List of Rostam and Akram Aziz companies & Mohamed Enterprises

Si maskini wa pesa tu bali hata roho zao.

Watu wanatakiwa waamke na kuchanganya bongo zao jinsi gani wataweza kufanikiwa katika biashara na mambo mengine ya kiuchumi. baadhi ya watu wamekalia maneno mengi lakini hawana mikakati ya kufanya kweli na kulinda mafanikio yao.

Yesir na Pundamilia,

Ni ukweli usiopingika kwamba wengi wanaoguswa na ufisadi wa RA na wengineo ni masikini. Mimi nashukuru Mungu sio masikini lakini naishi kwa kipato changu halali na nimepata nafasi ya kujua kwa nini Watanzania walio wengi ni masikini ndio maana niko mstari wa mbele kupigia kelele ufisadi.

Sijui kama kuna mwana JF yeyote asiyejua kwamba Rostam ni fisadi aliyekubuhu na hili hakuna anayepashwa kuja hapa kutaka tutoe ushahidi. Wanamtetea Rostam basi wamwanbie aende mahakamani akawashtaki wale waliomwita fisadi hadharani kama Dr. Slaa na Mzee Mengi. Hiyo ya kuja hapa na kutaka mchangiaji aje na data/takwimu za watanzania wanaomchukia rostam ni hoja inayolenga kutoa nje ya mada iliyo mbele yetu.

Twambie uhusiano uliopo kati ya RA na Mohamed Enterprise basi!!!!! Mengine ya kuchukua neno moja la mchangia hoja na kulisimamia kidete, ni kutaka kupotosha hoja.

Tiba
 
Kwakweli binafsi naona tumwache rostam ale nchi! Hakumforce kiongozi wa serikalini yoyote kumpa tenders, tax exemptions etc etc...he is just a businessman..a connected one too...ccm needed to loot the central bank , he took the risks for them ..sasa anakula matunda...if we wanna point fingers kwa sasa naona tuibane serikali tuu...
 
Kwakweli binafsi naona tumwache rostam ale nchi! Hakumforce kiongozi wa serikalini yoyote kumpa tenders, tax exemptions etc etc...he is just a businessman..a connected one too...ccm needed to loot the central bank , he took the risks for them ..sasa anakula matunda...if we wanna point fingers kwa sasa naona tuibane serikali tuu...

Lengo letu kuu ni kuibana serikali lakini ili uweze kuibana serikali vizuri lazima ujue network ya watu wote wanaonufaika na huu wizi. Maana tumeshachoka kupakwa matope, Kwahiyo tatizo sio RA tu bali tunapenda tujue washirika wake katika huu umafya mbali ya wanasiasa.
 
Njia rahisi na yenye maslahi kwa nchi na kizalendo ni mahakamani kama una ushahidi zaidi ya hapo umeingia mkenge labda uanze kutafutwa wewe kwa kupotosha ummah

unajua kwamba mtu anaweza kuushitaki mtandao wa jamii mahakama ikaamuru mawasiliano yako na taarifa zako zingine zitolewe kwa maslahi ya nchi ?? Unajua kwamba hilo linawezekana ?

Ndio utajua kwanini hizi chat huwa zina printiwa na kupelekwa kwa wenyewe wazisome

nenda kawatishe vikaragosi wa ufisadi; anayetaka kujua tunachoandika aombe nakala wala asihangaike kusubiri kuprintiwa! Wanafikiri wanaishi katika nchi ya mabwege!? Tena hivi ndio mnanitia hasira kweli kupigana mikwara mbuzi utadhani tuko shule ya msingi.. "nitakuandika jina ka kupiga kelele darasani".. !

Waambie wakatishane wao na wake zao vyumbani mwao!
 
Mkuu FMES,

Heshima mbele umekuwa mtu mzuri ku-motivate wadau waweze kutoa data wanazo jua zaidi kuhusu Rostam unfortunately wameendelea kukuangusha. Maana hawana la zaidi.

