Uchaguzi 2020 Lissu sema na wafuasi wako, hali ni mbaya sana

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,883
14,322
Wakuu ni matumaini yangu kuwa mu buheri wa afya , nami ni mzima kabisa .

Naomba kuzama ndani ya hoja yangu juu ya Mgombea wa CHADEMA na ACT-Wazalendo mheshimiwa sana na mwenye ilimu kuwaliko watanzania wote Mh.Tundu Lissu,huyu bwana amekuwa akiwalaghai wafuasi wake pamoja na jamii za kimataifa kuwa anakubalika sana hapa Tanzania,huku akicheza mchezo wa kuwaandaa wafuasi wake kuwa lolote litakalotokea tofauti na maatarajio /makusudio yake basi litakuwa limesababisha na tume ya uchaguzi pamoja na serikali kwa ujumla.

Kitendo cha Lissu kuwa anaituhumu Tume ya Uchaguzi mara kwa mara kisichukuliwe kuwa Lissu ni mlopokaji hapana, kina malengo makubwa Sana ambayo ni kuwafanya raia waamini kuwa Lissu anakubalika na lazima ashindwe huu uchaguzi ,ikiwa matokeo yatakuwa tofauti huyu bwana atakuwa na pakujifichia kuwa tangu mwanzo hakuwa na imani na tume ya uchaguzi hivyo kaibiwa kura zake, na yuko tayari kuwaambia wafuasi wake waandamane ili kuleta Fujo kwa kigezo cha kuibiwa kura.

Lakini pia tukio alilolifanya Lissu hivi majuzi juu ya kumtuhumu Mh. Rais Magufuli kuwa alifanya kikao cha siri na wakurugenzi ambao ni wasimamaizi wa uchaguzi nacho kisichukuliwe kuwa ni kukosa adabu kwa mgombea wa chadema la hasha ,zote hizo ni mbinu na nia ovu za Mgombea wa chadema ambaye anawaandaa wafuasi wake kisaikolojia ikiwa tu matokeo yatakuwa tofauti na mtizamo wake basi apate pa kujifichia kuwa kikao cha siri ndo kimepelekea yeye kupoteza ushindi hivyo wafuasi wake watakuwa tayari kuandamana ili kumtetea kiongozi wao.

Je, uhalisia ukoje? Uhalisia ni kwamba lissu hana mvuto tena kwa wapiga kura ,ukifanya tathimini maeneo ya vijijini ukiwaambia wakutajie wagombea wa irais wanaowafahamu, wengi wao watakutajia mh. Magufuli, Rungwe (huyu ni kutukana na Sera yake ya ubwabwa ambayo imewavutia wengi) na kwa mbali ni Prof. Lipumba.

Mwisho mbinu anazozitumia lissu kuwahadaa wagombea wake kuwa atashinda naomba atumie mbinu zile zile kuwaandaa kusikia habari ambazo zitakuwa chungu sana kwa masikio ya wafuasi wake, maana hali huku vijijini ambako CCM imekita mizizi ni ngumu sana,
 
Yani Polepole kakulipa kabisa alafu ndo unakuja kutoa utopolo wa namna hii?

Kweli mwaka huu ndo kifo cha CCM!!
 
Hebu tuambie Basi Nani anakubalika?

Je umetumia kigezo kipi?

Je wapiga kura wangapi watampigia Lissu na wangapi Magufuli?

Je Kama mgombea wako ameshashinda kwa Nini anafanya kampeni akae nyumbani asubirie apigiwe kura.

Kwa Nini unafikiri Lissu anafanya hadaa na sio wagombea wengine?

Kisa

Kuna Bwana mmoja alikua anahousegirl wake kitu chochote kikiisha nyumbani alitoa taarifa na Baba mwenye nyumba humpatia pesa kwenda kununua nahitaji yote ya familia.

Baada ya kuishi naye Yule housegirl kwa miaka 5 Yule baba akamwambia Yule house girl chukua mishahara wako uende kwenu ukapumzike maana nimepata msaidizi mwingine.

Yule housegirl akaanza Julia kwa uchungu huku anasema nimewapikia chakula miaka mitano, nimekua naenda kununua nahitaji yote ya familia, napiga deki, maisha vyombo napika, napasi Leo mmeona sifai mnataka kuleta mwingine?

Baba mwenye nyumba akamjibu, nimekulipa mishahara yako kwa kazi ulizokuwa unafanya. Lakini pia hukua unanunua nahitaji ya familia Bali Mimi ndio nilikua natoa pesa wewe kwenda kununua. Hivyo nakushukuru kwa huduma uliyotupatia lakini tunaomba uende kupumzika.

Kuna chama kinawaza sawsawa na huyo house girl.

Funzo: wenye nchi ni wananchi wanaweza muda wowote kumbadili housegirl.
 
Mada hizi mngeenda kuwalaghai huko facebook!Huwa hamna mshipa wa aibu kuandika upuuzi ili watu timamu wasome?
 
Angekuwa hana wafuasi wala msingeomba polis kubambikizia kesi wapinzani wenu kisiasa kama mlivyofanya arusha na tarime kwa heche...
 
Salum Mwalimu anaipukutisha CCM huko kusini. Sijui atapoingia mwenyewe mwamba itakuwaje.

Meko mpaka ateme damu msimu huu wa uchaguzi.
Kamanda tusijipe matumaini hewa
2426566_IMG_20200613_131913(1).jpg
 
Back
Top Bottom