LIVE:Kilimanjaro Stars VS Burundi From Kampala-Uganda

WABHEJASANA

JF-Expert Member
Jun 22, 2011
4,225
869
Wakuu,

Leo kwa mara nyingine tena tunaingia uwanjani kupambana na Timu ya Taifa Burundi katika mwendelezo wa michuano ya Challenge,na lengo ni moja tu kuhakikisha kwamba tunashinda mchezo huo ili kuwa Timu ya pili Kutinga hatua ya Robo fainali ya michuano hiyo.

Mchezo wa leo ni mgumu na hasa ikizingatiwa kwamba Burundi sio Timu ya Kubeza kwa sababu tayari wao ndio wanaoongoza kwenye kundi letu ingawa ni kwa tofauti na magoli ya kufungwa,tutajitahidi kuwaletea moja kwa moja michuano hii kwa siku ya leo kwa wale ambao watakuwa hawako kwenye TV wala redio.

lakini kwa wale wenye Tv TBC inarusha moja kwa moja michuano hiyo kutoka Kampala bila ushirika na Tv yoyote ile,lkini pia Kenya Broadcasting Co-oparation (KBC) ya Kenya,na Uganda Broadcasting Co-oparation (UBC) wanaonesha LIVE pamoja na Super Sport 9 East,Lakini kwa Redio kuna TBC Taifa,Kiss FM na Redio Free Africa Masafa ya kati.

Tuiombee Kilimanjaro Stars Ushindi..........Makoye Matale,Concrete,Bujibuji na Wengineo twende kazi sasa....
 
Nasubiri wafike Fainali nione kama ntakuwa na uwezo natoka hapa Kaisho-Murongo-Kikagati -Mbarara huyo Kampala
 
Nasubiri wafike Fainali nione kama ntakuwa na uwezo natoka hapa Kaisho-Murongo-Kikagati -Mbarara huyo Kampala

Hicho ndicho tunachooembea sisi sote ili walau tupate nafasi ya kurudi tena huku,leo mimi na kundi langu tumebahtika kuja huku asubuhi tulileta biashara yetu ya dhahabu kutoka huko Nyarugsu Geita sasa nimeona niingie uwanjani niangalie ka sababu mechi ya leo ni kali.

lakini yote kwa yote tumeshajipanga huko nyumbani kwetu wachimbaji wengi san tunawasha magari yetu tunapitia BK na kuja kwenye fainali,lakini hiyo ni nkama tu tutaingia Fainali ya mashindano haya Mkuu,na ikiwezekana tutapeana namba ili tukupitie hapo BK,au kama uko Kaisho maana yake ni kwamba tunakutana pale Kyaka sijui mkuu unasemaje?
 
ball control poor, blind pass good, cordination fair, goolkeeping excellent, striking moderate, foul play best.
 
Kila lililo la kheri Kili Stars...tunawasubiria robo fainali na nusu fainali mpira utakuwa mzuri sana maana kuna team nzuri sana na viwango juu kuliko mwaka jana
 
uwanja mbovu kinoma, km ulishawahi cheza mpira utaelewa, naona penati sasa inaelekezwa kwetu
 
Sikupenda uchezeshaji wa refa, nadhani alikuwa upande wa burundi, ona walivomfanya kazi moto nk
 
Ngapi? Unaona au umesikia?
Kilimanjaro Stars 0 - Burundi 1
Goli limefungwa kwa njia ya penati baada ya Shomali Kapombe kumchezea ndivyo sivyo ndani ya 18 Suleman Ndikumana mshambuliaji wa Timu ya Burundi
 
Hicho ndicho tunachooembea sisi sote ili walau tupate nafasi ya kurudi tena huku,leo mimi na kundi langu tumebahtika kuja huku asubuhi tulileta biashara yetu ya dhahabu kutoka huko Nyarugsu Geita sasa nimeona niingie uwanjani niangalie ka sababu mechi ya leo ni kali.

lakini yote kwa yote tumeshajipanga huko nyumbani kwetu wachimbaji wengi san tunawasha magari yetu tunapitia BK na kuja kwenye fainali,lakini hiyo ni nkama tu tutaingia Fainali ya mashindano haya Mkuu,na ikiwezekana tutapeana namba ili tukupitie hapo BK,au kama uko Kaisho maana yake ni kwamba tunakutana pale Kyaka sijui mkuu unasemaje?
Kyaka mbali kutoka kaisho, mie ni fasta dkk 20 nipo border ya uganda kutoka kaisho
 
Back
Top Bottom