mr vata
JF-Expert Member
- Jan 30, 2017
- 462
- 605
Afrika tunakosea wapi? Mbona tunapenda kutumia nguvu kwa kila jambo? Unamchapa viboko na kumdhalilisha baba ambae yupo na familia yake.
Mbona ulaya sijaona wakipigana mitaani kwa kisa kama hiki. Muhimu ni kuangalia nini chanzo cha watu kuendelea kutoka licha ya marufuku iliyotolewa. Hali ya uchumi ni mbaya mtu hawezi vumilia kukaa ndani na njaa yake.
Wengine wamefika mbali zaidi na kuwatandika raia risasi. Huu ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Unampiga mtu risasi kisa katoka nje au katumia usafiri wa uma. Kama angekua jambazi au muuaji ungempa adhabu gani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona ulaya sijaona wakipigana mitaani kwa kisa kama hiki. Muhimu ni kuangalia nini chanzo cha watu kuendelea kutoka licha ya marufuku iliyotolewa. Hali ya uchumi ni mbaya mtu hawezi vumilia kukaa ndani na njaa yake.
Wengine wamefika mbali zaidi na kuwatandika raia risasi. Huu ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Unampiga mtu risasi kisa katoka nje au katumia usafiri wa uma. Kama angekua jambazi au muuaji ungempa adhabu gani?
Sent using Jamii Forums mobile app