Live Updates: Press Conference CHADEMA Makao Makuu Leo tarehe 18/06/2013

Status
Not open for further replies.
wakuu naomba mnieleweshe...mikanda saivi ipo mikononi mwa polis? je baada ya vijana kuporwa mikanda na polis chadema watakuwa na mikanda tena?

Wale wana copy tu,watu wengi walirecord,Mkanda mkuu anao Mbowe!
 
Kuna watu hawana uchungu na Tanzania na Raia waishio Tanzania Nikianza na mfano halisi wa Ritz sijawahi kujua huyu ni mtu wa aina gani katika jamii yetu nimefatilia mabandiko yake yananichosha kabisa

Me nakuambia hivi Ritz ni IKULU period kama mnabisha shauri yenu. Maana IKULU kuna mijitu mle haijui UTAIFA kwanza wao ni matumbo yao.

Mtu anatoa comments kama hizi kweli

 
"Legitimacy is a state or government being accepted and recognized by the law and by the people with popular acceptance ,due to its accepted patterns and standards .Such acceptance must base on logical reasoning."

Kimsingi serikali yetu bado ni "legitimate" lakini kuna maeneo kadhaa hapo juu sasa yanatia shaka.

(1)Popular acceptance; Sijui kama kwa sasa ipo tena?

(2)Accepted patterns; Sijui kama hatua zinazochukuliwa na serikali kushughulikia haya mambo ya milipuko na kadhalika kwa sasa zinakubalika na kuwaridhisha walio wengi!

(03)Standards; Sijui kama taarifa zinazotolewa na na serikali kufuatia mambo kadhaa yanayozua taharuki nchini zinakuwa zimekidhi viwango vya kuifanya serikali kujihakikishia kwamba iko "Full legitimate".

Ni bora serikali ikajichunguza na kufikiria haya mambo kwa kina.Isikubali watu wawili tu eti kwa kuwa ni wanachama wa chama chao wakatuvurugia nchi.
 
Iweje WAFU wameibukia dar???? Nilidhani wameenda kuwazika wafu wenzao!!!!!! By the way, la arusha ni ule mwanzo wa MWISHO WA COCKROACHES IN COMBAT WEAR. STAY TUNED

Mhh!! mna roho ngumu mnafurahia damu kumwagika??? lakini mkumbuke upole wa Watanzania haimaniishi kwamba wao hawawezi kumwaga damu za wahusika, ishu ni kwamba Watanzania hawakuzoea mauaji yanayo anza sasa lakini ikumbukwe haya mauaji yanawazoeza tabia na roho ya kikatili ya umwagaji damu taaratibu Watanzania, hivyo naogopa sana tusije hivi karibuni tukaanza kusikia huku imemwagika damu ya Mwigulu na familia yake, huku damu ya Nape mara huku imemwagika ya RPC Arusha mara huku imemwagika damu ya Kamuhanda, mara Kikwete kakoswa risasi akizindua mradi sehemu, Mara Mkuu wa Mkoa kauawa katika mazingira ya kutatanisha n.k
 
Taarifa zilizoenea Singida
nzima ni CDM ndio wamefanya Ule ugaidi tena kwa lengo la kupata
umaarufu. Nimemtumia IGP message Kama Lwaks anahisika pia kwani yeye ni
gaidi namba Moja nchini

Hiyo singida yako labda ya kidaru kwa taarifa yako ni kuwa taarifa zilizoenea singida ni kwamba CHADEMA wameshinda udiwani kiseke pamoja na rushwa ccm mliyotoa .
 
kama hawajajilipua, wamewezaje kurekodi video kwenye tukio la ghafla kama lile???
MKUU acha ushamba chadema ni tasisi kamili mikutano yake mingi sio wa arusha tu inakuwa full surveillance ndio utaratibu wa chama katika kuweka kumbumbu nyinyi hamfanyi hivyo kwa kuwa hamkubaliki hamko tayari kuonyesha malori yanavyosomba watu kwenda kwenye mikutano yenu au jinsi watu wanavyowazomea ni wazi uwezi kuweka kumbumbu za aina hii kama wafanyavyo chadema
 
"Legitimacy is a state or government being accepted and recognized by the law and by the people with popular acceptance ,due to its accepted patterns and standards .Such acceptance must base on logical reasoning."

Kimsingi serikali yetu bado ni "legitimate" lakini kuna maeneo kadhaa hapo juu sasa yanatia shaka.

(1)Popular acceptance; Sijui kama kwa sasa ipo tena?

