routes were being diverted.
BBC reporter Holly Jones, who was on the bridge at the time of the incident, said the van was driven by a man and was "probably travelling at about 50 miles an hour".
About five people were being treated for injuries after the vehicle mounted the pavement and hit them, she said.
She said the van, which was travelling from the direction of central London, headed towards the south side of the river.
Ms Jones later reported seeing a man being arrested by police. She said he was handcuffed and had his shirt off.

SOURCE: BBC
Mhhhh......
 
Duh

Risasi nazo, tusubirie kujua zaidi

Maeneo hayo kwa matanuzi pia lazima watu wanasepa, walio njiani wanageuza kurudi makwao.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom