Elections 2010 Liwa Ule: CCM yalipisha wagombea Sh 1m kila mmoja

Buyaka

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
1,643
1,786
Lusinde ashitushwa wagombea udiwani kulipa Sh1m

Friday, 20 August 2010 08:55
Habel Chidawali, Dodoma
Mwananchi

BALOZI mstaafu Job Lusinde amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoa ufafanuzi wa kina juu ya kiwango cha Sh1.milioni, kinachotakiwa kutolewa na wagombea wa viti vya udiwani, ili kuchangia kampeni.

Wagombea udiwani katika Wilaya ya Dodoma, wamekuwa wakihaha kutafuta Sh1 milioni, kila mmoja ambazo zimeelezwa kwa kuwa ni mchango wa lazima.

Balozi Lusinde ambaye alikwenda katika ofisi za CCM za wilaya ya Dodoma mjini ili kupata ufafanuzi, alisema tayari jambo hilo limeanza kutafisiriwa vibaya na baadhi ya wagombea ambao sasa wanajutia kuomba nafasi hizo.

Mkongwe huyo wa siasa, aliingia katika ofisi hizo jana asubuhi kupokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wanachama wa CCM walioteuliwa kugombea udiwani katika kata za Wilaya ya Dodoma.

"Jambo hili linatia mashaka sana ndugu katibu, lazima muliangalie kwa sababu watu hao wamepitishwa na wanachama kwa kuzingatia uwezo wao katika kuongoza, lakini si matarajiri, sasa mnapowataka watoe Sh1 milioni, watazipata wapi," alihoji Balozi Lusinde.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Dodoma, David Mzuri, alisema hatua ya kuwataka wagombea kutoa kiwango hicho, inafuatia maelekezo ya CCM mkoa yaliyomtaka kila mgombea ,kutoa kiasi hicho kama mchango wake katika kampeni.

Mzuri alisema kila aliyepita kwake kuchukua fomu ya uteuzi aliaambiwa kutoa kiwango hicho.Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa kiasi hicho ni kiwango cha juu cha mgombea udiwani kutumia katika kampeni zake lakini si kiwango kamili anachotakiwa kuwa nacho.
Bajeti ya serikali inayumba, wizara na taasisi nyingi zinalalamika hazina hela, lakini hata siku moja sijasikia CCM inalalamikia bajeti yao. Huyo accountant anaewabunia miradi ya chama lazima umkubali kwa usanii
 
Hakika, Ninakwambia sijui kuna nini huko CCM maana ukimuuliza kila aliegombea CCM kuanzia ngazi ya udiwani kiwango cha chini alichochangishwa 400000/= kwa diwani na kwa wabunge ni 1500000/= eti kukisaidia chama gharama za uchaguzi na zote hizo zilikuwa zinatolewa kwa makatibu wa CCM wa kila wilaya cha ajabu ni kuwa je hela za ruzuku za CCM huwa zinatumikaje? au zote zinatumika makao makuu tu au hupelekwa wilayani bali wmakatibu wa CCM wilaya huamua watakavyo ili nao wavune! Ninakwambia baada y madiwani kupitishwa na CCM tayari baadhi ya makatibu wa CCM wa wilaya waliwaita(Wilaya tunayo) kuwa kila mgombea udiwani wa CCM aliyepitishwa alitakiwa kuandaa BAJEI ISIYOZIDI MILIONO KUMI NA HALAFU WATAFUTE HIYO FEDHA WENYEWE!!

HII ni kinyume kabisa na sheria ya mwak 2010(election expenses) N0 6.

(expenses for nomination process) say "14.(1) All expenses to be incurred during the nomination process withini the political parties shall be borne out by a political party concerned "

Je kwa mtindo huu wa CCM kutaka wagombea wake wajitolee fedha MASIKININI ATAPATA UONGOZI NDANI YA CCM?

AMA KWELI KAMA ASEMAVYO SHIBUDA- TANZANIA BILA MALARIA INAWEZEKANA LAKINI CCM BILA RUSHWA 'NA BILA KUCHANGISHA' MATAJIRI HAIWEZEKANA!
 
Back
Top Bottom