Litania ya hujuma za CCM Kwa UKAWA/CHADEMA ni masikitiko sana

TL. Marandu

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
3,625
5,805
Nijaribu Kueleza Kwa Kifupi sana, Hujuma Kubwa sana ya Kisiasa, Iliyofanywa na Inayoendelea Kufanywa na CCM dhidi ya UKAWA Tangu Kabla ya Uchaguzi wa 2015, Wakati wa Uchaguzi na Hadi sasa.

Matendo ya CCM wakati Ule yalionyesha Jinsi ambavyo walijua wazi Kuwa hawawezi kuishinda Ukawa Kihalali, Na Hata sasa Matendo yao Ya Hujuma chafu sana na Za Aibu, Za Fidhuli na Jesuri, Zinaonyesha Wanafahamu hawakushinda Kihalali na Wanahofu Kubwa sana Juu ya Ukawa.

Hujuma Chafu za CCM Kabla na Baada ya Uchaguzi.

1) Wakati CCM wakilikuwa wamefanya Ufunguzi wa Kampeni zao Jangwani bila ya Kubugudhiwa na Yeyote, CCM wakitumia Vibaraka Wao walijaribu sana Kuwazuia Ukawa wasitumie Uwanja wa Jangwani, Wazalendo, Wapenda amani Wa Ukawa wakajitahidi sana Kutafuta haki ya Kutumia uwanja Ule Kwa amani bila fujo.

2) Wakati wa Upigaji Kura CCM wakitumia Dola wakakataza Ukawa wasikae mita 200 Kulinda kura, na Pia Wakawazuia wengi wa Mawakala wao Kuingia vituo vya kuhesabia Kura, Ukawa Wakakumbatia amani.

3) Serikali ya CCM Ikavamia na Kupora Kijambazi kwa Kutumia Polisi Computer zaidi ya 60 za Ukawa za Vijana waliokuwa wakisaidia Kujumisha matokeo ya Kura za Urais Kuharibu Ushahidi wa Matokeo, Ikauma sana, Ukawa Wakakumbatia amani.

4) CCM wakitumia Dola Wakafuta Matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar ambapo Maalim Seif Alishinda, na Hapo Pia Ukawa Wakakumbatia Amani.

5) CCM wakitumia Vibaraka wao wakajaribu sana Kuiba Umeya wa Majiji ambayo Ukawa walishinda kwa Kutumia mbinu chafu sana na za Kutia aibu, Ukawa wakakumbatia amani, wakadai haki kwa Uvumilivu.

6) Akauawa Kiongozi wa Ukawa Alphozo Mawazo, CCM na Mapolisi wao wakazuia Mazishi, Ukawa wakakumbatia amani wakatafuta haki mahakamani, Kuzika Mfu wao, hujuma gani hii aibu gani hii?

Alivyokufa Mawazo


Na sasa Utawala Huu wa awamu ya Tano,

1) CCM Kwa Unafiki Mkubwa bungeni kwa Maagizo ya Serikali, wakazuia Matangazo ya Mojakwa moja ya Bunge Kwa Lengo chafu, La Kuzuia a)Uonevu Bungeni dhidi ya Ukawa Usionekane b)Vitisho vya CCM na Zomea zomea na Kejeli za CCM dhidi ya Ukawa Visionekane 3)Michango na Umahiri wa wabunge wa Ukawa Usionekane.

Serikali Kuleta Polisi Bungeni,


2) Ukawa wakaletewa Polisi na Mbwa Kupigwa Bungeni, Wakakumbatia amani.
3) Wabunge maarufu wa Ukawa Pamoja na Zitto Kakwe wakafungiwa. Pamoja na Kukamatwa na Kufuunguliwa Mashitaka ya Hovyo.
4) Magufuli Kuwaagiza Polisi wawanyamazishe Wabunge wa Upinzani wasifanye Mikutano au hata Makongamano ya ndani (Kama hajawatuma Mbona hawazuii) Wakati yeye na Wanaccm wenzake wakiendeleza siasa zao katika kila walifanyalo
5) Kejeli za Rais dhidi ya Viongozi wa Ukawa mfano alivyohoji iwapo meya wa jiji anapenda ujambazi?
6) Kukamatwa ovyo kwa Viongozi wa Ukawa hasa Vijana kuwatia hofu.
7) Kuzuia Sherehe za Wavyuo wa Chadema kwa Mabomu, Ingawa Sherehe kama Hizo zilifanywa na Wanavuo wa CCM Na Kufanana Kwa Kila hali Kimazingira na Maudhui.


Hawa hawakukguswa


Hawa wakapigwa mabomu

8) Waliomtukana Mgombea matusi hata ya Kumkejeli Mungu Mwenyewe wakati wa Kampeni eg. Nape Mnauye wakapewa Uwaziri na Mh. Magufuli, lakini Wasio CCM hata facebook zao zinaingiliwa na akisema mtu kinyume na Mh Magufuli anashitakiwa, Yako wapi Mashitaka ya waliosema Lowassa Kajinyea. Nikisema hivyo Juu ya Rais Leo Nashitakiwa!

Mimi Nadhani, Ni wakati sasa Ukawa Kuwaonyesha CCM sasa Basi, Kwa sababu Uzalendo wenu, Kupenda kwenu Kuchagua amani CCM wananusa Kuwa Ni Udhaifu. Na zaidi sana Msipovumilia tena, Watanzania waliowengi watawaelewa, Dunia Itawaelewa. Mmeonewa sana, Mmehujumiwa sana, Mmedhalilishwa sana. Na Ukweli wanaofanya hivyo sio kwamba wanayonguvu ya Kuzima Nguvu za Umma walio nyuma yenu, Wanakesha na Kuomba Muendelee Kutishika. Maana Siku Mkionyesha sasa Basi, Hakika ndipo mtajua hawa ni Chui wa Karatasi. Na kwa Kuwa hamdai Jambo Kubwa, Hamdai Kupindua serikali, Bali Mnadai Uhuru wa haki zenu za Kikatiba, Watakuwa na Wazimu Kuendelea na Tabia hii ya Kihuni wakiamini kuwa wataweza Kuliongoza Taifa. Baada ya Kenyata Kuteswa Kufungwa na Kuteswa alisema Maneno haya, "It is by our action that they will know that we mean business"



Kituko, Kioja wanachokifanya CCM, Ni Mithili ya Bondia Hayawani anayejitangazia Umahiri, halafu kwa kujuana na Refa, wanamfunga Bondia Mpizani, Mikono na Miguu hata asiweze Kujigeuza, Halafu Filimbi inapigwa, Bondia hayawani huyu anamvamia Bondia aliyefungwa Mikono na Miguu, anampiga Kila mahali hata chini ya Mkanda, Na refa asiye na aibu baada ya Kipenga cha Mwisho anamnyanyua Hayawani huyu Mkono Kuwa Kashinda, Ndio Mazingira wanayojijengea CCM na Magufuli 2020. Hili likitokea Uwanjani kweli mawili watazamaji watatoka nje, na wale wakali wasiovumilia upuuzi watampiga mawe na chupa za maji na za soda. Na wote watakuwa wamefanya sawa. Kama hili halifai Katika Michezo Livumiliweje Katika Demokrasia na Uhuru wa nchi yetu.

Ninavyosema kuwe na action sisemi kuvuruga amani? Na Nipo Tayari Kujibu Mahakama yoyote. Ila Naona Kuwa Muda Umefika wa Kupuuza Amri zilizokinyume na Katiba na Sheria. Ifike wakati Serikali ya CCM wakikataza Mikutano kwa Kutumia Polisi Basi Ukawa wafanye Mikutano Kwa Nguvu. Na kama Polisi wakija Kuvuruga amani na Kuwapiga wananchi, Basi Wananchi wajihami dhidi ya Uhalifu huo. Itakuwa Unafiki sana CCM Iliyowasaidia ANC, na FRELIMO Kupambana na Uonevu na Ubeberu leo wanafanya Ubeberu ule ule na Kuzidi dhidi ya Raia wanzao. This Must end. Kwa Wenye Hekima, in a long run huu upuuzi utaathiri sio tu Ukawa, bali Utaleta hasara kubwa sana, Kabisa! Kwa Taifa zima ikiwepo na CCM kama chama. Tabia hizi za Kijinga zitaangamiza maendeleo ya Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa, au hata Kutufikisha katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.
 
MACCM yamegundua kwamba UKAWA kuna watu makini mno na hivyo hawawezi kuwashinda kwa hoja ndani na nje ya Bunge. Hivyo wakaamua kuja na mkakati wa kubaka demokrasi na kutumia polisi ili kuwawezesha kukamilisha ubakaji wao wa demokrasi. Siku vyombo vya dola vikigoma kuikingia kifua CCM katika ubakaji wake wa demokrasi nchini siku hiyo ndiyo CCM itazikwa rasmi nchini. Naomba tu siku hiyo isiwe mbali sana ili Watanzania tuondokane na hawa wahuni, wezi, mafisadi, majangili, wakwapuzi wa mashirika ya umma, wapokea rushwa, wakwapuzi wa nyumba za Serikali n.k.
 
Mtoa mada ubarikiwe sana. viongozi wa upinzani wanapaswa kutafakari sana hatua hii taifa lilipofikia.wana njia mbili, ama waungane na ccm ama wasonge mbele. nje ya hapo hawataeleweka na umma wa watanzania kamwe....
 
Yote yana mwisho mkuu, hakuna uovu unaodumu milele
Mimi sina Kadi ya Chama chochote na Naapa Juu ya Uhai wa Watoto wangu mjue jinsi nilivyo sincere, Ingekuwa Ni Ukawa wangekuwa madarakani na Wakawafanyia CCM hivi Ningesikia uchungu huu huu. Kwani Mimi sio Miongoni mwa wanaotaka CCM ife, Nataka haki na equilibrium ya Kisiasa. Akishidwa mtu au chama uwe ni udhaifu au uzembe wake mwenyewe. Na Mbaya zaidi ya Yote Hainiingii akilini Mh. Magufuli ambaye anaimba Kila siku, "Msema Kweli ni mpenzi wa Mungu" awe Mnafiki Hivi. Inakuwaje Rais anayechukia Kutumiwa Kama ride ya Mafisadi, na Kwa Maneno yake, "Not me, aheri nikachunge ndege" Iweje huyu huyu atumike kama Upanga na Minyororo ya Uonevu. Iweje yeye akubali kutumika kama mbeleko ya CCM isivyo halali? Wapo Watu Makini na Wema ndani ya CCM na hawa hawahitaji Kubebwa na yeyote. Kwa anayofanya Bila Kujua ni Kustawisha wasiostahili CCM, akidhani anajiwekea Binafsi Mzingira mazuri. Ina faida Gani Kama Mh. Akashinda 2020 isivyo halali na akawa hajafanikiwa au Muda Mfupi tu mafanikio yake (ambayo kwa hali hii siyatabiri) yakayeyuka? Atakuwa amepata faida gani?
 
Mimi sina Kadi ya Chama chochote na Naapa Juu ya Uhai wa Watoto wangu mjue jinsi nilivyo sincere, Ingekuwa Ni Ukawa wangekuwa madarakani na Wakawafanyia CCM hivi Ningesikia uchungu huu huu. Kwani Mimi sio Miongoni mwa wanaotaka CCM ife, Nataka haki na equilibrium ya Kisiasa. Akishidwa mtu au chama uwe ni udhaifu au uzembe wake mwenyewe. Na Mbaya zaidi ya Yote Hainiingii akilini Mh. Magufuli ambaye anaimba Kila siku, "Msema Kweli ni mpenzi wa Mungu" awe Mnafiki Hivi. Inakuwaje Rais anayechukia Kutumiwa Kama ride ya Mafisadi, na Kwa Maneno yake, "Not me, aheri nikachunge ndege" Iweje huyu huyu atumike kama Upanga na Minyororo ya Uonevu. Iweje yeye akubali kutumika kama mbeleko ya CCM isivyo halali? Wapo Watu Makini na Wema ndani ya CCM na hawa hawahitaji Kubebwa na yeyote. Kwa anayofanya Bila Kujua ni Kustawisha wasiostahili CCM, akidhani anajiwekea Binafsi Mzingira mazuri. Ina faida Gani Kama Mh. Akashinda 2020 isivyo halali na akawa hajafanikiwa au Muda Mfupi tu mafanikio yake (ambayo kwa hali hii siyatabiri) yakayeyuka? Atakuwa amepata faida gani?
so what's your point?gamba tu wewe.

swissme
 
Kulialia tu mwanzo mwisho. Mbowe mwenyekiti wa kudumu, Seif katibu wa kudumu. Lowassa mgombea asiyepitishwa na wanachama, Sumaye alihamia asubuhi akala shavu la kumnadi mgombea. Wako wengine wengi waliohamia kipindi uchaguzi ili wapate nafasi ya ugombea na wakapata. Mfano kina Lembeli, Bulaya n.k.

Hii inaonesha upinzani bado una siasa za kufikirika, wafuasi wake wanadhani kuwa wanaweza kuonghoza nchi, lakini ukweli sivyo. Ni siasa za porojo tu, vyama vinaendeshwa na umaarufu wa mtu binafsi. Wapi NCCR Mageuzi, NLD na CUF huku bara? Sasa hivi show yote ni CHADEMA ya Lowassa tu. Think!!
 
Kulialia tu mwanzo mwisho. Mbowe mwenyekiti wa kudumu, Seif katibu wa kudumu. Lowassa mgombea asiyepitishwa na wanachama, Sumaye alihamia asubuhi akala shavu la kumnadi mgombea. Wako wengine wengi waliohamia kipindi uchaguzi ili wapate nafasi ya ugombea na wakapata. Mfano kina Lembeli, Bulaya n.k.

