VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Ulipojitokeza na kuanza kujibu kuhusu Waraka wa akina Makamba na sauti zilizovuja za viongozi mbalimbali waandamizi chamani na Serikalini, nikajua kuwa mbio zako ni fupi tu. Ni mara bada ya kumtaja na kumpania Benard Membe. Ukasema ukirudi toka nje ya nchi, utakuja kumkuna Membe panapomuwasha.
Ukaenda, ukarudi. Ukabaki kimya. Ni kwakuwa ulijua kuwa uligusa sehemu mbaya. Membe, ndani ya chama na Serikali, si mtu wa mchezo. Anasikilizwa; anapendwa; anafuatiliwa; anazingatiwa; anasomwa na kusikika. Si wa kupuuzwa hata kidogo. Ni vyema uliona mbali na kuamua kuwa kimya.
Membe ni zaidi ya Karandinga uliloliangusha Mtera. Ni zaidi ya 'aliyekutuma' kujibu Waraka na sauti za viongozi. Uligusa pabaya. Kwakuwa wewe ni mjanja na unajua namna ya kutunza ugali wako, ukabaki kimya badala ya kujichanganya kwa Membe. Hata waliokushangilia wangekuacha solemba.
Ropoka kwa stepu, Membe ni mtu mzito!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Urambo, Tabora)
Ukaenda, ukarudi. Ukabaki kimya. Ni kwakuwa ulijua kuwa uligusa sehemu mbaya. Membe, ndani ya chama na Serikali, si mtu wa mchezo. Anasikilizwa; anapendwa; anafuatiliwa; anazingatiwa; anasomwa na kusikika. Si wa kupuuzwa hata kidogo. Ni vyema uliona mbali na kuamua kuwa kimya.
Membe ni zaidi ya Karandinga uliloliangusha Mtera. Ni zaidi ya 'aliyekutuma' kujibu Waraka na sauti za viongozi. Uligusa pabaya. Kwakuwa wewe ni mjanja na unajua namna ya kutunza ugali wako, ukabaki kimya badala ya kujichanganya kwa Membe. Hata waliokushangilia wangekuacha solemba.
Ropoka kwa stepu, Membe ni mtu mzito!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Urambo, Tabora)