NIONAVYO MIMI:KUELEKEA MTANI JEMBE SAA 10 JIONI.
Kwa mara ya tatu mfululizo,Simba wanaingia kwenye mechi ya leo kama "underdogs" dhidi ya Yanga.Hawepewi nafasi na fans nje ya uwanja but wao huwa, wanajipa nafasi wenyewe ndani ya dk 90.9
Ukuta "Berlin" wa Masoud na baba Ubaya,huku Pengine Owino akicheza na ndugu yake Musoti itahitaji nguvu ya ziada kuuvunja.Natamani kumuona Berko golini badala ya Mapunda.Hii ndo simba,Taifa kubwa!
Anko Mrisho,Ninyonzima na Kavumbagu,ni attacking line up ambayo inaweza kufanya kazi ya "fasihi",kuelimisha na kuburudisha.Natamani kuona Okwi akianzia benchi na Dida akianza golini.
Yanga wanahitaji Chuji kuanza kwenye midfield na Dilunga,ili kuwapa ulinzi Beki wao wa kati.Wanahitaji more defensive minded midfileders mbele ya mabeki wao kuliko attacking.
Okwi akiingia kipindi cha pili wakati Masoud na Baba ubaya wamepungua nguvu,ile kauli ya "mbele daima nyuma mwiko" ndipo itakapo timia.
Tambwe akitumia ubovu wa beki ya kati ya Yanga,atawaliza na Anko mrisho bribling na kasi vikikubali leo,simba chali!
Mkuu haya maelezo yote hayana maana hapa tena saivi,nilitegemea sasa hivi saa sita kasoro utakuwa maeneo ya uwanja wa Taifa hapo kwa ajili ya kuanza kutupa Updates za mechi sasa unatoa maelezo mareefu!!
Ninavyojua kwa mechi kama hii ukijumlisha na ujio wa Okwi kwa sasa najua kuna amsha amsha nyingi sana,tupe updates ili na sisi ambao hatupo uwanja wa Taifa kwa leo tena tuko nje ya nchi tufaidi!.
Hakuna cha Okwi wala Mbuyu ni kichapo tu.
Asubuhi maeneo ya Steerz Posta nimefika pale kuwasubiria wauza tiketi matokeo yake walipofika wananambia zimebaki za VIP A kwa 40,000. Sasa hivi nataka kuelekea Taifa.
Mkuu uwe makini sana ukae juu kule kwa sababu ule upande wa jukwaa la Yanga network huwa inasumbua sana,sijajua ni kwa nini?!
Leo nitakua Simba kwa mkopo, lakini akifungwa sinta husika kwa lolote.