Ati Rostam anajificha kwa METL, kwani METL ni nani? yeye hawezi hukumiwa mwenyewe au kwa vile anafadhili vilabu vya mpira.

Kweli vita yetu ya Ufisadi imekosa dira, nadhani sasa hatui hata tunachofanya. Hakuna kitu rahisi kama kushitaki kampuni, loophole rahisi sana ni kuchukua tu wale wenzetu wa TRA kuangalia kama kodi zinalipwa kama hazilipwi tunawabana hapo hapo.

Cha kusikitisha tunabwatuka tu huku kwenye mitandao bila kuwa na lolote jipya.

- Mkuu Kasheshe heshima yako bro, ninakusikia sana, unayoyasema ni kweli sana ukizingatia kwamba DK. Hosea ni wakala wa Rostam, na the fact kwamba hakuna kiongozi yoyote aliyeteuliwa na rais katika miaka miaka mitatu ya mwanzoni ya utawala wake bila kupitishwa na Rostam kwanza, sio tatizo kuelewa ni kwa nini ushahidi unakuwa mgumu sana kuupata.

- Lakini sasa hivi kwa wale kama mimi tunaoamini kwamba mikono ya Rostam imejaa ufisadi, hatuna wasi wasi naye kwa sababu tunajua kwamba ushirika wa mafisadi haudumu, hivi miaka mitatu iliyopita ulitegemea kwamba tutawafikisha mafisadi hapa walipo yaani njia panda?

- Rostam amekwua mjanja na kubadili sana majina ya umiliki wa kampuni zake, lakini leo wametokea watu kama Leokweli, wametafuta mpaka kupata baadhi ya majina ya kampuni anazozimiliki kwa ujanja ujanja, huu kwetu ni mwanzo mzuri sana, na huku tukipigiwa kelele za malngo na watu makini kama wewe, inatusaidia sana kwanza kuwa makini na quality ya ushahidi tunaoutafuta, Mzee Mengi ameanza kuweka msingi na sasa pole pole tunawasogelea, ingawa ni safari ndefu sana, lakini hatuwezi kurudi nyuma, na tuna shukuru kwamba tuna watu kama wewe wa always kutukumbusha kwamba we need to work hard,

- Wewe na baadhi ya wenzako wengine mmekuwa so far a very good motivation katika vita hii ya ku-deal na mafisadi hasa Rostam, keep it up mkuu!

FMES!
 
Si mungeshika hiyo kampuni mpaka sasa mwasubiri nini?

Thubutu, nani aishike hiyo kampuni wakati nchi mikononi mwake (RA). Ingekuwa hivyo wahusika wa Kagoda wangekuwa wamefikishwa mahakamami, maana pesa wamerudisha na bado inadaiwa eti wahusika hawajulikani, hii ndo TZ ya wadanganyika.
 
Thubutu, nani aishike hiyo kampuni wakati nchi mikononi mwake (RA). Ingekuwa hivyo wahusika wa Kagoda wangekuwa wamefikishwa mahakamami, maana pesa wamerudisha na bado inadaiwa eti wahusika hawajulikani, hii ndo TZ ya wadanganyika.

1-Kwanza angeanzia hapa:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/29053-rostam-katika-tope-jipya-2.html

2- Hiyo barua ya CAG (japo ni ya mwaka 2000) inahoji kuibuka kwa RA katika biashara ya mahindi wakati hakuna jina lake katika mkataba. Ukweli ni kwamba nina ushahidi kwamba hata huyo Mohamed Enterprises kaingizwa mkenge na RA na amepata hasara na amewaingiza mkenge wengi wakiwami waasia wenzake na hata ndugu zake. Iko siku mutasikia tu. Katika hili ndio mujue staili ile ile ya Kagoda (EPA-2005) na Afritainer (EPA-2000). Miaka yote hiyo ni ya uchaguzi, ambayo uroho wa madaraka na tena baada ya kifo cha Mwalimu Nyerere, ndio wanasiasa wetu wakawa waroho wa madaraka na wakasahau utaifa wao.

