LIVE:Zitto,Lissu,Mdee Kuunguruma Geita Leo

WABHEJASANA

JF-Expert Member
Jun 22, 2011
4,225
869
Wanabodi,
Nimefika Kwenye mji wa Geita majira ya saa 2:40 mchana huu,kuna shmrashamra kila kona ya mji huu kufuatia ugeni wa makamanda wa CHADEMA Zitto Kabwe,Halima Mdee,na Tundu Lissu kudaiwa kuingia katika mji huu kuanzia majira ya saa 10 jioni kwenye viwanja vya Magereza mjini hapa.

Taarifa nilizozipata pia kupitia gari ya matangazo linalozunguka mjini hapa kuna taarifa pia kwamba pamoja na hao niliowataja,lakini pia kamanda Lema inaelezwa kwamba akawepo pamoja na wengine wengi kwa jili ya kuwasha moto katika mji wa Geita.

Ukweli usiopingika ni kwamba katika mji huu CDM inakubalika kwa asilimia 80 na watu wanaipenda vibaya mno kwa sababu mara kadhaa nimehudhuria mikutano ya CDM hapa mjini imekua ikitisha kwelikweli,na hkuna wananchi wanaosombwa kutolewa maeneo mengine ila wamekuwa wanajipeleka wao wenyewe,na kibaya zaidi CDM wamekuwa wakinyiwa viwanja vya karibu na mji ukiwelo ule a kalangalala,na sokoni na kupewa ule wa magereza ulioko mbali na mji lakini wanaume wamekuwa wakitembea na kujaa kwenye mkutano.

Panapo majliwa natarajiwa kuwajuza kila kitakachokuwa kinaendelea,lakini kwa sasa ngoja nipitepite kwenye kona za mji huu kuangalia baada ya mkutano nitajimuvuzisha vipi,Bujibuji,watu8,na wengineo jamani nipeni ramani ya mji ili huu ambao naona umejaa visholi vya kila aina nisije nikajikuta nakombwa kila kitu kama "Bujibuji" Juzi.
 
Wanabodi,
Nimefika Kwenye mji wa Geita majira ya saa 2:40 mchana huu,kuna shmrashamra kila kona ya mji huu kufuatia ugeni wa makamanda wa CHADEMA Zitto Kabwe,Halima Mdee,na Tundu Lissu kudaiwa kuingia katika mji huu kuanzia majira ya saa 10 jioni kwenye viwanja vya Magereza mjini hapa.

Taarifa nilizozipata pia kupitia gari ya matangazo linalozunguka mjini hapa kuna taarifa pia kwamba pamoja na hao niliowataja,lakini pia kamanda Lema inaelezwa kwamba akawepo pamoja na wengine wengi kwa jili ya kuwasha moto katika mji wa Geita.

Ukweli usiopingika ni kwamba katika mji huu CDM inakubalika kwa asilimia 80 na watu wanaipenda vibaya mno kwa sababu mara kadhaa nimehudhuria mikutano ya CDM hapa mjini imekua ikitisha kwelikweli,na hkuna wananchi wanaosombwa kutolewa maeneo mengine ila wamekuwa wanajipeleka wao wenyewe,na kibaya zaidi CDM wamekuwa wakinyiwa viwanja vya karibu na mji ukiwelo ule a kalangalala,na sokoni na kupewa ule wa magereza ulioko mbali na mji lakini wanaume wamekuwa wakitembea na kujaa kwenye mkutano.

Panapo majliwa natarajiwa kuwajuza kila kitakachokuwa kinaendelea,lakini kwa sasa ngoja nipitepite kwenye kona za mji huu kuangalia baada ya mkutano nitajimuvuzisha vipi,Bujibuji,watu8,na wengineo jamani nipeni ramani ya mji ili huu ambao naona umejaa visholi vya kila aina nisije nikajikuta nakombwa kila kitu kama "Bujibuji" Juzi.

Chezea VIROBA+JUA LA SAA 8 wewe...! vikikata kichwani kunywa maji mengi sana halafu uoge maji ya baridi.
 

Mkuu samahani sana mashine ya kazi ilileta matatizo sana hadi nikachanganyikiwa kiukweli!

hata hivyo mkutano umefanyika lakini viongozi niliowataja hawakuja kwenye mkutano huo baada ya kuelezwa kwamba walipata udhuru.

Isipokuwa aliendesha Mkutano huo ni Kamanda wa Jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje ambaye amesema Kamanda Lema amepatwa na Msiba lakini Zitto,Mdee,na Lissu wamepata Dharura na hivyo kushindwa kufika Geita.

Kwenye mkutano huo CHADEMA wamepata jembe lingine la kazi kwenye wilaya ya Geita.
 
Back
Top Bottom