(2)Accepted patterns; Sijui kama hatua zinazochukuliwa na serikali kushughulikia haya mambo ya milipuko na kadhalika kwa sasa zinakubalika na kuwaridhisha walio wengi!

(03)Standards; Sijui kama taarifa zinazotolewa na na serikali kufuatia mambo kadhaa yanayozua taharuki nchini zinakuwa zimekidhi viwango vya kuifanya serikali kujihakikishia kwamba iko "Full legitimate".

Ni bora serikali ikajichunguza na kufikiria haya mambo kwa kina.Isikubali watu wawili tu eti kwa kuwa ni wanachama wa chama chao wakatuvurugia nchi.

Serikali ni chombo kinachowekwa na wananchi kulinda matakwa yanayokubalika na wananchi.

Hapa kwetu serikali ni chombo kimewekwa kulinda matakwa ya wanaCCM milioni 2, miongoni mwao wakiwepo wahindi 20 wenye utajiri kushinda serikali yenyewe, na mafisadi wengine ambao wanayo hofu serikali ikibadilika utajiri wao haram upo mashakani.

Ufisadi ambao umefanywa hapa nchini kwa miaka hii yote umejenga tabaka linaloweza kununua hata mamluki wa kijeshi wakatumika kudhoofisha chama kinachohatarisha ufisadi. Kwa kufikiri tu, naamini upo uwezekano wa haya mauaji na mateso ya raia tunayo uhusisha na CCM zikawa ni njama za Wanachama wa CCM wanaofaidika na ufisadi, badala ya CCM kama taasisi.

Kwa mtizamo huu, tatizo la kiusalama tulilo nalo linaweza likawa SI CCM as such, bali udhaifu wa vyombo vya ulinzi na usalama: hasa TISS na Polisi, ingawa kwa kusema hivyo unamlaumu pia mwenyekiti wa kamatiya Ulinzi na Usalama ya Taifa--yaani Rais.

CCM imepoteza heshima (credibility) ya kuunda serikali nzuri. Jiaminisheni kuwa njia sahihi kwa ajli ya usalama wa taifa letu ni kuachia ngazi muwape watu wengine nafasi kujaribu kuongoza dola. Mtakosa mamlaka, lakini mtaishi katika nchi tulivu msimamie miradi yenu ambayo watoto wenu, ndugu zenu na marafiki zenu wameianziha kwa fedha za kifisadi.

Ondokeni kwa amani!
 
Roho zetu zitatolewa kwa Risasi na mabomu na zitapata stahiki machoni pa mungu muumba ila za kwao hao wauwaji zitatolewa na shetani kwa stahiki ya motoni. Tuendelee kuwaombea ndugu zetu waliotangulizwa kwa tamaa za madaraka, damu zao zitawalilia hadi ukamilifu wa dahari.
 
kama hawajajilipua, wamewezaje kurekodi video kwenye tukio la ghafla kama lile???

Ndugu yangu mbona unashindwa kutumia ubongo wako? Kulikuwa na watu wanarekodi matukio wakatii wa mkutano na hilo ni sehemu ya tukio hivyo lilirekodiwa hasa ukiweka maanani kuwa Wakati wa Mwangosi picha zilisaidia kupata ukweli. Wapo vijana walifuatilia na ndo maana hata muuaji kuingizwa kituo cha polisi watu walirekodi pia.
 
" WAFALME WAKITENDA YASIYO HAKI NI CHUKIZO , MAANA KITI CHA ENZI HUTHIBITIKA KWA HAKI ." Methali 16: 2 . R. I .P Makamanda
 
hapo sasa mnyika anaonyesha kuchanganyikiwa. kweli akili ndogo huwa na fikra finyu

Tulia unyolewe,video ipo na inaonesha kila kitu clear,utaona kama aliyechanganyikiwa ni mnyika au wewe na masavimbi wenzio,mlikuwa mnajua mtatoka kama kule kanisani eeh,mmezama msimu huu.
 
unaonea upuuzi unamiliki nini kichwani ishu serious watu wamekufa unaleta habari za uzandiki pumbavuuu
hawa jamaa kazi ya kuzurura tu. bungeni wamesusia baada ya waziri mgimwa kuwazidi kwa kila angle na sasa wanaamua kuendeleza porojo kwa mambo wanayojua kuwa yametokeaje
 
Cdm ujanja mwingi mbele giza, arusha mlikuwa mnapigwa udiwani na ccm na cuf, kuepuka aibu mkaua só. Mmeahirisha tu, aibu itawapiga kama umande wa asubuuhi.
 
Status
Not open for further replies.
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom