Livingstone Lusinde (Kibajaji) adakwa live na TAKUKURU nyumbani kwake akigawa rushwa kwa wajumbe wa CCM

Wiston Mogha

Senior Member
Feb 13, 2014
149
96

IMG_2198.JPG
Mapema leo TAREHE 7/07/2020 ,majira ya mchana kupitia kwa wananchi wa samaria jimbo la Mtera,Livingstone Lusinde amekamatwa na Takukuru na kuwekwa chini ya ulinzi pamoja na kusitisha mkutano wake na wajumbe wa ccm, baada ya taarifa rasmi za uhakika kutoka wananchi kuwa imekuwa ni kawaida yake kuwaita wapiga kura wake na kuandaa chakula kisha baadae kuwapatia pesa kila ifikapo kipindi hiki cha uchaguzi.

Hivyo basi kwa taarifa rasmi kesho amehitajika mapema kwa ajili ya maelezo zaidi na kusaidia na chombo hicho cha Takukuru,na hili tukio limefuata baada ya siku si nyingi kuandaa tukio kanisani na kuwaita wajumbe kwa kisingizio kuwa ni ibada ya shukrani.

Sambamba na hilo kwa muda mrefu wananchi wamekuwa wakikwazwa na kebehi,dharau na fedheha kutoka kwa Mbunge wao akidai ya kuwa mpinzani wake hajazaliwa, vile vile akijinasibu ya kuwa anafahamu atapita kwa fedha kwakuwa wagogo ni ombaomba na masikini, na mwishowe huwa anawapa ubwabwa kisha wagogo wanamchagua hivyo hata angekuja Kassim Majaliwa kugombea nae asingefua dafu kwake.

Vile vile amekuwa Mbungewa visasi na mara kadhaa akipishana na kiongozi yoyote aliye chini yake atamfanyia figisu na wakati mwingine kumuamisha kabisa au kumtoa kabisa kwenye nafasi yake,sambamba na hilo ni kiongozi anayetumia mabavu na lugha chafu hata kwa wapiga kura wake na kwa sasa jamii na wananchi wimbo wao ni mabadiliko hali inayopelekea Mbunge huyo kutumia nguvu Nyingi za ziada ikiwemo rushwa tena hadharani.

 
Hata angewatukana vipi sitoshangaa akipita maana "michango yake bungeni ni ya maana sana!!!" na ni miongoni mwa wabunge wanaosifiwa sana kwa utendaji wao kwenye majimbo yao. Ndio fisiemu wa mfano huyo yeye msukusu na yule mdogo wao kayaman.

Maendeleo hayana chama.
 
Bwana yule anaweza kuingilia kati na kumnusuru, maana hawa ndio watu anaowahitaji kule Mjengoni unless wameamua kumshughulikia sasa.

Hizi issue/kesi zote hizi mwisho wa siku zinaweza kuisha tu bila kueleweka zimeishaje.

Anyway,huu ni utamaduni wao wa miaka mingi kama ule wa kutom-challenge Mkulu alieko madarakani pale anapotafuta kipindi chake cha pili cha kuendelea kukaa ofisini.
 
Huu ni utamaduni wa CCM.

Mtindo huu aliufanya sana Nyalandu, alikuwa anawakusanya wajumbe wa jimbo zima pale Mwenge Sekondari na kuandaa tafrija, baada ya watu kushiba chakula linafuatia zoezi la kuwagawia elfu kumi kumi.

Bi Mkubwa alilamba elfu 10 mwaka 2010, aliporudi home akawa anasema hamna mtu wa kumuangusha Nyalandu kisa ana hela nyingi za kuwahonga wajumbe wa kura za maoni.

Ebu tuone akiwa upande wa pili kama atatumia mbinu gani.
 
Huu ni utamaduni wa CCM.

Mtindo huu aliufanya sana Nyalandu, alikuwa anawakusanya wajumbe wa jimbo zima pale Mwenge Sekondari na kuandaa tafrija, baada ya watu kushiba chakula linafuatia zoezi la kuwagawia elfu kumi kumi.

Bi Mkubwa alilamba elfu 10 mwaka 2010, aliporudi home akawa anasema hamna mtu wa kumuangusha Nyalandu kisa ana hela nyingi za kuwahonga wajumbe wa kura za maoni.

Ebu tuone akiwa upande wa pili kama atatumia mbinu gani...
Aliyekamatwa ni kibajaji ndivyo mada isemavyo je atachukuliwa hatua gani?
Au ni takrima za kawaida?
 
Hata angewatukana vipi sitoshangaa akipita maana "michango yake bungeni ni ya maana sana!!!" na ni miongoni mwa wabunge wanaosifiwa sana kwa utendaji wao kwenye majimbo yao!!! Ndio fisiemu wa mfano huyo yeye msukusu na yule mdogo wao kayaman
Maendeleo hayana chama...

Jimboni kwake kafanya nini?
 
Back
Top Bottom