LIVE:sherehe za uhuru wa JMT

Kikwete anakaribia kuwasili na kupokea salamu ya rais na kupigiwa mizinga 21.
 
Kikwete anaingia yuko kwenye gari la wazi pembeni yuko mwamunyange
 
Sherehe hizi zimepoa.tusubiri gwaride linaweza kulichangamsha.
 
Do some editing kwa heading yako bse 1961 JMT haikuwepo bali tulikuwa na Tanganyika
I wish Tanganyika yetu irudi maana zenji ndo washaanza kumekguka
 
ndo maana tukawa maskini, na tutaendelea kuwa maskini. kwasababu hata mawazo yetu ni ya kimaskini..hivi kuadhimisha siku ya uhuru ni kushabikia gwaride, au ni kuangalia jinsi wanajeshi wanavyopiga miguu uku jasho likiwatoka..nilitegemea siku ya leo vyomba vya habari vingekuwa vinatoa mstakabadhi wa nchi hii yenye ufisadi.. kila mtu anasimulia, eti mizinga 21 inapigwaa..AIBUU..
siku ya uhuru ni siku ya kujadili mustakabadhi wa taifa,..leo tungefarijika kusikia vyomba vya habari vinaongelea ufisadi au katiba mpya..
sio eti, "wanajeshi wanapiga kwata mpaka kofia zina-anguka"
AIBUU TUPU TZ
 
hizi ndo aibu za TZ..
eti mtangazaji anajisifia sio lazima kwenda cHINA kujifunza Kiduku. hata TZ tuna ujuzi
mi nilihisi hii ndo fursa kuwaelimisha wa-TZ kuhusu muktabadhi wa nchi yao.
sio kuwaambia maana ya mizinga 21, hivyo vitu vimepitwa na wakati, kwenye kizazi hiki cha utandawazi
 
Do some editing kwa heading yako bse 1961 JMT haikuwepo bali tulikuwa na Tanganyika
I wish Tanganyika yetu irudi maana zenji ndo washaanza kumekguka

naogopa kutumia hilo jina la Tanganyika kwa sababu hilo taifa halipo kwa sasa.ningeweza kutumia Tanzania bara but hata hilo taifa linatambuliwa na waandishi wa habari.unadhani kikwete ameenda pale kama raisi wa Tanganyika,Tanzania bara,jamhuri ya watu wa Tanganyika au jamhuri ya muungano wa Tanzania(JMT).CONFUSING !!!
Yote haya ni kwa sababu ya katiba iliyozeeka.
I will never edit kama vipi kila mtu atoke na jawabu lake la hii Tungo TATA.
 
ckuwa hewani kwa muda..wadau naomba kujua JK kahutubia leo? na kama kahutubia lipi jipya kwa maendeleo ya nchi yetu? vipi wapinzani walikuwepo? i mean CDM not others
 
naogopa kutumia hilo jina la Tanganyika kwa sababu hilo taifa halipo kwa sasa.ningeweza kutumia Tanzania bara but hata hilo taifa linatambuliwa na waandishi wa habari.unadhani kikwete ameenda pale kama raisi wa Tanganyika,Tanzania bara,jamhuri ya watu wa Tanganyika au jamhuri ya muungano wa Tanzania(JMT).CONFUSING !!!
Yote haya ni kwa sababu ya katiba iliyozeeka.
I will never edit kama vipi kila mtu atoke na jawabu lake la hii Tungo TATA.
lakini wewe umependekeza leo ni siku ya kumbukumbu uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaani (JMT)...? hivi huwezi kusherekea siku ya kuzaliwa kwa Babu yako ingawa hayuko duniani ni mfano tu
 
lakini wewe umependekeza leo ni siku ya kumbukumbu uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaani (JMT)...? hivi huwezi kusherekea siku ya kuzaliwa kwa Babu yako ingawa hayuko duniani ni mfano tu

babu hajafa(yupo ana miaka 49) ila jina lake limebadilika ingawa kuna utata wa jina lake.
 
Hata mimi hizi sherehe cha maana kilichoniongezea ni siku moja ya kupmzika nyumbani. Ningefurahi kama watanzania hasa watoa habari kwa umma na viongozi wangetumia fursa hii kutuelezea wapi taifa limetoka, wapi tulipo na wapi tunaelekea.
Kwa nini tupo tulipo na je tumeridhishwa?
kama ndiyo, tufanyeje tuendelee kubaki tulipo?
Kama sivyo, tilifanya nini kilichotuweka hapa tulipo?
Na tufanyeje ili tutoke tulipo?
Jamani, nchi yetu ina matatizo mengi zaidi ya kwenda kushangilia risasi na gwaride. I agree, it is part of the celebration kupata uhuru kutoka kwa wakoloni. But the way we celebrated it 40 years ago should not be the same as the way we celebrate it now. walau basi, tuonyeshwe silaha wanajeshi wetu wametengeneza, mbinu mpya walizokuja nazo, etc.
It is a time to display what we have achieved so far, and discuss on what is yet to be done.
Please, tubadilikeni...
la sivyo nchi hii itafia mikononi mwetu na itakuwa aibu kubwa kwetu...
 
babu hajafa(yupo ana miaka 49) ila jina lake limebadilika ingawa kuna utata wa jina lake.
Hahah mzee wa 24 ni afadhali uichukue kama mama:
alipokuwa mdogo aliitwa Tanganyika, baada ya kukua akaolewa na jina lake likabadilika kuwa Tanzania. So, ni sahihi kimuita Tanganyika na ni sahihi kumuita Tanzania...swala labda ni wakati gani na kwa madhumuni yapi!
 
Hahah mzee wa 24 ni afadhali uichukue kama mama:
alipokuwa mdogo aliitwa Tanganyika, baada ya kukua akaolewa na jina lake likabadilika kuwa Tanzania. So, ni sahihi kimuita Tanganyika na ni sahihi kumuita Tanzania...swala labda ni wakati gani na kwa madhumuni yapi!

teh teh teh! Mimi nimeamua kumpa heshima yake (Mrs)Tanzania.yawezekana angekua hayuko kwenye ndoa ningemuita (Miss )Tanganyika.yani ni mchanganyo mtupu! KATIBA !!KATIBA!! KATIBA!!
 
wewe jackb, hivi unaanzaje kwenda kule uwanjani kusherehekea uhuru?
Najiuliza mwenyewe hapa sipati jibu. Ni hiyari au watu wanapozwa? Siulizii wale askari wa vikosi na viongozi wa chama na serikali
 
Ukijaribu kufanya analysis utatambua kwa ujumla serikali na wananchi hawakuwa na muamko au uchangamfu ukilinganisha na sherehe zilizopita.
Kikwete hakuwa na raha kabisa labda aliogopa hata kuandaa speech akidhani CDM wangeweza kuja uwanjani na kufanya kama yale ya Dodoma.Ama inawezekana alikuwa anawaza ni kiasi gani wafadhili watachangia katika budget hasa baada ya mkulo kuchakachua.
Viongozi wengine walikuwa wapowapo tu,mfano seif na Bilal hawakuonekana kama ni mara yao ya kwanza kuhudhuria sherehe hizi kama makamu wa marais.
Kwa upande wa vyombo vya ulinzi na usalama walikuwa wamepoa kabisa,uchapaji wa miguu ulikuwa legelege ukilinganisha na mwaka jana au hapo kabla.washashtuka kama serikali haina heshima ya nini iheshimiwe(hii ni hatari sana).
Vikundi vya halaiki vilijaribu bila mafanikio kutumbuiza sherehe hizi.wale watoto wapatao 700 walionekana kama walikunywa chai kikombe kimoja na ka slesi cha mkate,yaani morali nguvu na sauti vilikuwa chini kabisa.
Watangazaji wa T.V ndio walikuwa hoi kabisa utadhani wanatangaza msiba wa kitaifa,hawakujua nini cha kuongea. sijui hawakuhadiwa kifuta jasho?
Wana JF,wengi wao hawakuonekana kuchangia hapa jamvini inaelekea wengi waliamka na "Hangover" ya safari au castle.
Na hii ndio analysis ya kilichojiri kwenye sherehe zetu tukufu.TAFAKARI CHUKUA HATUA.
 
Back
Top Bottom