Live in peace(L.I.P) vs Rest In Peace(R.I.P)

Pawaga

JF-Expert Member
Feb 14, 2011
1,330
966
PAWAGA lini uliambiwa "live in peace?". Niamini siku ukifariki zitakuwa Rest in peace nyingine sana!!!".
Hayo yalikuwa ni maneno ya mzee LUKOSI wa Kalenga. Ni mzee maarufu sana but very unique na alikuwa na desturi ya kuandaa kaburi lake ( yaan anachimba kabisa kaburi la kuzikwa endapo atafariki). October 2007 nkiwa mwalim pale Lipuli sec nlipanga nyumba jiran na mzee huyu ambae alikuwa mwanajeshi mstaafu,siku moja nliamua kumuuliza kwanini anajichimbia kaburi lake?. Alinijibu watu wengi hasa ndugu wanadhan undugu ni kuzikana tu ndo maana hakuna anaekutakia uishi vema dunian lakin ukifariki wengi watalia na kuomboleza " rest in peace PAWAGA ". Mimi nachimba kaburi kuwaonyesha kuwa si lazima wao wanizike.
Nkamuulize tena sasa mzee umechimba kaburi lkn kumbuka kuingia humo mapema kama hutaki kuzikwa na hao ndugu. Alijibu " maiti ni kama kinyesi bafuni huwez kuoga bila kukitoa hivyo hivyo hakuna atakaeweza kukaa na maiti hivyo kufukiwa lazima ntafukiwa hata kama na halmashaur tofauti ni uchimbaji tu wa kabur langu".
Kwa wakat ule sikumuelewa nliamua tu kukubaliana nae lkn ukwel nilimuona kama chizi but now nmemuelewa sana na natamani nimweleze aongeze na sanduku lake pia awalipe in advance watu wa kumlilia na kumzika siku akifariki ili ndugu wasisogelee kabisa.
Najaribu kuwaza kwa sauti siku nkifa hapa JF jinsi wall yangu itakavyotililika kwa "rest in peace Pawaga", sipati picha sifa ntakazomwagiwa hapa na watu ambao hata siku moja hawajawahi kuniambia " live in peace Pawaga". Nmejaribu kuwaza unafiki wa ndugu watakavyokuwa wanalia kwa sauti kubwa na michango itakavyotolewa.
Acha niishie hapa lkn hope Meseji ya mzee wangu Lukosi ambae sijawah hata siku moja kumwambia live in peace imewafikia.
Ok huyu mzee sijui yupo hai au ndo niseme R.I.P?.
 
Bado upo Iringa chief? Km kuna tatizo ni bora ukaomba ushauri maana huu ujumbe wako ni mzito mkuu
 
Back
Top Bottom