Hii inaonesha upinzani bado una siasa za kufikirika, wafuasi wake wanadhani kuwa wanaweza kuonghoza nchi, lakini ukweli sivyo. Ni siasa za porojo tu, vyama vinaendeshwa na umaarufu wa mtu binafsi. Wapi NCCR Mageuzi, NLD na CUF huku bara? Sasa hivi show yote ni CHADEMA ya Lowassa tu. Think!!
Bora wao wanachaguliwa Kwa Kura sio Kupitishwa Kwa Lazima, Lowassa alichaguliwa na Mkutano Mkuu, Mbowe alishinda Uwenyekiti wa Chadema kwa asilimia 98% dhidi ya Mgombea Mwenzake, Tare 23-7-2016 Mh. Magufuli atagombea na Nani? Sumaye Unayemsema alikuwa Waziri Mkuu kwa Miaka 10, kuliko Waziri Mkuu yeyote Tanzania unadhani angekuwa Ovyo Mkapa angemwacha?
Na Porojo Unazosema hapa zinajibu vipi hoja iliyoko mezani? Its Just Blah Blah
 
Kwa akili hizi za vijana wa ukawa ni hakika bila shaka kuwa taifa linaangamia. Ni akili zenye ubongo ulioganda, akili zisizoweza kubaini jambo na kutofautisha mema na mabaya full kulialia upuuzi na upumbafu. Ee Mungu linusuru taifa letu na hiki kizazi kilichopotoka kwa kuziuisha akili na fahamu zao na kukiponya.
 
Samia na upinzani
Akizungumza kwenye kikao na viongozi wa CCM wa mkoa, Samia alisema katika kipindi cha miaka 20 tangu siasa za vyama vingi ziliporejeshwa, vyama vya upinzani vimejijenga na sasa vinaweza kukabiliana na Serikali.

“Bila kusahau kwenye Bunge tuna wenzetu kutoka vyama vya upinzani ambao wamekua vya kutosha, wamepevuka vya kutosha,” alisema Makamu wa Rais.

“Katika miaka 20 ya vyama vingi, upinzani umezalisha watu makini ambao wako tayari kupambana na Serikali. Je, wa kwetu tumewaandaaje katika kupambana nao?”

Kwa akili hizi za vijana wa ukawa ni hakika bila shaka kuwa taifa linaangamia. Ni akili zenye ubongo ulioganda, akili zisizoweza kubaini jambo na kutofautisha mema na mabaya full kulialia upuuzi na upumbafu. Ee Mungu linusuru taifa letu na hiki kizazi kilichopotoka kwa kuziuisha akili na fahamu zao na kukiponya.
 
Nijaribu Kueleza Kwa Kifupi sana, Hujuma Kubwa sana ya Kisiasa, Iliyofanywa na Inayoendelea Kufanywa na CCM dhidi ya UKAWA Tangu Kabla ya Uchaguzi wa 2015, Wakati wa Uchaguzi na Hadi sasa.

Matendo ya CCM wakati Ule yalionyesha Jinsi ambavyo walijua wazi Kuwa hawawezi kuishinda Ukawa Kihalali, Na Hata sasa Matendo yao Ya Hujuma chafu sana na Za Aibu, Za Fidhuli na Jesuri, Zinaonyesha Wanafahamu hawakushinda Kihalali na Wanahofu Kubwa sana Juu ya Ukawa.

Hujuma Chafu za CCM Kabla na Baada ya Uchaguzi.

1) Wakati CCM wakilikuwa wamefanya Ufunguzi wa Kampeni zao Jangwani bila ya Kubugudhiwa na Yeyote, CCM wakitumia Vibaraka Wao walijaribu sana Kuwazuia Ukawa wasitumie Uwanja wa Jangwani, Wazalendo, Wapenda amani Wa Ukawa wakajitahidi sana Kutafuta haki ya Kutumia uwanja Ule Kwa amani bila fujo.

2) Wakati wa Upigaji Kura CCM wakitumia Dola wakakataza Ukawa wasikae mita 200 Kulinda kura, na Pia Wakawazuia wengi wa Mawakala wao Kuingia vituo vya kuhesabia Kura, Ukawa Wakakumbatia amani.

3) Serikali ya CCM Ikavamia na Kupora Kijambazi kwa Kutumia Polisi Computer zaidi ya 60 za Ukawa za Vijana waliokuwa wakisaidia Kujumisha matokeo ya Kura za Urais Kuharibu Ushahidi wa Matokeo, Ikauma sana, Ukawa Wakakumbatia amani.

4) CCM wakitumia Dola Wakafuta Matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar ambapo Maalim Seif Alishinda, na Hapo Pia Ukawa Wakakumbatia Amani.

5) CCM wakitumia Vibaraka wao wakajaribu sana Kuiba Umeya wa Majiji ambayo Ukawa walishinda kwa Kutumia mbinu chafu sana na za Kutia aibu, Ukawa wakakumbatia amani, wakadai haki kwa Uvumilivu.

6) Akauawa Kiongozi wa Ukawa Alphozo Mawazo, CCM na Mapolisi wao wakazuia Mazishi, Ukawa wakakumbatia amani wakatafuta haki mahakamani, Kuzika Mfu wao, hujuma gani hii aibu gani hii?

Alivyokufa Mawazo


Na sasa Utawala Huu wa awamu ya Tano,

1) CCM Kwa Unafiki Mkubwa bungeni kwa Maagizo ya Serikali, wakazuia Matangazo ya Mojakwa moja ya Bunge Kwa Lengo chafu, La Kuzuia a)Uonevu Bungeni dhidi ya Ukawa Usionekane b)Vitisho vya CCM na Zomea zomea na Kejeli za CCM dhidi ya Ukawa Visionekane 3)Michango na Umahiri wa wabunge wa Ukawa Usionekane.

Serikali Kuleta Polisi Bungeni,


2) Ukawa wakaletewa Polisi na Mbwa Kupigwa Bungeni, Wakakumbatia amani.
3) Wabunge maarufu wa Ukawa Pamoja na Zitto Kakwe wakafungiwa. Pamoja na Kukamatwa na Kufuunguliwa Mashitaka ya Hovyo.
4) Magufuli Kuwaagiza Polisi wawanyamazishe Wabunge wa Upinzani wasifanye Mikutano au hata Makongamano ya ndani (Kama hajawatuma Mbona hawazuii) Wakati yeye na Wanaccm wenzake wakiendeleza siasa zao katika kila walifanyalo
5) Kejeli za Rais dhidi ya Viongozi wa Ukawa mfano alivyohoji iwapo meya wa jiji anapenda ujambazi?
6) Kukamatwa ovyo kwa Viongozi wa Ukawa hasa Vijana kuwatia hofu.
7) Kuzuia Sherehe za Wavyuo wa Chadema kwa Mabomu, Ingawa Sherehe kama Hizo zilifanywa na Wanavuo wa CCM Na Kufanana Kwa Kila hali Kimazingira na Maudhui.


Hawa hawakukguswa


Hawa wakapigwa mabomu

8) Waliomtukana Mgombea matusi hata ya Kumkejeli Mungu Mwenyewe wakati wa Kampeni eg. Nape Mnauye wakapewa Uwaziri na Mh. Magufuli, lakini Wasio CCM hata facebook zao zinaingiliwa na akisema mtu kinyume na Mh Magufuli anashitakiwa, Yako wapi Mashitaka ya waliosema Lowassa Kajinyea. Nikisema hivyo Juu ya Rais Leo Nashitakiwa!

Mimi Nadhani, Ni wakati sasa Ukawa Kuwaonyesha CCM sasa Basi, Kwa sababu Uzalendo wenu, Kupenda kwenu Kuchagua amani CCM wananusa Kuwa Ni Udhaifu. Na zaidi sana Msipovumilia tena, Watanzania waliowengi watawaelewa, Dunia Itawaelewa. Mmeonewa sana, Mmehujumiwa sana, Mmedhalilishwa sana. Na Ukweli wanaofanya hivyo sio kwamba wanayonguvu ya Kuzima Nguvu za Umma walio nyuma yenu, Wanakesha na Kuomba Muendelee Kutishika. Maana Siku Mkionyesha sasa Basi, Hakika ndipo mtajua hawa ni Chui wa Karatasi. Na kwa Kuwa hamdai Jambo Kubwa, Hamdai Kupindua serikali, Bali Mnadai Uhuru wa haki zenu za Kikatiba, Watakuwa na Wazimu Kuendelea na Tabia hii ya Kihuni wakiamini kuwa wataweza Kuliongoza Taifa. Baada ya Kenyata Kuteswa Kufungwa na Kuteswa alisema Maneno haya, "It is by our action that they will know that we mean business"



Kituko, Kioja wanachokifanya CCM, Ni Mithili ya Bondia Hayawani anayejitangazia Umahiri, halafu kwa kujuana na Refa, wanamfunga Bondia Mpizani, Mikono na Miguu hata asiweze Kujigeuza, Halafu Filimbi inapigwa, Bondia hayawani huyu anamvamia Bondia aliyefungwa Mikono na Miguu, anampiga Kila mahali hata chini ya Mkanda, Na refa asiye na aibu baada ya Kipenga cha Mwisho anamnyanyua Hayawani huyu Mkono Kuwa Kashinda, Ndio Mazingira wanayojijengea CCM na Magufuli 2020. Hili likitokea Uwanjani kweli mawili watazamaji watatoka nje, na wale wakali wasiovumilia upuuzi watampiga mawe na chupa za maji na za soda. Na wote watakuwa wamefanya sawa. Kama hili halifai Katika Michezo Livumiliweje Katika Demokrasia na Uhuru wa nchi yetu.

Ninavyosema kuwe na action sisemi kuvuruga amani? Na Nipo Tayari Kujibu Mahakama yoyote. Ila Naona Kuwa Muda Umefika wa Kupuuza Amri zilizokinyume na Katiba na Sheria. Ifike wakati Serikali ya CCM wakikataza Mikutano kwa Kutumia Polisi Basi Ukawa wafanye Mikutano Kwa Nguvu. Na kama Polisi wakija Kuvuruga amani na Kuwapiga wananchi, Basi Wananchi wajihami dhidi ya Uhalifu huo. Itakuwa Unafiki sana CCM Iliyowasaidia ANC, na FRELIMO Kupambana na Uonevu na Ubeberu leo wanafanya Ubeberu ule ule na Kuzidi dhidi ya Raia wanzao. This Must end. Kwa Wenye Hekima, in a long run huu upuuzi utaathiri sio tu Ukawa, bali Utaleta hasara kubwa sana, Kabisa! Kwa Taifa zima ikiwepo na CCM kama chama. Tabia hizi za Kijinga zitaangamiza maendeleo ya Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa, au hata Kutufikisha katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

It is very true.

Zipo kila dalili kuwa serikali hii ya awamu ya 5 inafanya kila njia kuirejesha nchi hii kwenye mfumo wa Chama kimoja.

Hebu nitaje mifano michache ya kuthibitisha hoja yangu.

1. Bunge ambalo kazi yake kubwa ni kuisimamia serikali, limegeuzwa kuwa kama vikao vya NEC ya CCM........

2. Wakati Ibara ya 3 ya Katiba ya nchi inaeleza wazi kuwa nchi hii itakuwa ya mfumo wa vyama vingi, Mkuu wa nchi ameamua kuivunja Katiba ya nchi waziwazi kwa kutangaza hadharani kuvipiga marufuku vyama vya siasa vya upinzani kutofanya shughuli zozote za kisiasa hadi mwaka 2020, wakati chama chake cha CCM akikiruhusu kuendelea na shughuli za kisiasa bila kubughuziwa na Polisi.

3. Rais kufanya teuzi zake mbalimbali za kazi za utumishi wa Umma kwa makada wa CCM pekee, ambapo huo ni ubaguzi mbaya mno kwa nchi ambayo ipo kwenye mfumo wa vyama vingi.

4. Watendaji wengi wa serikali kufanya kazi zao kwa maelekezo ya Lumumba....

Matokeo ya nchi kuendeshwa kwa fikra za mtu mmoja pekee, kutaisababisha nchi hii kuingia kwenye matatizo makubwa huko mbele ya safari.........

Kwa hiyo ni muhimu watanzania wote tukapaza sauti zetu kwa nguvu zetu zote na kuwaeleza watawala wetu kuwa nchi hii inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu........

Tujikumbushe pia maneno ya hekima aliyowahi kuyatoa Mwalimu Nyerere aliposema kuwa Rais ambaye anaisigina Katiba ya nchi ambayo ndiyo sheria mama, Katiba ambayo aliapa kuitii na kuiheshimu, Mwalimu alibainisha wazi kuwa Rais wa aina hiyo hatufai..................
 
Kwa akili hizi za vijana wa ukawa ni hakika bila shaka kuwa taifa linaangamia. Ni akili zenye ubongo ulioganda, akili zisizoweza kubaini jambo na kutofautisha mema na mabaya full kulialia upuuzi na upumbafu. Ee Mungu linusuru taifa letu na hiki kizazi kilichopotoka kwa kuziuisha akili na fahamu zao na kukiponya.
Usiwalazimishe watu kuwa million saba.
Unapodai wanalialia unataka wafanyeje kama maudhi mnafanya kwa kushirikiana na dola ?! Wakireact hapo unazungumzia vita unapenda hiyo ?! Tunanafasi ya kufanya mageuzi ya ki demokrasi kwa AMANI.

Unadai UKAWA hawawezi kuongoza nchi umewapima kwa kigezo kipi ?! CCM miaka 55 Tz iko nyuma kuliko unavyodhani , Jaribu kutembelea nchi zingine uone tofauti ndio urudi humu Jf ku comment
 
Mara nying watz hatuna uthubutu. Tunapenda kuishi kwa shida miaka yote.badala ya kudadili maisha kwa tabu ya japo mwaka mmoja than tuandaye kizaz kijacho chenye raha. Mmea ili uzae matunda meng lazma ufe kwa kupandwa. We have to die for our nation!!
 
Samia na upinzani
Akizungumza kwenye kikao na viongozi wa CCM wa mkoa, Samia alisema katika kipindi cha miaka 20 tangu siasa za vyama vingi ziliporejeshwa, vyama vya upinzani vimejijenga na sasa vinaweza kukabiliana na Serikali.

“Bila kusahau kwenye Bunge tuna wenzetu kutoka vyama vya upinzani ambao wamekua vya kutosha, wamepevuka vya kutosha,” alisema Makamu wa Rais.

“Katika miaka 20 ya vyama vingi, upinzani umezalisha watu makini ambao wako tayari kupambana na Serikali. Je, wa kwetu tumewaandaaje katika kupambana nao?”
Umempatia nukuu sahihi maana hawezi kuelewa mpaka mkubwa wao aseme.
 
Nijaribu Kueleza Kwa Kifupi sana, Hujuma Kubwa sana ya Kisiasa, Iliyofanywa na Inayoendelea Kufanywa na CCM dhidi ya UKAWA Tangu Kabla ya Uchaguzi wa 2015, Wakati wa Uchaguzi na Hadi sasa.

Matendo ya CCM wakati Ule yalionyesha Jinsi ambavyo walijua wazi Kuwa hawawezi kuishinda Ukawa Kihalali, Na Hata sasa Matendo yao Ya Hujuma chafu sana na Za Aibu, Za Fidhuli na Jesuri, Zinaonyesha Wanafahamu hawakushinda Kihalali na Wanahofu Kubwa sana Juu ya Ukawa.

Hujuma Chafu za CCM Kabla na Baada ya Uchaguzi.

1) Wakati CCM wakilikuwa wamefanya Ufunguzi wa Kampeni zao Jangwani bila ya Kubugudhiwa na Yeyote, CCM wakitumia Vibaraka Wao walijaribu sana Kuwazuia Ukawa wasitumie Uwanja wa Jangwani, Wazalendo, Wapenda amani Wa Ukawa wakajitahidi sana Kutafuta haki ya Kutumia uwanja Ule Kwa amani bila fujo.

2) Wakati wa Upigaji Kura CCM wakitumia Dola wakakataza Ukawa wasikae mita 200 Kulinda kura, na Pia Wakawazuia wengi wa Mawakala wao Kuingia vituo vya kuhesabia Kura, Ukawa Wakakumbatia amani.

3) Serikali ya CCM Ikavamia na Kupora Kijambazi kwa Kutumia Polisi Computer zaidi ya 60 za Ukawa za Vijana waliokuwa wakisaidia Kujumisha matokeo ya Kura za Urais Kuharibu Ushahidi wa Matokeo, Ikauma sana, Ukawa Wakakumbatia amani.

4) CCM wakitumia Dola Wakafuta Matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar ambapo Maalim Seif Alishinda, na Hapo Pia Ukawa Wakakumbatia Amani.

5) CCM wakitumia Vibaraka wao wakajaribu sana Kuiba Umeya wa Majiji ambayo Ukawa walishinda kwa Kutumia mbinu chafu sana na za Kutia aibu, Ukawa wakakumbatia amani, wakadai haki kwa Uvumilivu.

6) Akauawa Kiongozi wa Ukawa Alphozo Mawazo, CCM na Mapolisi wao wakazuia Mazishi, Ukawa wakakumbatia amani wakatafuta haki mahakamani, Kuzika Mfu wao, hujuma gani hii aibu gani hii?

Alivyokufa Mawazo


Na sasa Utawala Huu wa awamu ya Tano,

1) CCM Kwa Unafiki Mkubwa bungeni kwa Maagizo ya Serikali, wakazuia Matangazo ya Mojakwa moja ya Bunge Kwa Lengo chafu, La Kuzuia a)Uonevu Bungeni dhidi ya Ukawa Usionekane b)Vitisho vya CCM na Zomea zomea na Kejeli za CCM dhidi ya Ukawa Visionekane 3)Michango na Umahiri wa wabunge wa Ukawa Usionekane.

Serikali Kuleta Polisi Bungeni,


2) Ukawa wakaletewa Polisi na Mbwa Kupigwa Bungeni, Wakakumbatia amani.
3) Wabunge maarufu wa Ukawa Pamoja na Zitto Kakwe wakafungiwa. Pamoja na Kukamatwa na Kufuunguliwa Mashitaka ya Hovyo.
4) Magufuli Kuwaagiza Polisi wawanyamazishe Wabunge wa Upinzani wasifanye Mikutano au hata Makongamano ya ndani (Kama hajawatuma Mbona hawazuii) Wakati yeye na Wanaccm wenzake wakiendeleza siasa zao katika kila walifanyalo
5) Kejeli za Rais dhidi ya Viongozi wa Ukawa mfano alivyohoji iwapo meya wa jiji anapenda ujambazi?
6) Kukamatwa ovyo kwa Viongozi wa Ukawa hasa Vijana kuwatia hofu.
7) Kuzuia Sherehe za Wavyuo wa Chadema kwa Mabomu, Ingawa Sherehe kama Hizo zilifanywa na Wanavuo wa CCM Na Kufanana Kwa Kila hali Kimazingira na Maudhui.


Hawa hawakukguswa


Hawa wakapigwa mabomu

8) Waliomtukana Mgombea matusi hata ya Kumkejeli Mungu Mwenyewe wakati wa Kampeni eg. Nape Mnauye wakapewa Uwaziri na Mh. Magufuli, lakini Wasio CCM hata facebook zao zinaingiliwa na akisema mtu kinyume na Mh Magufuli anashitakiwa, Yako wapi Mashitaka ya waliosema Lowassa Kajinyea. Nikisema hivyo Juu ya Rais Leo Nashitakiwa!

