Wafuasi wa CHADEMA na Lissu wamekuwa wakipagawa na kuota kwamba, uchaguzi wa October utawapatia ushindi na kwa mara ya kwanza toka tujipatie Uhuru nchi itaongozwa na upinzani.
Hii ni kutokana na Umati ambao umekuwa ukijitokeza kwenye kampeni za ugombea urais kwa mheshimiwa Tundu Lissu. Niwaambie wafuasi wa CHADEMA endeleeni kufurahia ngojera za mgombea wenu ila Urais mtaendelea kuusikia hadi 2925.
Sababu ya kwanza ni kwamba, watanzania wengi mnaowaona kwenye mikutano, hawajajiandikisha na hata hao waliojiandikisha, kwenye uchaguzi wa mwaka huu hawataamka kwenda kupiga hiyo kura kwa vile inajulikana wazi Mjomba Magu anarudi pale Chamwino na Magogoni.
Pili, vyama vya upinzani vyote vimeshapoteza mvuto kwa wananchi na kuikubali CCM na mgombea wake, kwa yale Serikali ya CCM iliyoyafanya na yanaonekana kwa macho na hata kuyagusa kwa mkono.
Tatu, Viongozi wa vyama vya upinzani wameshapoteza imani kwa wananchi na hasa Wasomi na waelewa wa mambo,ambao miaka michache iliyopita ndiyo tulikuwa tukiunga mkono mageuzi, kwa kuona CCM ni ya watu wasiojielewa. Kupotea kwa imani hii kumetokana na viongozi wenyewe wa vyama vya upinzani kufanya kama taasisi zao, na si za wananchi. Tazama Mbowe na Chadema, Zitto na ACT, hawana tofauti na Mzee Mrema wa TLP, au NCCR ya Mbatia.Ndiyo maana Dr Slaa aliyaona haya mapema akaamua kukaa pembeni.Chadema na wafuasi wenu msijidanganye.
Hii ni kutokana na Umati ambao umekuwa ukijitokeza kwenye kampeni za ugombea urais kwa mheshimiwa Tundu Lissu. Niwaambie wafuasi wa CHADEMA endeleeni kufurahia ngojera za mgombea wenu ila Urais mtaendelea kuusikia hadi 2925.
Sababu ya kwanza ni kwamba, watanzania wengi mnaowaona kwenye mikutano, hawajajiandikisha na hata hao waliojiandikisha, kwenye uchaguzi wa mwaka huu hawataamka kwenda kupiga hiyo kura kwa vile inajulikana wazi Mjomba Magu anarudi pale Chamwino na Magogoni.
Pili, vyama vya upinzani vyote vimeshapoteza mvuto kwa wananchi na kuikubali CCM na mgombea wake, kwa yale Serikali ya CCM iliyoyafanya na yanaonekana kwa macho na hata kuyagusa kwa mkono.
Tatu, Viongozi wa vyama vya upinzani wameshapoteza imani kwa wananchi na hasa Wasomi na waelewa wa mambo,ambao miaka michache iliyopita ndiyo tulikuwa tukiunga mkono mageuzi, kwa kuona CCM ni ya watu wasiojielewa. Kupotea kwa imani hii kumetokana na viongozi wenyewe wa vyama vya upinzani kufanya kama taasisi zao, na si za wananchi. Tazama Mbowe na Chadema, Zitto na ACT, hawana tofauti na Mzee Mrema wa TLP, au NCCR ya Mbatia.Ndiyo maana Dr Slaa aliyaona haya mapema akaamua kukaa pembeni.Chadema na wafuasi wenu msijidanganye.