3- Angalia thread zote za nyuma na kwa kukurahishia angalia Raia Mwema

Siri mpya ya EPA yaiumbua Kagoda

Kampuni ya Afritainer ni ya Rostam na hao waliotajwa ni watumishi wake. Nasikia anasema "EPA hiyo ya kwanza nilifanya clean deal" akiulizwa na Kagoda je? anakuwa bubu. Moja ya kampuni zilizotajwa hapo juu ya ATD ndiyo kampuni ya asili ya familia ya RA, nayo inahusika katika mambo mengi ambayo siku si nyingi mutayasikia, lakini kwa ufupi namba za simu na fax za KAgoda na Afritainer zilikuwa za kampuni hiyo ya ATD.


Kampuni ya Afritainer ilifanikiwa kuchota zaidi ya Shilingi bilioni 12 za EPA kwa kutumia nyaraka zilizosainiwa na watumishi wa kampuni moja maarufu ya Dar es Salaam (jina tunalo) wakidaiwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo kabla ya kufahamika kwamba hawakuwa wakurugenzi halali kisheria.

Kagoda, ambayo ilitumia nyaraka za kughushi, ilichotewa mabilioni hayo ya fedha kabla haijasajiliwa na katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi zinazoonyesha watu waliorejesha fedha za EPA kwa jina la Kagoda pamoja na kuwapo taarifa za uhakika kuhusiana na wafanyabiashara wazito waliorejesha fedha hizo kwa nyakati tofauti kabla ya muda uliowekwa kwisha Oktoba 31, 2008.

Nyaraka zilizotumiwa na Afritainer kuchota mabilioni ya fedha za EPA mwaka 2000 zinaonyesha kwamba kampuni hiyo imetumia namba za simu 2861371 na 2861372 ambazo pia ndizo zimetumiwa na Kagoda katika kuchota fedha za EPA mwaka 2005. Namba hizo zinaonekana katika nyaraka za kampuni nyingine yenye uhusiano na wamiliki wa Afritainer.

Nyaraka kutoka Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) zinaonyesha kwamba Tabu Omari Masula na Barati A. Goda, walidaiwa kuingizwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo Mei 15, 2000 kinyume cha sheria.

Barua ya BRELA ya Februarin 18, 2002, miaka miwili baada ya Tabu na Barati kuchota fedha za EPA, ilieleza kwamba wakurugenzi hao hawakuwa halali kutokana na kutokuwa na hisa katika kampuni ya Afritainer.

Kwa mujibu wa barua hiyo kwenda kwa kampuni ya mawakili ya M.A.Imail, Tabu na Barati walikiuka kifungu cha 50 cha hati ya usajili ya kampuni hiyo kinachomlazimu mkurugenzi kuwa na hisa katika kampuni kwanza ili aweze kuwa na maamuzi.

Waraka wa Afritainer uliowasilishwa BRELA Mei 15, 2000, ulieleza kwamba wakurugenzi pekee na waazilishi wa Afritainer ni Bahram Abdurasul Chakaar na Gulam Abdurasul Chakaar, wamejiuzulu ukurugenzi na kuwaachia Tabu na Barat.

Hata hivyo, BRELA katika barua ya Februari 18, 2002 iliyoandikwa na Msajili Msaidizi wa wakala huo, L. Kimaro, ilieleza wazi kwamba hadi wakati huo ubadilishaji wa wakurugenzi haukuwa umeidhinishwa kutokana na kutokufuata masharti ya usajili.

Tabu anatajwa kufanya kazi katika kampuni moja ya jijini Dar es Salaam yenye ofisi zake eneo la viwanda barabara ya Nyerere na Upanga.

Kwa mujibu wa habari ambazo Raia Mwema imezipata fedha hizo kiasi cha Sh. Bilioni 13 zilichukuliwa Agosti 2000 kabla ya uchaguzi wa pili wa vyama vingi ambao Benjamin Mkapa aligombea tena urais.

