Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 4,953
- 4,326
Huyu mtu ana akili nyingi sana na ni mzalendo wa dhati mwenye maono mazito juu ya nchi yake. Ni nadra sana kuwa na watu wa aina hii. Tatizo letu watanzania ni kushindwa kuwatumia vizuri watu wa aina hii kwa maendeleo ya taifa letu.
Tangia awe mbunge zaidi ya miaka 10 mfululizo, michango yake bungeni mara zote huwa zilizoshiba na akianza kuchangia bunge zima na nchi nzima husisimuka.
Kutokuwa na cheti cha degree isiwe hoja kwani alichonacho kichwani wengi wa hao wenye vyeti vya madigrii hawanacho vichwani mwao. The man is a real genious. Hakupata fursa ya kuendelea kupata formal education kwa sababu ya ufukara wa kutupwa waliokuwa nao wazazi wake.
Jamii yake ya wagogo ilitambua uwezo wake mkubwa wa akili na wakaamua kumubwaga Malecela aliyekuwa waziri mkuu kwenye ubunge wa jimbo la Mvumi na kumpatia Lusinde. Hapo ndipo jina la Kibajaji lilipatikana kwani tela lilikuwa ni Malecela lakini likapinduliwa na kibajaji.
UDOM, Chuo kikuu kilichoko mkoani kwake sijui ni kwa nini kimeshindwa kutambua akili ya mtu huyu na kumtunukia PhD ya heshima? Watu wa aina hii ndiyo wanaofaa kuongoza wizara zile ngumu zilizowashinda wengi kama ile ya nishati ambayo ilimshinda Lowasa hadi akaachia uwaziri mkuu, akaja Prof Muhongo akavurunda, akaja Ngereja fedha za escrow account zikamuzoa etc.
Wizara nyingine iliyokuwa ngumu ilikuwa ni ya ardhi na makazi. Nayo iliwashinda wengi hadi ilipompata William Lukuvi ambaye naye background yake ni kama ya Kibajaji kwani alitokea kwenye cheti cha ualimu wa primary school hadi kutunukiwa Master degree in political science and economics na Open University of Tanzania (OUT).
Hawa watu ni genious na inafaa tukawatumia vizuri. Michango yao ya mawazo haipaswi tu kuishia bungeni bali inapaswa kufika hadi kwenye Cabinet ambako ndiko kwenye maamuzi ya utekelezaji.
Wizara nyingine ya muhimu sana ambayo imekuwa ngumu kupata mkunaji mwenye uwezo ni wizara ya kilimo. Bashe alijipambanua kupitia michango yake bungeni iliyoshiba kuhusiana na kilimo kama ambavyo Kibajaji amekuwa akijipambanua bungeni. Kwa kuwa Bashe hivyo vyeti vya digrii anavyo, haikumchukua miaka mingi sana kupewa wizara hiyo na leo kila mtu anakubali kuwa wizara ya kilimo imepata mkunaji anayefaa sana.
Angalia leo mchango wake wa namna ya kukabiliana na athari za madhara yatokanayo na majanga kama ya vita ya Russia vs Ukraine, Covid 19 na mengineyo:
Tangia awe mbunge zaidi ya miaka 10 mfululizo, michango yake bungeni mara zote huwa zilizoshiba na akianza kuchangia bunge zima na nchi nzima husisimuka.
Kutokuwa na cheti cha degree isiwe hoja kwani alichonacho kichwani wengi wa hao wenye vyeti vya madigrii hawanacho vichwani mwao. The man is a real genious. Hakupata fursa ya kuendelea kupata formal education kwa sababu ya ufukara wa kutupwa waliokuwa nao wazazi wake.
Jamii yake ya wagogo ilitambua uwezo wake mkubwa wa akili na wakaamua kumubwaga Malecela aliyekuwa waziri mkuu kwenye ubunge wa jimbo la Mvumi na kumpatia Lusinde. Hapo ndipo jina la Kibajaji lilipatikana kwani tela lilikuwa ni Malecela lakini likapinduliwa na kibajaji.
UDOM, Chuo kikuu kilichoko mkoani kwake sijui ni kwa nini kimeshindwa kutambua akili ya mtu huyu na kumtunukia PhD ya heshima? Watu wa aina hii ndiyo wanaofaa kuongoza wizara zile ngumu zilizowashinda wengi kama ile ya nishati ambayo ilimshinda Lowasa hadi akaachia uwaziri mkuu, akaja Prof Muhongo akavurunda, akaja Ngereja fedha za escrow account zikamuzoa etc.
Wizara nyingine iliyokuwa ngumu ilikuwa ni ya ardhi na makazi. Nayo iliwashinda wengi hadi ilipompata William Lukuvi ambaye naye background yake ni kama ya Kibajaji kwani alitokea kwenye cheti cha ualimu wa primary school hadi kutunukiwa Master degree in political science and economics na Open University of Tanzania (OUT).
Hawa watu ni genious na inafaa tukawatumia vizuri. Michango yao ya mawazo haipaswi tu kuishia bungeni bali inapaswa kufika hadi kwenye Cabinet ambako ndiko kwenye maamuzi ya utekelezaji.
Wizara nyingine ya muhimu sana ambayo imekuwa ngumu kupata mkunaji mwenye uwezo ni wizara ya kilimo. Bashe alijipambanua kupitia michango yake bungeni iliyoshiba kuhusiana na kilimo kama ambavyo Kibajaji amekuwa akijipambanua bungeni. Kwa kuwa Bashe hivyo vyeti vya digrii anavyo, haikumchukua miaka mingi sana kupewa wizara hiyo na leo kila mtu anakubali kuwa wizara ya kilimo imepata mkunaji anayefaa sana.
Angalia leo mchango wake wa namna ya kukabiliana na athari za madhara yatokanayo na majanga kama ya vita ya Russia vs Ukraine, Covid 19 na mengineyo: