CHADEMA
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 488
- 2,468
Ndugu Wananchi popote mlipo ndani na nje ya nchi yetu tuko hapa ofisi ya CHADEMA Makao Makuu Kinondoni Mtaa wa Ufipa kwa ajili ya kuwaletea Live updates za Mkutano na Waandishi wa Habari ambao unatarajiwa kuanza hivi punde. Tutakuwepo hapa kuwaletea live updates. Stay tuned.
Anasema haiingii akilini eti Polisi ambao ni Watuhumiwa wakuu eti waunde tume ya kujichunguza wao wenyewe!! Mnyika anasema tume hii ya IGP ni ya kinafiki na inalenga kuficha ukweli. Anasema mtu kama Mngulu na Chagonja ni waongo wa mfululizo katika tume mbalimbali ambazo wamekuwa wakiziongoza. Anashauri badala ya watu hawa kuendelea kupoteza fedha za wananchi. Anasema bomu lile kwa ushuhuda wa Wananchi waliokuwepo uwanjani akiwemo mototo mdogo ni dhahiri liliwalenga Viongozi wa Chama chetu. Anasema Serikali,CCM badala ya kuomboleza na wafiwa wao wanaendesha propaganda. Anasema IGP anapaswa kuambiwa na watanzania wote kwamba wajibike au awawajibishe makamanda wake
Anasema baada ya Maombelezo kuisha ni wakati wa kusema kuwa mauaji yametosha sasa. Anawakumbuka Mwangosi, Mbwana Masoud, Ally Zona, Mbwambo na wengineo kuwa wameuawa na hakuna hatua zozote hivyo wakati wa watu kuendelea kuuawa umekwisha sasa. YATOSHA SASA
Waandishi wanauliza maswali sasa. Swali la 1. Je mko tayari kupokea milioni 100 za serikali, 2. Mtarejea lini bungeni 3. mko tayari kukabidhi video polisi? 4. mnaweza kutupa waandishi wa habari hizo video tuwape Watanzania?
Polisi wamekamata vijana watatu wa CHADEMA na kuwapiga na kuwatesa ili wawape mkanda badala ya kuwachukulia kama raia wema. Hivyo kuwapa mkanda imetutia hofu. Lakini mkanda utatolewa baada ya Wanasheria wetu akiwemo Tundu Lissu, Mabere Marando, Prof. Safari kutathmini athari za kisheria baada ya mkanda huo kutolewa. Hatujajadili kuhusu kupokea Milioni za Lukuvi lakini kwa maoni yangu (Mnyika) Lukuvi kutoa dau kwa mauaji yaliyofanywa na polisi wao ni ufisadi mkubwa wa kutaka kufuja hela za serikali kwa kisingizio cha kupata taarifa kutoka kwingineko. Anashauri fedha hizo zielekezwe kwenye maendeleo. Anashangaa Rais kutokutoa rambirambi hata kwa mjane wa Mwangosi. Kuhusu kurudi Bungeni amesema tutarudi lakini Sekretarieti imekubaliana na kauli ya M/kiti na hivyo sasa ni kauli ya Chama kwamba hakuna Mbunge yoyote wa CHADEMA atakayeshiriki vikao vya Bunge hadi taratibu maombolezo yaishe. Anashangaa kwanini Bunge linaendelea wakati katika matukio mbal...imbali kama ya Mtwara n.k bunge limewahi kuahirisha vikao vyake lakini kwa hili la CHADEMA anashangaa bunge kuendelea na shughuli zake. Pia anashangaa kauli ya serikali kutolewa miongozo 4 wakati kanuni haziruhusu kauli ya serikali kuibua mjadala otherwise kauli hiyo inabidi ijadiliwe lakini jambo hilo halikufanyika. ni udhaifu wa Bunge. Anasema wakirudi Bungeni lazima Bunge lieleze kuanzia mauaji ya Arusha, Mwangosi, mateso ya Ulimboka, Kibanda kiasi cha Waziri Mkuu kusema uongo Bungeni. Anasema serikali imekuwa ikikamata watu hewa na kuwapeleka Mahakamani ili kulizuia Bunge lisijadili mambo hayo muhimu yanayowagusa Wananchi kama haya. Anasema watarudi kwa Wananchi na kuwaeleza yote. Anawaomba Wananchi wote walioguswa na misiba hii na iliyopita kushiriki kwenye mazishi kama wako karibu na misiba hiyo na kwa wale waliombali wamtumie ujumbe IGP kwenye namba yake aliyosambaza. Ujumbe wa maombolezo na wa kutaka uwajibikaji. Anasema serikali hii inayojiita sikivu haisikii na hivyo wananchi lazima wailazimishe kusikia kwani yenyewe ndio inayohusika kwenye kadhia zote hizi. Wananchi wanapaswa kuikataa CCM kwanza.
Asema kuna watu wanaamini kikwete ni msikivu lakini kwa hili la mauaji kikwete sio msikivu hata kidogo. na ndio maana amewapandisha cheo wakuu wa polisi wote waliohusika na mauaji. Anasema Serikali ina nafasi nyingine ndogo sana (finyu) kabla maombolezo hayajaisha. Nafasi hiyo ni kuunda tume ya kijaji kuchunguza mauaji haya kwani huko tunakoelekea ni kubaya sana. (NA TUMEFIKISHWA HAPA KWA UDHAIFU WA RAIS, UZEMBE WA BUNGE). Anaulizwa Je CHADEMA wanamkakati gani mwingine zaidi ya kuhusu haya mambo hasa huu uonevu wa Serikali kuhusu swala la Arusha. Kwani wanaua watu na serikali imekataa kutangaza hata kata wazi iliyoachwa na diwani wa CCM aliyehamia CHADEMA? Mnyika anasema watatoa taarifa baada ya maombolezo lakini ijulikane tu kwa sasa kuwa SASA IMETOSHA. "Asantheni kwa kunisikiliza" Anamaliza. Asantheni kwa kutufuatilia