Mimi Nadhani, Ni wakati sasa Ukawa Kuwaonyesha CCM sasa Basi, Kwa sababu Uzalendo wenu, Kupenda kwenu Kuchagua amani CCM wananusa Kuwa Ni Udhaifu. Na zaidi sana Msipovumilia tena, Watanzania waliowengi watawaelewa, Dunia Itawaelewa. Mmeonewa sana, Mmehujumiwa sana, Mmedhalilishwa sana. Na Ukweli wanaofanya hivyo sio kwamba wanayonguvu ya Kuzima Nguvu za Umma walio nyuma yenu, Wanakesha na Kuomba Muendelee Kutishika. Maana Siku Mkionyesha sasa Basi, Hakika ndipo mtajua hawa ni Chui wa Karatasi. Na kwa Kuwa hamdai Jambo Kubwa, Hamdai Kupindua serikali, Bali Mnadai Uhuru wa haki zenu za Kikatiba, Watakuwa na Wazimu Kuendelea na Tabia hii ya Kihuni wakiamini kuwa wataweza Kuliongoza Taifa. Baada ya Kenyata Kuteswa Kufungwa na Kuteswa alisema Maneno haya, "It is by our action that they will know that we mean business"



Kituko, Kioja wanachokifanya CCM, Ni Mithili ya Bondia Hayawani anayejitangazia Umahiri, halafu kwa kujuana na Refa, wanamfunga Bondia Mpizani, Mikono na Miguu hata asiweze Kujigeuza, Halafu Filimbi inapigwa, Bondia hayawani huyu anamvamia Bondia aliyefungwa Mikono na Miguu, anampiga Kila mahali hata chini ya Mkanda, Na refa asiye na aibu baada ya Kipenga cha Mwisho anamnyanyua Hayawani huyu Mkono Kuwa Kashinda, Ndio Mazingira wanayojijengea CCM na Magufuli 2020. Hili likitokea Uwanjani kweli mawili watazamaji watatoka nje, na wale wakali wasiovumilia upuuzi watampiga mawe na chupa za maji na za soda. Na wote watakuwa wamefanya sawa. Kama hili halifai Katika Michezo Livumiliweje Katika Demokrasia na Uhuru wa nchi yetu.

Ninavyosema kuwe na action sisemi kuvuruga amani? Na Nipo Tayari Kujibu Mahakama yoyote. Ila Naona Kuwa Muda Umefika wa Kupuuza Amri zilizokinyume na Katiba na Sheria. Ifike wakati Serikali ya CCM wakikataza Mikutano kwa Kutumia Polisi Basi Ukawa wafanye Mikutano Kwa Nguvu. Na kama Polisi wakija Kuvuruga amani na Kuwapiga wananchi, Basi Wananchi wajihami dhidi ya Uhalifu huo. Itakuwa Unafiki sana CCM Iliyowasaidia ANC, na FRELIMO Kupambana na Uonevu na Ubeberu leo wanafanya Ubeberu ule ule na Kuzidi dhidi ya Raia wanzao. This Must end. Kwa Wenye Hekima, in a long run huu upuuzi utaathiri sio tu Ukawa, bali Utaleta hasara kubwa sana, Kabisa! Kwa Taifa zima ikiwepo na CCM kama chama. Tabia hizi za Kijinga zitaangamiza maendeleo ya Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa, au hata Kutufikisha katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Your right brother, its true inabidi ukawa waseme basi najua watakufa baadhi ya watu lkn watakumbukwa kwa kuiokoa Tanzania na ndg zao. CCM wanatumia uoga wa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani ambao bila shaka wapo wanaoshirikiana na serikali ya CCM. Kuinufaisha baadhi ya viongozi wa CCM na serikali yao kwa kuhongwa ili wasiwape wafuasi wao nguvu ya kudai haki yao.

Nionavyo mimi kama mwenyekiti wa CHADEMA atashindwa kuwaongoza wanachama wa CHADEMA kudai haki yao inayozuiwa kwa maksudi na CCM kwa kushirikiana na polisi,aachie ngazi ili mwenyekiti wapewe watu Wenye uwezo wa kudai haki kwa kushirikiana na wananchi wao. Tumechoka na uoga wa mbowe. Tunawataka akina List,Lema, Msigwa, Heche ambao hawataogopa kulala keko pmj na wanachama wao. Akikamatwa Lema au Lisu nasi wanachama tutakuwa nyuma yao hata kwa kupigana na mapolisi CCM hata kama magereza yakijaa ni sawa. Kama Amani wanachadema na ukawa wanaongoza kwa kulinda amani. Ni ukweli bila chenga kuwa KWA SASA WAPINZANI, UKAWA KUSEMA BASI KAMA AMANI KUVUNJIKA ACHA IVUNJIKE
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom