Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,604
- 3,163
Si maskini wa pesa tu bali hata roho zao.
Watu wanatakiwa waamke na kuchanganya bongo zao jinsi gani wataweza kufanikiwa katika biashara na mambo mengine ya kiuchumi. baadhi ya watu wamekalia maneno mengi lakini hawana mikakati ya kufanya kweli na kulinda mafanikio yao.
Yesir na Pundamilia,
Ni ukweli usiopingika kwamba wengi wanaoguswa na ufisadi wa RA na wengineo ni masikini. Mimi nashukuru Mungu sio masikini lakini naishi kwa kipato changu halali na nimepata nafasi ya kujua kwa nini Watanzania walio wengi ni masikini ndio maana niko mstari wa mbele kupigia kelele ufisadi.
Sijui kama kuna mwana JF yeyote asiyejua kwamba Rostam ni fisadi aliyekubuhu na hili hakuna anayepashwa kuja hapa kutaka tutoe ushahidi. Wanamtetea Rostam basi wamwanbie aende mahakamani akawashtaki wale waliomwita fisadi hadharani kama Dr. Slaa na Mzee Mengi. Hiyo ya kuja hapa na kutaka mchangiaji aje na data/takwimu za watanzania wanaomchukia rostam ni hoja inayolenga kutoa nje ya mada iliyo mbele yetu.
Twambie uhusiano uliopo kati ya RA na Mohamed Enterprise basi!!!!! Mengine ya kuchukua neno moja la mchangia hoja na kulisimamia kidete, ni kutaka kupotosha hoja.
Tiba