digba sowey
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 7,883
- 14,322
Wakuu ni matumaini yangu kuwa mu buheri wa afya , nami ni mzima kabisa .
Naomba kuzama ndani ya hoja yangu juu ya Mgombea wa CHADEMA na ACT-Wazalendo mheshimiwa sana na mwenye ilimu kuwaliko watanzania wote Mh.Tundu Lissu,huyu bwana amekuwa akiwalaghai wafuasi wake pamoja na jamii za kimataifa kuwa anakubalika sana hapa Tanzania,huku akicheza mchezo wa kuwaandaa wafuasi wake kuwa lolote litakalotokea tofauti na maatarajio /makusudio yake basi litakuwa limesababisha na tume ya uchaguzi pamoja na serikali kwa ujumla.
Kitendo cha Lissu kuwa anaituhumu Tume ya Uchaguzi mara kwa mara kisichukuliwe kuwa Lissu ni mlopokaji hapana, kina malengo makubwa Sana ambayo ni kuwafanya raia waamini kuwa Lissu anakubalika na lazima ashindwe huu uchaguzi ,ikiwa matokeo yatakuwa tofauti huyu bwana atakuwa na pakujifichia kuwa tangu mwanzo hakuwa na imani na tume ya uchaguzi hivyo kaibiwa kura zake, na yuko tayari kuwaambia wafuasi wake waandamane ili kuleta Fujo kwa kigezo cha kuibiwa kura.
Lakini pia tukio alilolifanya Lissu hivi majuzi juu ya kumtuhumu Mh. Rais Magufuli kuwa alifanya kikao cha siri na wakurugenzi ambao ni wasimamaizi wa uchaguzi nacho kisichukuliwe kuwa ni kukosa adabu kwa mgombea wa chadema la hasha ,zote hizo ni mbinu na nia ovu za Mgombea wa chadema ambaye anawaandaa wafuasi wake kisaikolojia ikiwa tu matokeo yatakuwa tofauti na mtizamo wake basi apate pa kujifichia kuwa kikao cha siri ndo kimepelekea yeye kupoteza ushindi hivyo wafuasi wake watakuwa tayari kuandamana ili kumtetea kiongozi wao.
Je, uhalisia ukoje? Uhalisia ni kwamba lissu hana mvuto tena kwa wapiga kura ,ukifanya tathimini maeneo ya vijijini ukiwaambia wakutajie wagombea wa irais wanaowafahamu, wengi wao watakutajia mh. Magufuli, Rungwe (huyu ni kutukana na Sera yake ya ubwabwa ambayo imewavutia wengi) na kwa mbali ni Prof. Lipumba.
Mwisho mbinu anazozitumia lissu kuwahadaa wagombea wake kuwa atashinda naomba atumie mbinu zile zile kuwaandaa kusikia habari ambazo zitakuwa chungu sana kwa masikio ya wafuasi wake, maana hali huku vijijini ambako CCM imekita mizizi ni ngumu sana,
Naomba kuzama ndani ya hoja yangu juu ya Mgombea wa CHADEMA na ACT-Wazalendo mheshimiwa sana na mwenye ilimu kuwaliko watanzania wote Mh.Tundu Lissu,huyu bwana amekuwa akiwalaghai wafuasi wake pamoja na jamii za kimataifa kuwa anakubalika sana hapa Tanzania,huku akicheza mchezo wa kuwaandaa wafuasi wake kuwa lolote litakalotokea tofauti na maatarajio /makusudio yake basi litakuwa limesababisha na tume ya uchaguzi pamoja na serikali kwa ujumla.
Kitendo cha Lissu kuwa anaituhumu Tume ya Uchaguzi mara kwa mara kisichukuliwe kuwa Lissu ni mlopokaji hapana, kina malengo makubwa Sana ambayo ni kuwafanya raia waamini kuwa Lissu anakubalika na lazima ashindwe huu uchaguzi ,ikiwa matokeo yatakuwa tofauti huyu bwana atakuwa na pakujifichia kuwa tangu mwanzo hakuwa na imani na tume ya uchaguzi hivyo kaibiwa kura zake, na yuko tayari kuwaambia wafuasi wake waandamane ili kuleta Fujo kwa kigezo cha kuibiwa kura.
Lakini pia tukio alilolifanya Lissu hivi majuzi juu ya kumtuhumu Mh. Rais Magufuli kuwa alifanya kikao cha siri na wakurugenzi ambao ni wasimamaizi wa uchaguzi nacho kisichukuliwe kuwa ni kukosa adabu kwa mgombea wa chadema la hasha ,zote hizo ni mbinu na nia ovu za Mgombea wa chadema ambaye anawaandaa wafuasi wake kisaikolojia ikiwa tu matokeo yatakuwa tofauti na mtizamo wake basi apate pa kujifichia kuwa kikao cha siri ndo kimepelekea yeye kupoteza ushindi hivyo wafuasi wake watakuwa tayari kuandamana ili kumtetea kiongozi wao.
Je, uhalisia ukoje? Uhalisia ni kwamba lissu hana mvuto tena kwa wapiga kura ,ukifanya tathimini maeneo ya vijijini ukiwaambia wakutajie wagombea wa irais wanaowafahamu, wengi wao watakutajia mh. Magufuli, Rungwe (huyu ni kutukana na Sera yake ya ubwabwa ambayo imewavutia wengi) na kwa mbali ni Prof. Lipumba.
Mwisho mbinu anazozitumia lissu kuwahadaa wagombea wake kuwa atashinda naomba atumie mbinu zile zile kuwaandaa kusikia habari ambazo zitakuwa chungu sana kwa masikio ya wafuasi wake, maana hali huku vijijini ambako CCM imekita mizizi ni ngumu sana,