Afritainer ni ya ndugu zake Rostam Bahram Abdurasul Chakaar na Gulam Abdurasul Chakaa na waliopewa hisa ni watumishi wa Caspian Tabu Omari Masula na Barati A. Goda

https://www.jamiiforums.com/jamii-i...a-agriculture-ltd-another-bot-scandal-33.html



 

Attachments

  • 2879d1226673134-kagoda-agriculture-ltd-another-bot-scandal-nyaraka.jpg
    2879d1226673134-kagoda-agriculture-ltd-another-bot-scandal-nyaraka.jpg
    158.7 KB · Views: 72
Mtu aliyeziba macho hata ukimuwekea taa usoni atapata mwanga kwenye ubongo wake na anatajua kuna mwanga mbele yake lakini ataendelea kubisha kuwa bado ni giza!
 
Hivi we SHY unajua unachokiongea kweli wewe??? Mbona unaleta vichekesho visivyo na maana hapa,, kama unaona huna points za kuongea kaa pembeni angalia watu wanavyotoa maoni yao sio kukurupuka kuandika tu au unataka uongeze idadi ya post???

Shame on u

ANAJUA anachokiongea lakini HAJUI ANACHOKIONGEA.
 
this is pure racism.. hamna mengi,lowassa,hata huyo kikwete mwenyewe.watu wakiona muarabu kafanikiwa,wao ni 'ufisadi' tu. mimi ni mwarabu,na familia yetu ina hela siziso za kifisadi ila watu wakiona tuna magari mapya,ni hayo hayo maneno ya 'kifisad,kifisadi'

Hujaulizwa wewe ni nani na wala watu hawahitaji kujua wewe ni nani. Mawazo yako ndiyo yanayopimwa na kujua wewe ni nani.

Usituambie familia yenu wana pesa, inawezekana unafanya kazi ya UYAYA katika nyumba ya chandra (msafisha kinyesi cha watoto) ila kwa kuwa wamekudanganya kwa kukupa fursa utmie internet kwa maslahi yao na wewe unajiona wa maana.

Wangapi wanamagari mapya na hawaitwi mafisadi?
 
hawa ccm kwa u2mbo walioufanya awamu hii wamenifanya na mimi 2010 nifikirie kupiga kura hata kwa upinzani ingawa hata upinzani una9ingua 2
 
Mirambo pia..

Unamaanisha 50Milambo zilipo ofisi zake? 50Milambo linamilikiwa na chama cha ANC, Afrika ya kusini. Nyerere aliwapatia hicho kiwanja ili wapate source of income wakati wa kutokomeza apartheid.

Vp kuhusu Kagoda, Dowans na Richmond, mbona hazimo kwenye list?
 
"Nina uhakika Wembere Hunting Safari company na Tanzania Packages Manufacturing Co haipo kwenye tovuti ya bunge "

Na sasa Channel Ten...

C:rolleyes: Wadau CV ya Mheshimiwa Rostam Aziz (MB) kama inavyoonekana katika Tovuti ya Bunge hiyo hapo.
Hon Rostam A Aziz (MP) Igunga CV as posted on the Parliament Website.
GENERAL
Salutation Honourable Member picture


First Name: Rostam
Middle Name: Abdulrasul
Last Name: Azizi
Member Type: Constituency Member
Constituent: Igunga
Political Party: CHAMA CHA MAPINDUZI
Office Location: P.O. Box 11, Igunga
Office Phone: +255 754 555555
Ext.:
Office Fax:
Office E-mail: raziz@parliament.go.tz

Member Status: Current Member
Start Date: 28 December 2005
End Date: 30 August 2010
Date of Birth 31 December 1969
EDUCATIONS
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
- BA (Economics) GRADUATE
CERTIFICATIONS
Certification Name or Type Certification No. Issued Expires
No items on list

EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
Research on Business Managing Director
Africa Trade Development Director
Africa Tanneries Ltd. Director
Tanzania Leather Industries Ltd Director
Caspian Construction Ltd Director
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
No items on list

PUBLICATIONS
Description Published Date
No items on list

SPECIAL SKILLS
Skill Name or Description Years Experience Acquired Through Skill Level
No items on list

RECOGNITIONS
Recognition Type Recognition Date Reason Action Taken Issued by
No items on list
 
Yesir na Pundamilia,

Ni ukweli usiopingika kwamba wengi wanaoguswa na ufisadi wa RA na wengineo ni masikini. Mimi nashukuru Mungu sio masikini lakini naishi kwa kipato changu halali na nimepata nafasi ya kujua kwa nini Watanzania walio wengi ni masikini ndio maana niko mstari wa mbele kupigia kelele ufisadi.

Sijui kama kuna mwana JF yeyote asiyejua kwamba Rostam ni fisadi aliyekubuhu na hili hakuna anayepashwa kuja hapa kutaka tutoe ushahidi. Wanamtetea Rostam basi wamwanbie aende mahakamani akawashtaki wale waliomwita fisadi hadharani kama Dr. Slaa na Mzee Mengi. Hiyo ya kuja hapa na kutaka mchangiaji aje na data/takwimu za watanzania wanaomchukia rostam ni hoja inayolenga kutoa nje ya mada iliyo mbele yetu.

Twambie uhusiano uliopo kati ya RA na Mohamed Enterprise basi!!!!! Mengine ya kuchukua neno moja la mchangia hoja na kulisimamia kidete, ni kutaka kupotosha hoja.

Tiba

Tiba,
Sitaweza kula pini wakati nikijua kuwa thread hii imebeba maneno ambayo siyo sahihi, na nimeona hivyo nikatoa angalizo kwa aliyeanzisha thread hii lakini ameona kuwa hana haja ya kuwa mkweli katika bandiko lake. Sasa kwa sisi tunaotaka kuona mambo yanakwenda kwa kuzingatia taarifa sahihi siwezi kuona kama hii thread ina maana yeyote zaidi ya kutaka kuendelea kumwongelea Ra bila ya kuwa na ushahidi wa kutosha, unamwita fisadi then huna ushahidi, ndiyo unakuwa umefanikisha nini?

Kasheshe amesema kuwa hili suala la ufisadi hapo JF limekwisha poteza dira, sasa ni juu yenu kugeuka na kuangalia ni kwa kiasi gani inawezeana kuwa ni kweli dira imepotea. Kwa mfano kuendelea kumwongelea RA bila ya ushahidi kwa mtazamo uliosahihi ni upotevu wa mwelekeo hapa jamvini.

Vita hivi si vya kuelekezwa kwa RA elekezeni kuona ni jinsi gani mtapambana na UFISADI kwa maana ya mfumo, then matokeo yake ni obvious yata-deal na wahusika ambao kimsingi ni wengi sana na wengine huenda labda wewe ni fisadi pia.
 
Kwakweli binafsi naona tumwache rostam ale nchi! Hakumforce kiongozi wa serikalini yoyote kumpa tenders, tax exemptions etc etc...he is just a businessman..a connected one too...ccm needed to loot the central bank , he took the risks for them ..sasa anakula matunda...if we wanna point fingers kwa sasa naona tuibane serikali tuu...

Mkuu Kapinga,
Mimi ninakubaliana kabisa na wewe. Hatuwezi kufanikiwa lolote katika vita hii kama tutaacha kwa makusudi kuushambulia mfumo wa UFISADI na badala yake tukazane kupoteza nguvu nyingi kwa RA. Mafisadi ni wengi sana kwa style hii ya kwenda kwa mtu na mtu tutakesha. Leo akiondoka RA tutakuwa tumemaliza tatizo? au tutatafuta mwingine twende nae weee ilhali kunarundo kubwa n awengine wanazaliwa kila kukicha. We need to objective and strategic.
 
jamani serikali imejitoa kwenye biashara, hilo halina majadala, pengine nieleweshwe kama na wananchi wametakiwa wajitoe kwenye huo mhimili muhimu wa uchumi kwa ustawi wa maendeleo ya nchi.
 
Back
Top Bottom